Saturday, August 10, 2013

NEW MNIMBO GENERAL ENTERPRISES LIMITED



NEW MNIMBO GENERAL ENTERPRISES LIMITED         

P.O BOX 105018  Dar es Salaam Tanzania 
Cell: 0767 203691   / 0784 20369   /  0719 965074 / 0754 309346



                                                          COMPANY -PROFILE 

new  mnimbo General Enterprises Limited  was established in 2011. It is situated in Temeke district Dar es Salaam .  New  mnimbo General Enterprises Limited has a reputation for its reliability of server delivery in engineering and fabrication industries. New Mnimbo General Enterprises supply precision tooling to the industries including Verniers standard, Dial and digital and specialized gear tooth micrometers standards and Digital and specialized.

Thread and bore, cutting tools including High speed steel and amp ; Solid carbide power saw Blades.

New Mnimbo General Enterprises Limited also supply a variety to tungsten carbide inserts to the manufacturing. New Mnimbo General Enterprises Limited tools include General hand tools, Workshop tools in including Hydraulic pneumatic and mechanic maintenance and  power tools.

PRODUCT & SERVICES 

>eletrical power transformers
>fasteners, bolt nuts ,rivets & washers 
> firefighting & rescue equipments
>footware
>General Eletrical Equipment 
>Greases
>Hose Fittings 
>Lifting taccle & attachment
>Hydralics & Pneuamatics 
>Machine tools 
> Material Handling Equipment 
> Non- Ferrous metals 
>.power tools
>Pulleys 
>Pumps 
>Safety Equipment & Clothing 
.>Tool die & Drill Steel
>Washing, Screening & Cleaning Plant Equipment 
>Welding & Flame cutting equipment
>Wire ropes & steel cables 
>Hardware
>Adhesives
>bearing 
>belting require sites
.>Boilers , steam generators & super heaters


SHEIKH APIGWA PANGA SWALA YA IDD



na Ibrahim Yassin

 SHEIKH Mkuu wa Wilaya ya Kyela, mkoani Mbeya Nuhu Mwafilango, ameshambuliwa na kujeruhiwa kwa panga baada ya kuzuka kwa vurugu katika msikiti mkuu wa wilaya ya Kyela. Vurugu hizo zilisababisha kujeruhiwa vibaya kwa watu wengine watatu baada ya kushambuliwa kwa mapanga na visu.

 Mashuhuda wa tukio hilo wameiambia Tanzania Daima kuwa vurugu hizo zinazoaminika kuwa ni za kugombea madaraka, zilizuka majira ya saa mbili asubuhi jana wakati sheikh huyo akiongoza ibada ya Idd el Fitri katika msikiti huo. Imedaiwa kuwa kundi la vijana likiongozwa na mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari ya kutwa ya Kyela (jina limehifadhiwa) alimshambulia kiongozi huyo kwa panga na kusababisha vurugu kubwa.

 Imeelezwa kuwa kikundi hicho cha vijana ambao baadhi yao wanadaiwa kukodiwa kutoka katika misikiti ya mikoa jirani, wakiwa na mapanga, nondo na visu walianza mashambulizi hayo, na ndipo wakakumbana na hasira za waumini wengine waliokuwa wamejiandaa kukabiliana na mashambulizi hayo. Mmoja wa vijana waliojeruhiwa vibaya kichwani ametajwa kwa jina la Hamis Hussein ambaye alipambana na vijana walioanza kumshambulia sheikh huyo. Imedaiwa kuwa kulikuwa na fununu za kuzuka kwa mapigano hayo, hatua iliyofanya uongozi wa msikiti kutoa taarifa polisi ambao walijipenyeza katika swala hiyo ya Idd.

 Wengine waliojeruhiwa vibaya ni mmoja aliyetajwa kwa jina la Magogo anayetuhumiwa kuchochea vurugu na mapigano hayo katika kile kilichoelezwa jitihada za kuwaondoa viongozi walioko msikitini na kuwadhamini vijana ambao wanadaiwa kuwa ni waasi wa msikiti huo.

Akizungumza na Tanzania Daima Mwenyekiti wa BAKWATA Wilaya ya Kyela Daud Mwenda alisema kuwa kikundi hicho kinapingana na uongozi uliopo msikitini hapo hivyo wanataka kushinikiza waumini wengine waupindue uongozi uliopo. Mganga wa zamu katika Hospitali ya Wilaya ya Kyela ambaye hakutaka kutaja jina lake alikiri kupokea majeruhi watatu waliotokana na vurugu hizo. Kwa upande wake Afisa Tarafa ya Unyakyusa Helly William alisema kuwa ofisi yake imepokea taarifa za vurugu katika msikiti huo na kudai kuwa jambo hilo limewasikitisha sana kama viongozi wa serikali.

William alisema msikitini sio mahali pa kufanyia vurugu bali eneo takatifu linalotumiwa na watu kumuabudu Mungu.
RESPECT TANZANIA DAIMA

Friday, August 9, 2013

BREAKING NEWS:::: MILLIONI 10 KWA ATAKAE FANIKISHA KUKATWA KWA WAHUSIKA WA TINDIKALI ZANZIBAR......





Polisi nchini Zanzibar wameahidi kutoa zawadi ya shilingi milioni 10 za Tanzania kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazopelekea kukamatwa kwa watu waliowashambulia wasichana wawili waingereza kwa Tindikali.
Wasichana hao kutoka London, Kirstie Trup na Katie Gee, walirushiwa Tindikali kwenye nyuso zao walipokuwa wanatembea mjini Jumatano Jioni.

Polisi wanasema kuwa hizo ni pesa nyingi sana kisiwani Zanzibar.
Serikali ya Zianzibar ndio itakayotoa zawadi hiyo.
Kirstie Trup na Katie Gee, wote wenye umri wa miaka 18 kutoka London, walipelekwa hospitalini nchini Tanzania baada ya kushambuliwa Mashariki mwa kisiwa hicho.
Inaaminika kuwa walitoka Tanzania kuelekea Uingereza Alhamisi usiku.
Mama za wasichana hao, Rochelle Trup na Nicky Gee, walielezea kughadhabishwa mno na shambulizi hilo ambalo sababu yake haiwezi kujulikana na ambalo halikuchochewa kivyovyote. Walishambuliwa na wanaume wawili waliokuwa kwenye pikipiki.
Polisi walisema kuwa walirushiwa Acid kwenye nyuso zao, kifuani na kwenye mikono yao walipokuwa wanatembea mjini .
Mwandishi wa BBC anasema kuwa waliowashambulia walitoroka na polisi hawajui kwa nini wanawake hao walilengwa.
Mama za wasichana hao walisema kwenye taarifa yao kuwa walighadhabishwa mno na shambulizi hilo na hawaelewi kwa nini wasichana hao walishambuliwa ili hali walikwenda Zanzibar kwa nia njema.

'Tunashukuru kwa wale wanaotaka kujua kinachoendelea lakini tungeomba vyombo vya habari vituwache kwa sasa hadi tutakapokutana na watoto wetu,'' alisema msemaji wa familia za wasichana hao.
Wasichana hao walikuwa wamekaa Zanzibar kwa muda wa wiki mbili ingawa walitarajiwa kuwa huko kwa wiki tatu, kupitia kwa kampuni ya usafiri ya i-to-i Travel, ambayo ilisema inafanya kila iwezalo kuwarejesha nyumbani Uingereza.
Kari Korhonen, mkurugenzi mwenza wa kampuni ambayo wasichana hao walikuwa wanafanyia kazi, alisema kuwa hali yao si mbaya ikizingatiwa athari za Acid kwa mwili na visa ambavyo vimewahi kushuhudiwa vya kuchomwa kwa Tindikali
Msemaji mwingine aliongeza kuwa wasichana hao walikuwa njiani kuelekea kwa maankuli ya jioni wakati wa shambulizi hilo.

Thursday, August 8, 2013

HII KALI: WANAUME WA KIAFRIKA WANAONGOZA KUWA NA UUME MKUBWA....





Kwa sababu ambazo binafsi sizielewi, mwanasayansi mmoja kutoka nchini Ireland aliamua 

kufanya “utafiti” wa kulinganisha wastani wa ukubwa wa uume wa watu wa nchi mbalimbali. Alifanya utafiti huo kwa kulinganisha mataifa 113, ambapo wanaume wa Afrika ndio waliongoza kwa ukubwa na Waasia walikua wa mwisho.


Utafiti huo ulifanywa na Profesa wa saikolojia, Richard Lynn, wa Chuo Kikuu cha Ulster na utachapishwa katika jarida la kisayansi la Personality and Individual Differences. Profesa huyo alisema matokeo ya utafiti wake yamethibitisha nadharia ya awali kuhusu mahusiano ya urefu wa uume, ya kwamba Negroids(watu weusi) ndio wanaoongoza kwa ukubwa wa wastani wa uume, na Mongoloids (Waasia) ndio wana wastani mdogo kuliko watu wote.


Top 4 kati ya nchi zote 113
1. Congo ndio wanaoongoza kwa urefu wa wastani wa uume ambao ni inchi 7.1
2. Ecuador kwenye wastani wa inchi 7.0, 
3. Waghana inchi 6.8; na 
4. Raia wa Colombia inchi 6.7.


Katika wanaume wa Ulaya, 
1. Wataliano ndio walioongoza na wastani wa inchi 6.2
2. Ugiriki inchi 5.8 
3.Ujerumani inchi 5.7
4. Waingereza inchi 5.5 , na 
5. Wafaransa, inchi 5.3
Walioongoza kwa udogo katika mataifa yote yaliyofanyiwa utafiti ni Korea zote mbili (Kaskazini na Korea ya Kusini) ambao wote kipimo chao, ni wastani wa inchi 3.8. 
Swali je Tanzania tupo wangapi?


USHAHIDI

DIVA WA CLOUDS FM TENA......... "SIJAWAHI ONA MWANAUME MZURI KAMA PREZZO HAPA DUNIANI"

Kwa  mara  nyingine  tena,  mtangazaji  wa  Clouds fm  maarufu wa  jina  la  DIVA  amejitosa Istagram  na  kuanza  kuisifia  suruali yake ( Prezzo)  huku  akiwaponda  wanaume  wa  kibongo  na  wale  wote  wanaomchukia  Prezzo....


HUU NDO UJUMBE WAKE KWENU

“The way my heart beats for u Mentiond of your name, One touch never enough you driving me Insane, swing me take you back, who am i to blame but myself, need you back in my life simple and plain, Crazy nights arguments running towards the door, lying to myself that I don’t wanting you no more. 


"No matter what we been through You’re the only man that I adore… you are the only one I need in this world.. see People use to tell me I was Crazy, told me not to give in, told me that you would never love me all I did is pretend.

"I told them to mind their business Cause they are not in my Position… when I said I was in love… they said with that UGLY face ‘ girl you tripping… 

"I cut the negativity cut the haters off and I got into my man… coz I take him for all he is.. and he takes me as I am. 


"The way I feel about him is God’s Perfect plan. Everyone know I am his girl……he is the Only One I need. habari ndio hiyo. Sibadiliki and haachwi mtu.”

EID MUBARACK...................

Team Truth inawatakia Watanzania wote Eid MUBARACK AMANI NA UPENDO VIWATANGULIE WOTE..........

Wednesday, August 7, 2013

NGOMA MPYA: MABESTE ft PETER MSECHU - NISHAURI DOWNLOAD HAPA

DOWNLOAD HAPA

SABABU ZA KIBIASHARA ZAIHAMISHIA BONGO STAR SEARCH (BSS) TBC1!!!!!!

Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1. 


Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1.


“Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1. 


Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”

Monday, August 5, 2013

18+ NDANI YA DARASA HURU: KWA VIGEZO HIVI KIDUME UTAPENDWA TU!!!!!!!!!!!!





Jana kulikua na kikao cha dharura na cha ndani ya TEAM TRUTH ambapo moja ajenda ilikua ni kunipongeza mimi (TEAM TRUTH 18+) kwa kazi nzuri ninayo ifanya na kwa ratiba ilikua nimalize session hii ya mapenzi jumatatu ila nikapewa muda zaidi hivyo kuamua leo kudondoka na hii kwa ajili ya mabrother wenzangu............................


watu wengi wamekua wakitafuta jinsi gani wanaweza kupendwa na wasichana au wanawake na ni wazi kila mwanamke ana chaguo lake kwa mwanaume ampendae huendaa ukawa na vigezo kibao na bado akapenda vigezo vichache na ukabaki unashangaa why kantosa?

KWA MSAADA TEAM TRUTH 18+ NIMEAMUA KUDONDOKA NA VIGEZO 10 AMBAVYO NI KIVUTIO KWA WASICHA AU WANAWAKE WENGI.....................................................

wengi watajiuliza why not pesa? jibu ni rahisi sana imetokea mara nyingi mtu akapendwa tu bila kujali pesa na watu pia wakashangaa mbona hata sura hana? mchunguze mtu huyu kuna kigezo lazima kakuzidi na ukikigundua BELIEVE ME YOU WILL ALWAYS STAY CONNECTED WITH GIRLS!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

1) kuwa na malengo yote ya muda mfupi na mrefu katika maisha yako na misimamo isiyo tingishika.

2) mwenye kujiamini.

3)mwenye kutunza siri na si mropokaji ovyo.

4) mcheshi (na hii kivutio kwa wasichana walio wengi)

5) hisia na uadilifu.

6) mwenye kusamehe tena na kusahau.

7) mwenye kujithamini.

8) mwenye utashi na upeo wa mambo.

9) huruma na heshima kwa wote wadogo na wakubwa

10) mwenye hadhi na mtanashati katika mambo yake ikiwemo uwezo binafsi wa upembuzi wa mambo.


Sunday, August 4, 2013

18+ NDANI YA DARASA HURU; USAGAJI (lesbianism) KWA WANAWAKE NA SABABU ZAKE. (VERY SENSITIVE IN TANZANIA HASA KWA MASTAAA)


SAMAHANI KWA PICHA HII

Usagaji (lesbianism) ni tabia ya wasichana/wanawake kujiridhisha kimapenzi wenyewe pasi kuhitaji kuridhishwa na mwanaume. Wasichana hawa hutumia vidole, ulimi na hata sex toys (dildo) kama zana wakati wa kufanya tendo hilo. Wengi wa wasichana wanaojihusisha na tabia hiyo hufurahia zaid tendo hilo tena kuliko hata wakifanya na wanaume na hivyo kuwafanya wajione kwamba hawana sababu ya kuwa na partners wa kiume. Zifuatazo hapa chini ni sababu ambazo kwa mtazamo wangu ambazo naziona ndio sababisho la wasichana wengi kujiingiza kwenye tabia hii na hata kuona ndiyo maisha yao.
Sababu hizo kwa mtazamo wangu ni hizi hapa

• Kuiga kutoka kwa wenzao: wengi wa wasichana ambao wamejikuta wanatabia hii wameiiga kwa wenzao, hasa wanapokuwa kwenye eneo ambalo wapo wenyewe kama vile shule hasa za bweni na maisha ya hosteli. Wasichana wengi ambao walisoma shule za bweni ama kuish maisha ya hosteli walijikuta wanafundishwa tabia hii na wenzao ambao tayari walikuwa wameshaanza tabia hizi toka kabla ya kuja shule. 


 Kutaka kujiexplore: kwa kawaida watoto hupenda kujiexplore viungo vyako, yaani watoto wakiwa wadogo hutaka kujidadisi wawe wa kiume ama wa kike. Mfano mzuri watoto wa kiume wanapokuwa pamoja hata wakioga hujikuta wanachezeana sehem zao za siri hadi uume unasimama, like wise watoto wa kike hupenda kujidadisi kwa kucunguliana sehem zao za siri. Tabia hii kwa umri wa udogo huwa haina neon manake khuishia hapo lakini wapo wachache ambao tabia hii hawaiachi huiendeleza hadi ukubwani na hivyo kuwa ni sababisho la kujiingiza kwenye same sex plays.

• Hormonal make up: hii hutokana na jinsi binti alivyzaliwa. Kuna baadhi ya mabianti ambao wamezaliwa na hormone za kiume na hivyo kujikuta kwamba wanatabia za kiume. Wengi wa mabinti ambao wana tabia hizi kwenye mashule ya bweni huwa na desturi ya kuoa na hivyo kuitana mume na mke na wao huwa na tabia za kukaa kimapenzi mapenzi na hwa wanaowaita waume ama wake. Wasichana kama hawa huweza kuwashawishi sana wale ambao ni wasichana wa kawaida hadi kujikuta wanaanza tabia hii ya kusagana wakiwa mashuleni na wakisha ianza basi huwa siyo rahisi kuiacha mpaka nguvu nying zimetumika kumfanya aache.


• Raha itokanayo na tendo lenyewe: wengi wa wasichana /mabinti wanaoshiriki tendo hili huwa wanadai wanaridhika sana kimapenzi wanapofanya hivi ukilinganisha na wakiwa wanafanya na wanaume. Kutokana na tabia hii wengi wa wanwake ambao wako kwenye mahusiano ya kindoa hujikuta wanafanya hii tabia ili tu kuridhika kwasababu wanapofanya na jinsia ya kiume hawaridhiki.

• Maudhi ya mahusiano ya heterosexual, maudhi yatokanayo na mahusianoa ya jinsia mbili huwa yanawakinai wengi wa wasichana/ wanawake na hivyo kugeukia upande wa pili ambapo wanaamini kwamba hakuna maudhi hayo. Wanajua wazi kwamba wakiwa wenyewe watabembelezana, na kupeana raha zisizokuwa na maudhi.



• Umbali kutoka walipo wenzi wao: kuna tabia ambayo imeibuka siku hizi na kwa masiksitiko makubwa sana inafanywa na wanawake ambao wenzi wao wako mbali nao. Baadhi ya wanawake ambao waume zao wako mbali nao kwa mauda mrefu wamejikuta wakiwa na mahusiano na jinsia moja kwa kigezo kwamba hawataki kuwasaliti waume zao. Na kwamba wanataka waume zao wakirudi wawakute hawajatumika kabisa. Sikatai usaliti ni mbaya lakini hata huu wa jinsia moja nao ni usaliti tu.

Ikumbukwe kwamba mahusiano ya jinsia ya aina moja haimaaniash kwamba hayana maambukizi ya magonjwa kama HIV/AIDS and the like hivyo yeyote anayefanya hivi kwa kigezo kwamba anataka kujikinga na magonjwa anajiongopea na kwamba chances za infection huwa kubwa tu.


Pia ni kujidanganya sana kusema kwamba mapenzi ya jinsia moja ama ya usagaji ni matamu sana kwani huwa mwanaume akifundishwa kufanya kama vile ambavyo mwanamke msagaji anaweza kufanya basi mapenzi haya yatakuwa na raha kama kawaida. Haina maana kwamba mwanamke tu ndio anayeweza kutumia ulimi wake ama kidole chake ili kumpatia mwenzie raha, ila hata mwanaume pia anaweza kutumia vitu hivi na hivyo kumpatia raha mwenzie.

Pia tabia hii ya usagaji kwa wale ambao wanaifanya hasa pale waume zao wanapokuwa safarini, eti kisa wanataka waume wakirudi wawakute hawajazini wanajidaganya sana kwani kusagana na kuzini kwa kawaida kote ni kuzini hata kama hukuingiziwa kitu ndani ya uke. Kinacho determine kutokuwa mwaminifu ni kitendo cha usaliti iwe umezini na mtu mume ama mwanamke mwenzio. Hivyo usidanganye nafsi yako kwamba huwez kuzini na mwanaume kisa utamsaliti mumeo, ukasahau kwamba hata na huyo mwanamke mwenzio pia ni usaliti.

reference

Saturday, August 3, 2013

18+ NDANI YA DARASA HURU : SABABU KUU ZA MWANAMKE KUKOSA HAMU YA KUFANYA TENDO LA NDOA / MAPENZI (KUJAMIIAANA)

Matatizo ya kufanya mapenzi au kujamiana kwa wanawake yanatambulika kama tatizo linalojirudia kwa muda mrefu ambapo huathiri mzunguko wa tendo la kujamiana (kusisimka, kufikia kilele, kurudia) na hivyo kusababisha msongo wa mawazo au kuharibu uhusiano wa mwanamke na mpendwa wake. Tatizo hili huathiri asilimia 43 ya wanawake wa rika zote duniani na huonekana sana kwa wanawake wenye umri kati ya 45-64.
Visababishi vya tatizo hili kwa wanawake ni;

  • KUSAGANA AU MAPENZI YA JINSIA MOJA KWA WANAWAKE.

  • Msongo wa mawazo – Asilimia kubwa ya tatizo hili linaweza kutokea kutokana na msongo wa mawazo ambapo huchangiwa na ugumu wa maisha (uchumi), matatizo katika uhusiano (ugomvi, kutoelewana, kutoaminiana au kukosa uaminifu katika uhusiano {infedility} nk) na magonjwa mbalimbali.
  • Kupungua au kukosekana upendo/mapenzi katika uhusiano au ndoa
  • Kujifungua mtoto – Hii ni kutokana na homoni aina ya prolactin kuwa katika kiwango cha juu wakati mama ananyonyesha, homoni hii pia hufanya kazi ya kumfanya mtu kuridhika baada ya tendo la ndoa/kujamiana kwa kuingiliana na ufanyaji kazi wa homoni/kichocheo chengine kinachojulikana kama dopamine (ambayo ndio humfanya mtu kufikia kilele wakati wa kujamiana). Mbali na kunyonyesha, homoni ya prolactin pia huongezeka wakati mtu amelala (usingizi mzito au REM sleep), wakati wa alfajiri, baada ya kufanya mazoezi, kula,baada ya tendo la kujamiana, baada ya upasuaji mdogo na hata baada ya kupata degedege. Sababu nyengine ya kuongezeka kiwango cha kichocheo hiki cha prolactin ni kuwa na saratani katika ubongo (anterior pitituary tumors). Dalili za saratani hii ni pamoja na kutonyonyesha vizuri kwa mama, kukosa hedhi, ugumba kwa wanawake na uhanithi kwa wanaume(impotence).
  • Kupungua mzunguko wa damu katika tupu ya mwanamke na hivyo kusababisha maumivu wakati wa kujamiana.
  • Hypothyroidism – Matatizo ya homoni ya tezi la koo, huonekana sana kwa wanawake kuliko wanaume.
  • Utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi au vya majira kwa muda mrefu
  • Unywaji pombe kupindukia – Kinyume na fikira potofu za watu wengi ambao huamini kwamba unywaji pombe kali huongeza hamu ya kujamiana au kupunguza uzito lakini ukweli ni kwamba pombe kali au kilevi cha aina yoyote hupunguza hamu ya kujamiana na pombe huongeza uzito na kusababisha utapia mlo.
  • Ugonjwa wa kisukari
  • Uvutaji sigara
  • Ujauzito – Kutokana na mabadiliko katika mfumo wa homoni au vichocheo wakati wa ujauzito, na pia kutokana na mabadiliko ya maumbile ya wanawake wakati huu na hivyo kuchangia kutojiamini kwa mwanamke.
  • Uzito uliopitiliza (obesity)
  • Ugonjwa wa mifupa (arthritis)
  • Utumiaji madawa ya kulevya
  • Madhara katika neva inayohusika na kuongeza msisimko wakati wa kujamiana (pudendal nerve damage) wakati wa upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi kwa mwanamke mwenye matatizo ya uzazi au katika mfuko wa kizazi.
  • Madhara ya dawa – Kama dawa za kutibu shinikizo la damu,antidepressant medication, dawa za saratani nK.
  • Uchovu – Kuzidiwa kwa mwanamke na majukumu ya kulea mtoto/watoto, kazi na kumhudumia mume wake hivyo kusababisha uchovu.
  • Ugonjwa wa moyo
  • Saratani ya aina yoyote ile
  • Kuwa na wasiwasi (anxiety), depression nk.
  • Historia ya kubakwa, au kupata maumivu wakati wa kujamiana hapo awali kutokana na mwanamke kutokuwa tayari kujamiana au kutotayarishwa vyema kabla ya kujamiana au magonjwa ya zinaa.
  • Tatizo la vaginismus – Hii ni tatizo ambalo husababisha tupu ya mwanamke kuwa ndogo wakati wa kujamiana na hivyo husababisha mwanamke kupata maumivu wakati wa kujamiana.
  • Kupenda intaneti kupita kiasi (addiction) – Katika tafiti mpya iliyofanyika mwaka huu nchini marekani, imeonyesha ya kwamba kati ya ndoa 6,000 zilizovunjika asilimia 57 zimesababishwa na mwenza mmoja au wote kupenda kuchat au kutumia intaneti kupita kiasi na hivyo kusababishwa msisimko kupotea kati ya wenza wawili na hatimaye mwisho ni kupungua uwezo au hamu ya kujamiana.
Ni kundi gani la wanawake lililo katika hatari ya kukumbwa na tatizo hili?
  • Wanawake ambao wana historia ya kupungua hamu ya kujamiana
  • Wale ambao wamefanyiwa upasuaji wa kuondoa mayai yao ya uzazi kutokana na sababu mbalimbali
  • Wanawake ambao waliofika umri wa kuacha kupata hedhi (menopause- miaka 42-58)) na kupata dalili mbalimbali kama kutokwa na jasho usiku, kukosa usingizi mzuri nadepression.

Friday, August 2, 2013

18+ NDANI YA DARASA HURU: MADHARA YA UPIGAJI PUNYETO




ATHARI za PUNYETO
Wanaume waliowengi hukidhi haja zao kwa kutuliza matamanio yao kwa njia ya kujichua/ kupiga punyeto bila kufahamu madhara yake: Nikweli punyeto inasaidia kupunguza hamu ya tendo na ni njia nzuri ya kujiepusha na zinaa kwa kujilinda na maradhi ila kiukweli ina madhara na madhara yake mara nyingi hutokea kwa mtu anaependelea sana kupiga punyeto, kutokana na utafiti uliofanywa kisayansi imeonekana punyeto ni nzuri kiafya ila endapo kama utakuwa unapiga mara moja moja na sio kila siku. Napenda kuwashauri watu wanaopiga punyeto wawe makini na wasiendekeze jambo hili kwani madhara yake ni makubwa sana na Athari zake kubwa ni hizi zifuatazo:

1. PUNYETO INAUA NGUVU ZA KIUME:
Upigaji wa punyeto unaweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, kwani kipindi unapiga punyeto jua ile mishipa inayofanya uume usimame unakuwa unaichua na uume unakuwa umesimama kwa muda mrefu sasa ikitokea ukawa unafanya hivi kila siku ile mishipa inaregea na uume unakuwa unakosa nguvu hata ukisimama haui strong unakuwa kama umeregea.

2. KUWAHI KUMALIZA MAPEMA KATIKA TENDO:
Mara nyingi mtu aliezoea kupiga punyeto huwahi kumaliza mapema pindi akiwa anafanya mapenzi na mpenzi wake na wakati mwingine uume hushindwa kusimama kwa mara ya pili na kujikuta anashindwa kurudia tendo ikiwa mpenzi wake bado hajaridhika na anahitaji kuendelea kusex.

Athari nyingine ni kama zifuatazo 

3.Uchovu wakati wote 
4.Maumivu ya nyonga 
5.Kusinyaa kwa Nywele/Nywele kunyonyoka 
6.Maumivu ya kende 
7.Maumivu ya kiuno 

Mpendwa wa safu hii hizo ni athari kuu 2 tu, ingawa ziko nyingi ila hizi nilizozitaja ni kwa uchache na ndio zinazo wakumba wanaume walio wengi. Ushauri wangu mimi kama wewe unapiga punyeto basi jitahidi usiwe unapiga kila siku atlist kwa wiki mbili mara moja endapo kama utajisikia hamu ya kusex kama huna mpenzi au ukishindwa acha kabisa.

Thursday, August 1, 2013

SOMA NI MUHIMU SANA SANA NA INASIKITISHA: KANSA YA NGOZI YAMHARIBU MTOTO WA MIAKA 7 VIBAYA SANA....

MTOTO Ashura Mustapha (7) mkazi wa Mwandege, wilayani  Mkuranga, Pwani anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya ngozi tangu akiwa na mwaka mmoja.

Akizungumza na mwandishi wetu, baba mzazi wa mtoto huyo, Mustapha Makombe alisema: “Mwanangu anateseka sana jamani, ugonjwa ulianza kama malengelenge akiwa na umri wa mwaka mmoja tukawa tunakwenda hospitali ndogondogo lakini baadaye tukaamua kumpeleka Muhimbili ambapo tulipewa barua ya kutuelekeza kwenda CCBRT, kule ndipo wakagundua mwanangu ana kansa ya ngozi steji ya nne.




“Baada ya kuhangaika katika hospitali nyingi bila mafanikio, nikaamua kwenda Hospitali ya Regency (Dar) kuomba msaada wa kwenda kutibiwa India.

“Pale waliniambia nichangie shilingi milioni moja na laki tano kwa ajili ya tiketi na viza ili mwanangu akatibiwe India, hizo hela mimi sina. Naomba Watanzania mnisaidie hata kwa fedha za mitandao kwa namba 0769 517765 na 0715 424697 ili niweze kumpeleka mwanangu India akatibiwe,” alisema baba mzazi. 

REFERENCE

JOINT MPYA: OMMY DIMPOZ ft J MARTIN - TUPOGO DOWNLOAD IT HERE

DOWLOAD IT HERE

NU JOINT: NEY WA MITEGO ft NEYBA - SALAMU ZAO............. DOWNLOAD

DOWLOAD HAPA

Wednesday, July 31, 2013

KUELEKEA UCHAGUZI 2015: SHEIKH PONDA ISSA PONDA APENDEKEZWA KUGOMBEA URAIS





Ikiwa  imebakia  miaka  miwili  kabla  ya  kufanyika  kwa  uchaguzi  mkuu wa  Rais  na  wabunge  hapa  nchini,baadhi  ya  waumini  wa  kiislamu  wameanza  kupendekeza  wagombea  wa  urais  wanaoona  kuwa wanafaa  ambapo  jina  la Sheikh  Ponda Issa Ponda  limeongoza....

Mapendekezo  hayo  yamedhihirika   katika  mihadhara kadhaa  anayoifanya Ponda  katika  mikoa  mbalimbali  nchini,ambako  amekuwa  akipendekezwa  na  kushauriwa  na  waumini  agombee  nafasi hiyo.....

Walianza  waumini  wa  msikiti  mkuu  wa  Ijumaa  wa  Arusha  alipokuwa  kwenye  ziara  mkoani  humo  ambapo  muumini  mmoja  alisimama  na  kusema  kwamba  kwa  mawazo  yake  anaona  Ponda  anafaa  kugombea  nafasi  ya  urais  kwa  vile  anaamini  kuwa  uwezo  wa   kuongoza  anao..

Alisema  mbali  na  uwezo pia  yuko  makini  katika  kusimamia  jambo lolote  lenya  maslahi  kwa  waislam  na  kwamba  mtu  wa  namna  hiyo  atafanya  vyema  zaidi  akipewa  dhamana  ya  kuongoza  nchi....

Inaelezwa  kuwa Ponda  alipotembelea  Zanzibar  alipata  wakati  mgumu  wa  kuwakataa  waislam  waliojitokeza   kumlaki  katika  misikiti  ya  Mpendae na  Mbuyuni  ambako  alifanya  mihadhara  na  kupendekezwa kugombea  urais  kwa  kura  nyingi  na  waumini  ....

Kufuatia  kusikika  kwa  mapendekezo  hayo,Kisiwa  lilimtafuta  Ponda  ili  kusikia  maoni  yake  juu  ya  maombi  ya  waislam  kumtaka  agombee  urais.

"Sikuwa  na  fikra  hiyo  hata  mara  moja,lakini  maadam limeletwa  nami  ni  kiongozi  wa  taasisi  ninawashukuru  waliofikiria  hivyo...

"Kwa  sasa  siwezi  kuzungumza  lolote  kuhusu  hilo, ntalifikisha  katika  taasisi  na  maulana  ndio  watakaolitazama  na  kutoa  uamuzi." Alisema  Sheikh Ponda

Ponda  alisema  kuwa  inawezekana  waumini  wakawa  na  mtazamo  huo  lakini  viongozi  wakawa  na  mtazamo  tofauti  kabisa,hivyo  akawataka  waumini  kuwa  na   subira  katika  hilo.


REFERENCE

DOWLOAD NEW AND BRAND HIT........... MAKOMANDO - KIBABAA


DOWNLOAD HAPA

SIKILIZA NA DOWNLOAD NEW HIT.... COUNTRY WIZ ft G- NAKO - WATCH ME MASTERING

INGIA HAPA KUDOWNLOAD

NEW MUSIC: DOWNLOAD..... ADAM MCHOMVU - AU SIO

INGIA HAPA KUDOWLOAD

Tuesday, July 30, 2013

SOMA MUHIMU SANA.............BIDHAA 48 HAZITAKIWI SOKONI TBS IMETHIBITISHA.




Shirika la Viwango (TBS) limetangaza orodha ya bidhaa 48 ambazo hazitakiwi kuwepo sokoni kutokana na muda wa kuitumia nembo ya kampuni hiyo katika bidhaa zao kumalizika na wahusika kushindwa kuwasilisha bidhaa zao kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuruhusiwa tena.

Hatua hiyo ya TBS inatokana na watengenezaji wa bidhaa hizo ambazo awali zilithibitishwa na TBS na kuruhusiwa kutumia nembo yao hiyo ya ubora kumalizika na wahusika kushindwa kuwasiliana na shirika hilo kwa ajili ya uhakiki wa bidhaa zao hizo.

Ofisa Uhusiano wa TBS, Rhoida Andusamile aliliambia Mwananchi kuwa bidhaa hizo kuanzia hivi sasa hazitakiwi kuonekana sokoni na msako utaanza wakati wowote kuziondoa na zile ambazo zitakamatwa wahusika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Tumetoa tangazo lakini kabla ya hapo tuliwapa muda wawe wameleta bidhaa zao kwa ajili ya kuhakikiwa kabla ya kuruhusiwa kuendelea kutumia nembo yetu,akini wamekaidi ndio maana tumewatangazia kama utaratibu unavyoagiza” alisema Rhoida.

Bidhaa ziliazoainisha katika tangazo hilo ni pamoja na 
majina ya watengenezaji /wasambazaji katika mabano ni pamoja na karatasi laini ‘tissue’ za Alawi Supplies ya Zanzibar, Milk Marie Biscut za Britania, Maji ya Great Zone, Mishipi na nyavu za kuvulia samaki za Imara Fishnet, maji ya Raha na fulana za Kibo Trade.


Bidhaa zingine ni matofali ya GM Gross, taulo za watoto za Hengan Sanitary, baadhi ya rangi za Chui, beteri za Dry Cell, magodoro ya Jumbo foam, sabuni za Mbasira Investment ya Shinyanga, mifuko ya plastiki ya Centaza na mafuta ya kupikia ya Sun Flower Seed (Sun Shine) na korosho zinazosambazwa na Frabho Enterprises.

Pia taulo za wanawake za Sythentic Detergent (ARIEAL) za Procter&Gambler, mifuko ya B-Twill Jute na A-Twill, mifuko ya plastiki ya Tropical, mafuta ya kupikia ya Sun Flower ya A TO Z Oil Mills, Korosho za Munawar ya Mbeya, Sabuni za kunawia za Brite Chemicals, pipi, lawalawa, mipira ya kutafuna ya rangi mbili.

Vilainisha vya injini (Saud Oil) za Star Composed, betri za 777 kutoka China, maji ya kunywa ya Shia yanayotengenezwa na Siha Beverage, mtindi wa Morani Dairy ya Tanga, pikipiki za Star Shineray, vigae vya Mbezi, sabuni ya Liquid Detergent, mbao zilizotiwa dawa za Mombo, Jam iliyochanganywa ya Les Group ya Musoma.

Orodha hiyo pia inataja Jusi za nanasi za Unnat Fountain ya Morogoro, Maji Uluguru, springi za magari za kampuni ya TASIA, Gypsum zinazotengenezwa na Tanzania Gypsum ya Dar es Salaam, Maji ya Uzima, magodoro ya Plyfoam,Mvinyo wa nanasi wa Kivumbui ya Arusha na mabati ya RD Roofing & Wire Product.

Bidhaa zingine ni unga wa sembe wa Kweniml ya Machame Kilimanjaro, boriti za Ravji Manufacturing, mafuta ya breki za magari ya Automotive Packed ya Dar es Salaam, maJi ya kunywa ya AAMFA, pikipiki za Foshan Fost za China na mvinyo wa matunda wa Victoria Food Product ya Mara pia Jibini, mtindi na maziwa ya Kyaka Milk Processing , Sabuni za kufulia za Jamii za Kampuni ya Mbasira ya Shinyanga.