Saturday, August 17, 2013

UNYAMA ULIO KITHIRI:::::::: MWANAMKE ABAKWA NA KUCHOMEKWA KISU SEHEMU ZA SIRI HUKO SHINYANGA

mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 30 amekutwa amekufa katika makaburi ya Majengo soko la mjini Kahama mkoani Shinyanga huku mwili wake ukiwa ametobolewa macho na kuonesha kupigwa na kitu kizito usoni.
Mwanamke huyo ambaye hajatambulika jina lake na anakotoka alikuwa amevaa Blauzi nyeusi yenye madoa meupe, viatu vyenye urembo wa silva, mnene kiasi, mweusi na mwenye nywele ndefu.

Mwili wa Mwanamke huyo amegunguliwa leo majira ya saa sita Mchana baada ya watu waliokuwa wanachimba kaburi kuuona mwili huo pembeni ya eneo hilo na kutoa taarifa Polisi.
Kwa mujibu wa majirani wanaoishi eneo la makaburi hayo, tukio hilo linakisiwa kutokea usiku wa kuamkia jana huku baadhi ya kina mama wakisema kuwa walisikia sauti ya mwanamke akipiga mayowe katika eneo la mnadani.
 
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha Majengo  Kaskazini Noel Mseven amesema amepata taarifa kutoka kwa wananchi na baada ya kufika katika eneo hilo walibaini kuwa sehemu za siri za mwanamke huyo ziliingiziwa kitu chenye ncha kali.
 
Jeshi la Polisi wilayani Kahama limethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku Mrakibu msaidizi wa Polisi Aziz Mayunga akitoa wito kwa wananchi kufika katika chumba cha kuhifadhia maiti ili kuutambua mwili huo.

Thursday, August 15, 2013

TINDIKALI YAUZWA KWEUPE.....!!!!


LICHA ya serikali kutangaza kudhibiti upatikanaji holela wa tindikali, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa kimiminika hicho bado kinapatikana kirahisi mitaani..........................BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI»
Mwishoni mwa wiki iliyopita, IGP Said Mwema, Mkurugenzi wa Mashitaka Tanzania, Dk. Eliezer Feleshi na Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samweli Manyele walitoa tamko la kudhibiti upatikanaji holela wa tindikali ambao umesababisha kujeruhiwa kwa watu wengi nchini.

Jumatatu iliyopita, mapaparazi wetu walizama mitaani na kuanza kuisaka bidhaa hiyo ili kuona kama upatikanaji wake una ugumu wowote.
 

Katika maabara moja iliyopo Kinondoni, Dar mapaparazi waliambiwa tindikali inapatikana, nusu lita shilingi 45,000. Maabara moja iliyopo Ilala, bidhaa hiyo inapatikana kwa nusu lita shilingi 30,000, lakini bei inaweza kupungua hadi shilingi 25,000.
 

Mapaparazi hawakuishia hapo, walifika hadi Kipawa jijini Dar ambapo walikutana na mwalimu mmoja wa shule ya sekondari ambaye alisema anaiuza bidhaa hiyo kwa shilingi 16,000 tu na hashushi zaidi ya hapo. Tindikali hiyo ni mali ya shule. Zoezi la kuiandaa likaanza ambapo mwalimu huyo alikuwa akichanganyachanganya malighafi na kupata tindikali kamili.

Ili kuithibitisha kuwa ni tindikali kweli, aliwapa mapaparazi makaratasi maalum (litmus paper) ambayo hutumiwa kufanyia ‘test’ kitaalam. Makaratasi hayo hubadilika rangi toka bluu kuwa mekundu kila yanapokutana na tindikali na kuashiria kuwa ni yenyewe. Wakati akiendelea kuchanganya, mara kadhaa wanafunzi waliingia lakini aliwatoa nduki.

Huku akirekodiwa video kwa siri (ipo Global), mwalimu huyo alisema amekuwa akiwauzia watu mbalimbali bidhaa hiyo na alikiri kwamba huwa hawaulizi wanakwenda kufanyia nini kama ambavyo hakuwauliza mapaparazi wetu.
 

Hadi mapaparazi wetu wanaondoka shuleni hapo, mwalimu huyo hakujua kama wanunuzi waliokwenda kununua tindikali hiyo ni ‘wapelelezi’ mahiri kutoka Global Publishers.  Mitaani watu wanasema tindikali ni silaha mpya ya maangamizi kwa kizazi cha sasa ambapo kila kukicha hofu ya watu kujeruhiwa na kimiminika hicho inazidi kupanda.
 

Mpaka sasa, Watanzania wengi wameshamwagiwa tindikali na watu wanaosadikiwa ni wabaya wao. Miongoni mwa watu waliokumbwa na balaa hilo ni mmiliki wa Home Shopping Center, Said Mohamed Saad, Shehe wa Bakwata wilayani Arumeru, Issa Makamba na mtu  aliyedaiwa ni mpiga debe wa CCM, Igunga  Mussa  Tesha.
 

Wengine ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo, Katibu wa Mufti Zanzibar, Shehe Fadhili Soraga na wasichana wawili raia wa Uingereza, Kirstie Trup na Katie Gee.Chanzo;GLOBAL PUBLISHERS BLOG

SOMA NI MUHIMU::::::: Mapenzi kwa njia ya MDOMO Ni chanzo cha SARATANI YA KOO....


Saratani imeendelea kuwa tishio hapa nchini huku hofu ikiendelea kuikumba jamii kutokana na wataalamu wa afya kushindwa kufahamu tiba halisi ya maradhi hayo hatari. Takwimu kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road zinaonyesha ongezeko la saratani ya mdomo na koo kwa kiasi kikubwa kutoka kesi 167 mwaka 2006 hadi 277 mwaka 2012.

Mkurugenzi wa Idara ya Kinga Ocean road, Julius Mwaiselage anaeleza kuwa watanzania wasipende kuiga mambo ambayo si sahihi bila kujua madhara yake kama kufanya mapenzi kwa njia ya mdomo. “Saratani ya mdomo ipo, na nyingine zinasababishwa na zinaa “ anasema Dk Mwaiselage.

Tafiti za saratani

Tafiti mbalimbali zimewahi kufanyika nchini na kubaini kuwepo kwa ongezeko la saratani ya mdomo.Utafiti uliofanywa na Dk Innocent Mosha wa Kitengo cha Patholojia cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), umebaini aina za saratani 1,594, kati ya hizo 509 zikiwa ni za midomo kwa mwaka 2003 pekee.

Matokeo hayo yanaonyesha kuwa kati ya saratani 509 za mdomo, saratani 242 zilisababishwa na Virusi vya Human Papiloma ambavyo hutokana na zinaa. “Ninachojua mimi ni kuwa Virusi vya HPV husababishwa na magonjwa ya zinaa, hivyo mtu anayeugua saratani ya aina hiyo, imetokana na zinaa,” anasema Dk Mosha.

Wanaume waathirika zaidi wa Saratani

Takwimu hizo ni zile zilizopatikana kwa watu waliokwenda kufanyiwa uchunguzi katika Mkoa wa Dar es Salaam pekee. Dk Mosha anasema kuwa wanaume ndiyo huathiriwa zaidi na saratani ya mdomo ambapo kwa hapa nchini, asilimia 53 ya wanaume waliofika MNH kwa ajili ya vipimo, walibainika kuugua saratani hiyo, huku wanawake wakiwa ni asilimia 47. Utafiti kama huo ulifanywa pia na Dk Amos Mwakigonja, mkuu wa Idara ya Patholojia katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Muhimbili (MUHAS).

Dk Mwakigonja alifanya utafiti wa saratani ya mdomo aina ya Kaposi’s Sarcoma ambapo wagonjwa 78 walibainika na saratani hiyo kuanzia mwaka 1990 hadi 2003. “Saratani za mdomo zipo za aina nyingi na zimetofautiana kulingana na visababishi vyake,” anasema Dk Mwakigonja. Katika utafiti wake Dk Mwakigonja alibaini kuwa wanawake wengi walikuwa na saratani ya mdomo aina ya Kaposi’s Sarcoma kuliko wanaume.

Hata hivyo, utafiti huo ulionyesha kuwa asilimia 50 ya wanaume walikuwa na saratani ya mdomo hatari zaidi (systemic) kuliko wanawake ambao ni asilimia 37.

Mapenzi kwa mdomo husababisha maradhi

Dk Mwakigonja anasema kuwa mapenzi yoyote kwa njia ya mdomo lazima yasababishe maradhi ya zinaa iwapo mmoja ameambukizwa. Pia anasema kwamba sampuli nyingi za wanaume wanaojihusisha na mapenzi na wanaume wenzao (mashoga) zilibainika na saratani ya mdomo. Utafiti huo ni sehemu ya utafiti wa Shahada ya Uzamivu ambao ulionyesha kuwa wagonjwa wengi wa saratani ya mdomo walikuwa ni wanaume wenye umri wa miaka kati ya 38 na kuendelea na wanawake ni 31.

Ufatiti wa WHO Tanzania

Shirika la Afya Duniani (WHO) pia lilifanya utafiti mwaka 2010 nchini kwa kushirikiana na Kituo cha Taarifa za HPV, ambapo ilibainika kuwa asilimia 20 ya saratani za koo na mdomo nchini zinasababishwa na ufanyaji wa mapenzi kwa njia ya mdomo.

Taarifa hizo za WHO zinaeleza kuwa wanaume 747 hugundulika na saratani ya mdomo kila mwaka wakati wanawake 472 hubainika na saratani hiyo pia. Wakati huohuo, wanaume wanaopoteza maisha kutokana na saratani hiyo ni 444, kwa mwaka na wanawake ni 270, kwa mwaka. Utafiti wa WHO umebaini kuwa saratani ya mdomo inashika nafasi ya sita katika aina 24 za saratani 24 zinazoisumbua zaidi Tanzania.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa wanaume wanaoathirika zaidi ni wenye umri wa kati ya miaka 15 na 55, ambao tayari wameshaanza kujihusisha na ngono. Kama maradhi mengine ya kuambukiza, Virusi vya HPV huambukizwa kwa urahisi zaidi kutoka kwa wanawake kwenda kwa wanaume kuliko kutoka kwa wanaume kwenda kwa wanawake. Utafiti huo uliodhaminiwa na mfuko wa Bill na Melinda Gates na Kituo cha Saratani na Mpango wa Utafiti wa Taasisi ya ICO unaeleza kuwa mitandao ya kijamii na picha za ngono ndiyo chanzo cha watu wengi kuiga ufanyaji wa mapenzi ya aina hiyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, tafiti zimefanyika na kubaini kuwa asilimia 70 ya wagonjwa wanaobainika na saratani ya koo na mdomo duniani, husababishwa na Virusi vya Human Pappiloma vinavyotokana na magonjwa ya zinaa.Tafiti hizo zinaonyesha kuwa wagonjwa wengi wanaogundulika na saratani hiyo ni wanaume wenye umri wa kati, wenye uwezo wa kifedha, wasiovuta sigara wala siyo walevi waliokubuhu.

Utafiti huo ulibaini kuwa wanaume wapo hatarini zaidi kupata saratani ya koo inayosababishwa na Virusi vya HPV. Miaka ya 80, idadi ndogo ya watu waliougua saratani ya koo walihusishwa na maambukizi ya Virusi vya HPV. Kihistoria, watu waliobainika na ugonjwa huo, ni wenye umri wa miaka 70 kwenda juu ambao walikuwa ni wale walevi waliokubuhu na wavuta sigara.

Ilielezwa kuwa Virusi vya HPV vipo kwa wingi kiasi ambacho watu wazima wanaojihusisha na ngono ya aina yeyote ile, huweza kupata maambukizi ya zinaa hata kama siyo saratani. Hata hivyo ilibainishwa kuwa saratani isababishwayo na virusi vya HPV ni rahisi kuitibu kuliko saratani ya koo isababishwayo na tumbaku au pombe kali.

Virusi vya HPV ni nini?

Kwa jina la jumla, saratani ya koo au mdomo huitwa saratani ya kichwa na shingo. (Neck and Head Cancer) HPV ni miongoni mwa virusi hatari zaidi duniani visababishwavyo na magonjwa ya zinaa na vinaweza kuathiri sehemu mbalimbali za mwili. Zipo aina zaidi ya 120 za HPV, baadhi huweza kuzalisha usugu (warts) ambazo si saratani katika sehemu za siri, mikononi na miguuni. Maambukizi ya HPV hufanyika kwa urahisi, hata kwa kugusana ngozi au majimaji, huku maambukizi mengine yakisababishwa na ngono.

Virusi hatari na vinavyosababisha saratani ni HPV-16, HPV-18, HPV-31 na HPV 45. Aina hii ya Virusi vya HPV husababisha saratani ambapo uvimbe waweza kujitokeza kwa ndani na unaweza usionekane ukilinganisha na vivimbe vingine vya saratani. Wataalamu wanasema HPV-16 na HPV-18 inahusishwa zaidi na saratani ya shingo ya kizazi na endapo mapenzi kwa njia ya mdomo yatafanywa na mtu mwenye uambukizo huu ni rahisi

Muuaji Wa Bilionea Kilimanjaro Anaswa


Polisi wamefanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiashara tajiri wa madini ya Tanzanite huko Mirerani anayetajwa kuwa ndiye aliyepanga na kukodi watu waliomuua bilionea Erasto Msuya. 

Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zimedai kuwa mfanyabiashara huyo alikamatwa mwishoni mwa wiki na jana na juzi alikuwa akihojiwa na makachero.


Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mfanyabiashara huyo ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki mbili zilizotumika katika mpango huo na pia alitoa fedha kwa ajili ya kununua simu mpya na laini mpya.“Tumewakamata watu wametupa mwanga mzuri na huyo mfanyabiashara ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki na siku moja kabla ya tukio zilihifadhiwa nyumbani kwake,” alidokeza polisi mmoja.

Habari hizo zimedai kuwa polisi pia imewahoji mawakala wa kampuni za simu ambao walitumiwa kusajili laini mpya za simu zilizotumika kumpigia marehemu na kutumika kupanga mauaji hayo.

Pikipiki hizo mbili, zilinunuliwa siku moja kabla ya tukio kisha zikahifadhiwa nyumbani kwa mfanyabiashara huyo hadi siku iliyofuata ambapo aliwakabidhi wauaji na zote zimekamatwa.

Mahojiano kati ya mfanyabiashara huyo na Polisi yamekuwa yakifanyika kwa siri na katika kituo cha polisi (jina tunalo) na kwamba mambo ni mazuri ingawa jina lake halijatajwa.

credit  http://networkedblogs.com/O73DM

Tuesday, August 13, 2013

YAMEZIDI SASA:::::: BILIONEA MWINGINE AUAWA KWA KUPIGWA RISASI JIJINI DAR

MAUAJI ya wafanyabiashara wakubwa ‘mabilionea’ yameshika kasi nchini ambapo baada ya tajiri mkubwa Arusha, Erasto Msuya kuuawa kwa risasi hivi karibuni, Agosti 3, 2013 bilionea Elia Daniel Endeni (49) naye aliuawa kwa kupigwa risasi nje kwa mwanamke anayedaiwa kuwa ni mke wake mdogo aitwaye Juliana Labson (28).

Tukio hilo lilijiri siku hiyo saa 2 usiku maeneo ya Temeke Mikoroshini jijini Dar es Salaam ambako ni nyumbani kwa Juliana.
 

Elia alikuwa na kampuni iitwayo Elia Herdons Ltd ya kupakua na kupakia mizigo ya makontena bandarini, maduka na majumba ambapo polisi walikuta shilingi 151,000,000 taslimu ofisini kwake akiwa amezihifadhi.

Ilidaiwa kuwa muda huo, Elia alikuwa amefika nyumbani kwa mwanamke huyo lakini kabla hajashuka katika gari lake, Pick-up lenye namba za usajili T 319 AFJ alichomolewa kwenye gari na kupigwa risasi na watu wawili wasiojulikana.


Taarifa zilieleza kwamba waliotekeleza unyama huo walikuwa wakimfuata marehemu huyo kwa nyuma wakiwa kwenye pikipiki.

Baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili walisema marehemu alikuwa na kawaida ya kufika nyumbani kwa Juliana nyakati za usiku na kabla ya kushuka kwenye  gari, alikuwa akimpigia simu mwanamke huyo ili afungue mlango.

“Ilikuwa wakati anapiga simu ndipo alivamiwa na watu hao ambao walivunja kioo cha gari kwa kutumia kitako cha bastola kisha kutoa ‘loki’ ya mlango na kumchomoa.
 


“Walimdhibiti bila kutoa sauti, wakati huo sisi tulikuwa tumekaa nje tukishuhudia lakini tuliamini kwamba huenda walikuwa wamegongana barabarani kwani hata marehemu hakusikika akiomba msaada,” alisema mwanamke mmoja jirani ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.

Mwanamke huyo aliendelea kusema kwamba hakukusikika mlio wa risasi, bali marehemu alianza kulia ghafla akiomba msaada.

Aliongeza kuwa watu walipokaribia eneo la tukio, wauaji hao walipiga risasi mfululizo hewani, kitendo kilichowafanya watawanyike kuokoa maisha yao na majambazi hayo yakatoweka.

Inadaiwa majirani walipofika, walimkuta tajiri huyo akiwa amelala katika dimbwi la damu huku ameishiwa nguvu kiasi kwamba alishindwa kuongea chochote.

Habari zinasema mke huyo mdogo aliyezaa naye watoto wawili, alipotoka ndani alizimia baada ya kuona Elia akiwa katika dimbwi la damu.

Muda mfupi baadaye, polisi walifika eneo la tukio na kumchukua majeruhi kumpeleka Hospitali ya Temeke ambapo alifariki dunia akiwa njiani.

Taarifa zinadai kwamba Julai 28, mwaka huu marehemu Elia alikoswa na risasi akiwa njiani kwenye gari akitokea msibani Same, Kilimanjaro.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, ACP Engelbert Kiondo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba walifika katika eneo hilo wakiwa na wasiwasi kwamba huenda watu hao walimnyang’anya bastola.


“Ilitubidi twende ofisini kwake Kurasini na kupekua, tukaikuta bastola. Hili suala linaonekana ni kisasi kwa sababu wamemuua bila kuchukua kitu chochote, tunaendelea na upelelezi,” alisema Kamanda Kiondo.

Mazishi ya Elia yalifanyika Jumatano iliyopita, Same ambapo Juliana alikuwa miongoni mwa waombolezaji. Mke mkubwa wa marehemu aishiye Kimara King’ong’o jijini Dar ndiye aliyekuwa ameongoza msiba huo.

Monday, August 12, 2013

CHEKA NA MTANDAO;;;; Atumia Biblia Kumtongoza Msichana na Kumpata!


Jamaa: Hello mrembo, samahani, una mpenzi?
Binti: Hapana. Sina mpenzi.
Jamaa: Kitabu cha Mwanzo 2: 18 “Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”
Binti: Lakini mimi sikupendi jamani.
Jamaa: Waraka wa kwanza wa Yohana 4:8 “Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.”
Binti: Mh! Mi ntajuaje kwamba na wewe unamaanisha hayo maneno?
Jamaa: Injili ya Mathayo 12:34b “Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.”
Binti: Jamani leo kazi. Mi ntajuaje kwamba we ni mkweli na mwaminifu?
Jamaa: Injili ya Marko 13:31 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Binti: Wewe! Na kwanini umekuja kwangu? Wasichana mbona wako wengi tu!
Jamaa: Mithali 31:29 “Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.”
Binti: We una mambo wewe! Sasa mimi kwangu umependa kitu gani?
Jamaa: Wimbo Ulio Bora 4:7 “Mpenzi wangu, u mzuri pia pia, Wala ndani yako hamna ila.”
Binti: Mh! Huo uongo, mbona mimi hata sio mzuri kihivyo. Unaongeza chumvi tu!
Jamaa: Mithali 31:30 “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.”
Binti: Nikisema nimekukubalia itakuaje?
Jamaa: Mwanzo 2:24 ” Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”
Binti: Jamani we mkaka. Inakuaje unajua maandiko kiasi hicho?
Jamaa: Yoshua 1:8 “Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.”
Binti: Wowwww! Naona unampenda sana Mungu.
Jamaa: Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini.”
Binti: Mh! Haya bwana. Basi nipe muda nifikirie ombi lako.
Jamaa: Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.”
Binti: Mh! Jamani wewe, haya, nimekubali. Mpaka hapo nakupenda tayari!!
Jamaa: Ufunuo wa Yohana 22:21b “Amina”

HII KALI::: Bilionea Msuya kuzikwa leo, jeneza lafunguliwa kwa ‘rimoti’


Arusha. Mazishi ya kifahari yanaandaliwa na familia ya marehemu Erasto Msuya, huku ikielezwa kuwa jeneza litakalotumika kubeba mwili wake linafunguka kwa kutumia ‘rimoti’.
Msuya aliyeuawa wiki iliyopita, anazikwa leo huku familia ikitangaza kutokulipiza kisasi kwa waliohusika, badala yake wamemwachia Mungu.
Kinachovutia katika msiba huo ni jeneza lililobeba mwili wa mfanyabiashara huyo lililoagizwa Nairobi, la aina yake huku likifunguliwa kwa kutumia ‘rimoti’.
Jeneza hilo lililoagizwa kutoka Kampuni ya Montezuma & Monalisa Funeral Home, linafunguliwa kwa kubonyeza kifaa maalumu hata mhusika anapokuwa mbali.
Hali hiyo ilionekana kuwaacha na mshangao maelfu ya waombolezaji waliofika kuaga mwili wakati wa ibada iliyofanyika nyumbani kwake, Kwa Iddi, wilayani Arumeru.
Mfanyabiashara huyo aliyeuawa kwa kumiminiwa risasi zaidi ya 20 na watu wasiojulikana, anazikwa leo nyumbani kwao eneo la Kairo Mirerani, Wilaya ya Simanjiro, mkoani Manyara.
Kaka wa marehemu, Israel Msuya, alisema jana kuwa mazishi hayo yatafanyika makaburi ya familia ya mzee Elisaria Msuya ‘Kikaango’, baba wa marehemu Erasto.
Kwa mujibu wa Kamati ya Maandalizi ya mazishi hayo inayoongozwa na kaka mkubwa wa familia ya Msuya, Gady, zaidi ya Sh100 milioni zimepangwa kugharimia shughuli za maombolezo na mazishi.
Jeneza na gari maalumu la kubebea mwili wa marehemu yameagizwa kutoka Kampuni ya Montezuma & Monalisa Funeral Home ya Nairobi, Kenya kwa gharama ya Sh8 milioni.
Chakula, vinywaji, mapambo na magari ya kukodishwa kutoka Arusha kwenda Mirerani na kurudi yanatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh80 milioni.
Katika hatua nyingine, polisi mkoani Arusha imeendelea kuwahoji wafanyabiashara maarufu wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani, wilayani Simanjiro, wakidaiwa kuhusika na kifo hicho.
Habari zilizopatikana jana zinadai mfanyabiashara mmoja kijana ambaye aliibuka ghafla kuwa tajiri mkubwa kutokana na biashara ya madini ya Tanzanite, anashikiliwa Arusha kwa mahojiano.
Jana, kwenye viunga vya Mji wa Mirerani watu walitangaziwa kuwa mfanyabiashara huyo, alikuwa anashikiliwa kwa mahojiano kuhusiana na kifo hicho.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, hakupatikana mara moja kuelezea suala hilo kwani simu yake ilipopigwa ilikuwa haipatikani.
Marehemu ameacha mke na watoto wanne, huku akiacha rasilimali nyingi ikiwamo jumba la kifahari lililopo Sakina kwa Idd, hoteli maarufu za SG Resort na Mezza Luna zilizopo Arusha.

AJALI AJALI AJALI AJALI........... MPAKA LINI?



Lilikuwa likisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda mkoani Arusha, lilipata ajali maeneo ya barabara ya Chalinze- Segera Bagamoyo. Abiria wawili wamefariki dunia na wengine 63 wamejeruhiwa na kulazwa katika vituo vya afya kadhaa, zahanati pamoja na Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani baada ya basi mali ya Kampuni ya Meridian kuacha njia na kupinduka jana katika Barabara Kuu ya Chalinze- Segera wilayani Bagamoyo mkoani Pwani

Abiria waliofariki ni miongoni mwa majeruhi 24 wa ajali hiyo ambao walipelekwa moja kwa moja kupata matibabu katika Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani, Tumbi baada ya hali zao kuonekana ni mbaya zaidi ya wengine katika eneo la tukio. Wengi walikuwa wamevunjika sehemu mbalimbali za miili yao.
Kamanda wa Polisi Pwani Ulrich Matei alithibitisha kutokea ajali hiyo.

Akizungumza hospitali hapo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya hiyo, Dk Peter Dattan alithibitisha kupokea baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo na kusema kuwa kati ya 24 waliofikishwa hapo wawili walifariki na wote ni wanaume majina yao bado hayajajulikana.
Dk Dattan alisema majeruhi 22 wanaendelea kupatiwa matibabu na kati yao wanawake ni 12 na kwamba kwa jumla hali zao wote ni mbaya kutokana na majeraha makubwa waliyoyapata.
Naye Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya Chalinze walikolazwa majeruhi wengine Dk ,Victor Bamba akizungumza kituoni hapo alisema majeruhi waliofikishwa hapo ni 12.

Alisema majeruhi watatu kati ya hao walikuwa wakifanyiwa mpango wa kupelekwa Tumbi baada ya hali zao kubadilika na kwamba wengi wao wameumia zaidi sehemu za kichwani, kuvunjika miguu, mikono na mbavu
Dk Bamba aliiomba Serikali na wadau wa afya kuhakikisha kuwa utoaji na usambazaji dawa na vifaa tiba unalenga kwenye maeneo yenye ajali nyingi za barabarani ili kuweza kupatikana dawa na vifaa tiba kwa wakati pindi inapotokea matukio ya ajali.
Kwa mujibu wa mashuhuda na wakazi wa Kijiji cha Kimange, Hamis Shaaban na Yusufu Mzee walisema ajali hiyo ilitokea saa 5.40 asubuhi jana
mwananchi.

UTAMJUAJE MWENYE MAPENZI YA KWELI?????



Nimeandika mada hii kutokana na watu wengi kushindwa kutofautisha kupendwa kweli na kutamaniwa. Wapo walioingia mkenge kwa neno hilo hasa walio wageni katika uwanja huu wa mahaba. Ukiambiwa unapendwa basi unachanganyikiwa na kusahau maneno matupu hayajengi nyumba.

Nina maana gani?

Watu wengi wamekuwa wakitumia neno hili kama mtego wa kumpata mtu, kwa kujifanya anakupenda sana na nahau nyingi za mapenzi ambazo zinaweza kukufanya masikio yako yazibe na kuona nani kama wewe.

Siku zote mtafutaji ana lugha tamu ya mapenzi na kabla ya kutamka lolote lazima atangulize nakupenda sana na kuongezea ajuavyo. Hii si mara moja watu kuingia mkenge inapotokea wanakutana na hali hiyo.

Lazima uelewe serikali ya mwili wako inakutegemea wewe, ukiipeleka vibaya lawama zitakuwa juu yako. Usiwe na papara ya kutoa uamuzi wa kukubali uambiwavyo unapendwa bila kufikiria kwa kina. Hakuna hata siku moja mtu anayekutaka kimapenzi akuambie anakuchukia.

Fikiri kabla ya kutenda na kuona kauli uliyopewa ina nia gani na wewe, kweli anakupenda au anataka kukuchezea na kukuacha.

Katika uchunguzi wangu nimegundua wengi hupima kwa masikio juu ya kile aambiwacho na si kufikiria nini hasa kilichomvutia aliyekutamkia maneno hayo. Japo kakutamkia anakupenda, ni vema ukafanya kadiri uwezavyo kupata muda kufikiria kwa kina kabla ya kutoa uamuzi wowote ambao unaweza kukufanya uwe na faida au hasara.

Neno nakupenda siyo mapenzi kamili, bali tabia ya mtu na kuonyesha kweli anakupenda kwa dhati. Akupendaye huwa hana haraka ya kufanya ngono, hufuata taratibu zote ili mradi kujenga uaminifu moyoni mwako.

Hii hutokana na kuwa na uhakika wewe ni wake, hana hofu ya kutanguliza ngono mbele katika uhusiano wenu wa kimapenzi. Ukiona umekutana na mtu anayetanguliza ngono baada ya neno nakupenda huyo hakupendi bali anakutamani.

Tumekuwa tunatumia neno nakupenda kama kiwakilishi cha ujumbe wa mapenzi na si penzi kamili.
Mapenzi ya kweli ni ya vitendo na si maneno, anayekupenda utamjua tu wala hajifichi. Atakuwa mpole, mwenye huruma, anayekujali, muaminifu na mtu aliye muwazi mwenye kukupa uhuru wa kumjua kwa undani ili kukuondoa wasiwasi.

Mapenzi mengi ya siku hizi yamekuwa ya usiri mkubwa yenye mipaka. Kama kweli anakupenda kwa nini akudanganye na akuwekee mipaka ya kumjua? Wakati huo mdomoni kwake ana kila nahau tamu za kimapenzi na kulitamka neno nakupenda kama kiwakilishi.

Huyo si mkweli wala hana mapenzi bali ni muongo aliyejificha nyuma ya neno nakupenda. Kuwa macho na watu hawa sipendi kesho uniulize swali hili.source ya mada hii,Muandishi Joseph shaluwa

HOTUBA YA MUGABE BAADA YA UCHAGUZI


Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anatarajiwa kutoa hotuba yake ya kwanza tangu kushinda uchaguzi mkuu wa Zimbabwe zaidi ya wiki moja iliyopita. Mugabe atahutubia umma wakati wa sherehe za kuadhimisha siku ya mashujaa mjini Harare kuwakumbuka wale waliofariki wakipigania uhuru wa taifa hilo.
Chama pinzani cha MDC, chake waziri mkuu Morgan Tsvangirai, kitasusia sherehe hizo.

Chama hicho kimewasilisha malalamiko yake kuhusu uchaguzi mkuu ambao kinasema ulikumbwa na wizi wa kura kikitaka uchaguzi huo kurejelewa.Bwana Mugabe alishinda 61% ya kura kwenye uchaguzi huo uliokamilika tarehe 31 mwezi Julai, huku mpinzani wake Morgan Tsvangirai akichukua nafasi ya pili kwa 35% ya kura zilizopigwa.

Chama cha Mugabe Zanu-PF kilishinda wingi wa viti vya bunge kikipata zaidi ya thuluthi mbili ikiwa ni viti 160 ya viti kati ya 210 vya bunge zima.Sherehe za kuadhimisha siku ya mashujaa Zimbabwe, ni sherehe za kujivunia kwa wazimbabwe wakati ambapo nchi hiyo ilijipatia uhuru wake miaka ya sabini.
Hii leo Mugabe atatoa hotuba yake ya kwanza katika eneo la kumbukumbu la vita hivyo na ambako baadhi ya wapigania uhuru wamezikwa.
Hotuba za Mugabe zinasifika zaidi kwa siasa zake kali za kizalendo, na ambazo zaidi hulenga mkoloni wake wa zamani Uingereza na pia anatarajiwa kujipiga kifua kufuatia ushindi wake mkubwa katika uchaguzi mkuu uliopita mwezi jana.

Chama cha MDC kinasusia sherehe hizo katika kile kinachosema ilikuwa wizi mkubwa wa kura uliofanywa na chama cha Zanu-PF, kwa hivyo sherehe hii bila shaka itazongwa na siasa.
Mugabe bado hajaapishwa kwa muhula wake wa saba akitawala Zimbabwe, kwa sababu ya kesi ya MDC mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi huo.
MDC kilisema kina ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa wizi wa kura ulitokea na kwamba kulikuwa na visa vingine vilivyohujumu matokeo ya uchaguzi huo ikiwemo, rushwa , dhuluma na kuvurugwa kwa daftari la wapiga kura.

NIMEIPENDA:::: KUTOMFIKISHA KILELENI MPENZI WAKO NI SAWA NA KOSA LA JINAI AMBALO HUKUMU YAKE NI "KUMWAGANA"












Ndoa yoyote ambayo mke au mume hafiki kilele hiki cha Mlima Kilimanjaro…,hiyo siyo ndoa inayokwenda sawa na kuna madhara makubwa kwa pande zote, kwa maana ya mwingine kuweza kuamua kutoka.
 

Ni vizuri walio kwenye ndoa kujifunza namna ya kupeana raha iwapasayo wanandoa kuipata. Kama unafikiri mkeo unaye kwa sababu amekuja kutafuta kula au kununuliwa magari na nguo, hilo ni kosa. Tafakari namna ya kupeana raha kwa kila kona.

 

Kama ni kula, kila mtu anaweza kujitafutia kwa njia mbalimbali kama ni kuuza mama ntilie na kadhalika.
 

Mwanamke yuko kwa mume kwa sababu anahitaji kupata vitu ambavyo wanawake huvipata kutoka kwa wanaume; …Mume ndiyo kichwa, iongoze ndoa yako vizuri kwa hekima; …Kichwa kikiwa ‘bangi’, ubavu (mke) atafanya nini?



Ni suala la lazima

Kwa asili, inatakiwa mke na mume kufanikisha zoezi hilo la kuwezeshana kufika kileleni  na  ni jambo muhimu kama ilivyo kutoka jasho mwilini, maana siyo tu mwili unaondoa uchafu ndani ya mwili, pia inasaidia kuupoza mwili kuwa sawasawa.


Najua wapo wanaoweza kusema aaah mbona mimi nimekaa mwaka sitaki tena mwanaume au mwanamke na sijapata madhara… Inawezekana ni kweli, lakini wengi hupata madhara.
 

Kadhalika kuna wengine wanafanya vitu vya hatari kama kutumia vitu mbalimbali kama mwanasesele (sex toys) au mashine maalumu zenye umbo kama la mwanaume au wengine kujichua au kusagana.

 

Ukidumu bila tendo la ndoa muda mrefu, baadhi ya madhara madogomadogo ni kama kuwa na hasira za mara kwa mara katika mambo madogo, hii hasa kwa wanawake ambao walishawahi kuwa na uhusiano unaokaribiana kuoana au waliwahi kuwa kwenye ndoa kisha wakatoka.

 

Kwa wanaume madhara yake ni kupendelea zaidi kuangalia picha za ngono. Kwa wote kwa maana ya wanaume na wanawake huwa na hali ya kusahausahau.


Kwa wanawake, wapo ambao hutokwa damu nyingi wakati wa hedhi. Kwa watu wote yaani wanawake na wanaume hupenda kurukia mambo ya watu wengine (tabia ya kufuatilia mambo yasiyokuhusu) na wakati mwingine huongea kwa sauti ya juu hasa kunapotokea migogoro. 



 Wengine wana uwezo mkubwa wa kutukana au kutoa kauli yoyote unapomuuzi, anasema Leonard Trelawny katika jarida lake la mageuzi alilochapisha, New York Marekani.



Athari nyingine ni kuumwa na kichwa kwa wanaume na wanawake, kupoteza umakini katika kazi na kwa jumla sehemu za kazi wengi wa watu ambao wamesema hawataki tena kusikia mapenzi, siyo viongozi wazuri, wana kauli chafu, hata uamuzi wao mara nyingi siyo mzuri, ingawa siyo wote.



Hali kadhalika siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno. Aidha, unawaweza kuanzisha tabia nyingine mbaya kama ulevi, kukaa ofisini tu bila sababu.
Dismas Lyassa ni mtaalamu wa uhusiano aliyesajiliwa na Serikali kupitia taasisi ya Global Source Watch

-Mwananchi
 
 

KARIBU NYUMBANI FEZA KESSY,........ TULIKUMIS SANA


Hatimaye safari ya Tanzania katika Big Brother ‘The Chase’ imefikia tamati jana (August 11) baada ya mshiriki pekee aliyekuwa amesalia Feza Kessy kutolewa.


Feza ambaye amefanikiwa kudumu kwenye mchezo kwa siku 77 amekuwa mshiriki wa 20 kuliaga shindano hilo huku Cleo na Dillish waliokuwa dangerzone wakibaki salama.

 
Feza aliyekuwa ameshikilia bendera ya Tanzania wakati wa eviction hakuonekana kushtuka sana baada ya mtangazaji wa eviction show IK kumtaja kuwa ndiye anayefungasha mizigo, huenda kwasababu tayari alikuwa ameshakata tamaa ya kubaki toka wiki iliyopita.

 
Matumaini ya Feza yalionekana kufifia kuanzia eviction ya wiki iliyopita ambayo hakuamini kuona amebaki huku kipenzi chake Oneal akitolewa, lakini katika dairy session ya jana jioni masaa machache kabla ya eviction pia alisikika akimwambia biggie “I feel like it is over for me,” baada ya Biggie kumuuliza alimaanisha nini aliposema “I have lost hope but not in a bad way I think it is a defence mechanism”.
 
Nguvu ya ushindi kwa Feza ilianza kupungua siku kadhaa baada ya kuzama kwenye mapenzi na Oneal kiasi cha kuwafanya washiriki wenzao kuwaona wanajitenga muda mwingi na kujisahahu kuwa wapo mchezoni.

 
Moja ya maswali ambayo IK alimuuliza Feza baada ya kutoka ni kama bado anampenda Oneal, na jibu lilikuwa “Yes I do”, je unadhani hii inamaanisha kuna kitakachoendelea sasa baada ya ONEZA wote wawili kurudi katika maisha yao ya kawaida?


Baada ya Feza kuondolewa katika The Chase sasa Tanzania inaungana na Kenya na Uganda kubaki kuwa watazamaji baada ya washiriki wote wa Afrika mashariki kutolewa.


Nigeria ndio nchi pekee ambayo mpaka sasa washiriki wake wote wawli Melvin na Beverly bado wako mchezoni wakiwa ni miongoni mwa washiriki 7 waliosalia huku zikiwa zimesalia siku 13 kufika fainali. Unahisi nani ataondoka na $300,000 za Big Brother mwaka huu?