Friday, August 23, 2013

KILA MTU ATAKUA NA MAONI YAKE KWA HII PICHA ::::::::pic of the day::::::::::::

CREDIT: mwananchi.

TUNDAMAN AFANIKIWA KUWATOROKA POLISI AKIWA NUSU UCHI....KISA NI DENI LA LAKI NANE


Msanii Tundaman amejikuta akiambulia aibu ya mwaka baada ya kujitosa nusu uchi mtaani akiwakwepa askari polisi ambao walivamia kwake leo asubuhi kwa lengo la kumkamata....

Chanzo cha Tunda man kusakwa na polisi ni deni la sh. laki nane ambazo alikopa mwanzoni mwa mwaka huu kwa mwanadada mmoja ( jina kapuni).... 

Taarifa zinadai kwamba, baada ya kupewa hela hiyo, Tunda man aligeuka kisima cha matusi ya nguoni kwa mrembo huyo. Kila akipigiwa simu alikuwa hapokei, na akipokea ni matusi ya nguoni..... 

Baada ya hali hiyo, mwana dada huyo aliamua kulifikisha swala lake polisi ambapo Tundaman alikamatwa. Akiwa mikononi mwa polisi, msanii huyo aliomba apewe nafasi ya kulilipa deni lake kwa awamu tatu kuanzia tarehe 12/8/2013 

Baada tarehe hiyo, Tundaman hakuweza kulipa kiasi chochote na wala hakutoa ushirikiano wowote, hali iliyomfanya mwanadada huyo arudi kuripoti polisi.... 

Polisi walianza jitihada za kumsaka ambapo leo majira ya saa nne asubuhi walivamia kwake ( Tabata Savana ) kwa lengo la kumkamata..... 

Bahati nzuri au mbaya, Tundaman alifanikiwa kuwatoroka polisi akiwa na bukta tu ( kwa mujibu wa mashuhuda) na kutokomea kusikojulikana...

Ifuatayo  ni  HATI  YA  MAKUBALIANO  yao  ambayo  mpekuzi  wetu  amefanikiwa  kuipata....

Kama kuna jambo ambalo linaichafua Tanzania katika jukwaa la kimataifa kwa siku hizi, basi ni tatizo la usafirishaji wa dawa za kulevya.
Zamani tatizo hili halikuwa kubwa sana, ni mtanzania mmoja mmoja sana alikuwa akikamatwa nje kwa kusafirisha dawa za kulevya. Kwa hiyo jina la nchi yetu lilikuwa linasikika mara moja moja sana au kwa bahati mbaya kuhusiana na tatizo la dawa za kulevya. Lakini katika siku za hivi karibuni tumesikia kuwa kuna watanzania wanakamatwa Ulaya, Amerika Kaskazini, Amerika Kusini, Asia na hata katika nchi za Afrika, kama ilivyotokea majuzi huko Afrika Kusini. Kwa sasa ukisikia jina la Tanzania linatajwa kuhusiana na tatizo la dawa za kulevya, si bahati mbaya tena na si mara moja moja kama zamani.
Serikali yetu imekuwa ikijitahidi sana kujenga jina zuri la Tanzania na kuitanganza Tanzania kuwa ni kisiwa cha amani, nchi yenye vivutio vingi vya utalii na yenye ukarimu kwa wageni. Na kweli kama ukitembelea nchi yoyote yenye watu wanaoifahamu Tanzania, si vigumu kusikia Tanzania ikisifiwa, lakini kama ukiona mtu amekaa kimya, basi ujue kuna uwezekano kuwa hataki kutaja suala la dawa za kulevya.
Mwanzoni nilikuwa naamini kuwa watanzania ni watu wenye maadili ambao wanapokwenda nje ya nchi wanakumbuka kuwa “mabalozi wazuri” wa nchi. Lakini baada ya kutembelea sehemu mbalimbali duniani, hasa nchi za Asia na Asia Kusini Mashariki, na kukutana na wenyeji na kuwauliuza mtazamo wao kuhusu Tanzania na watanzania, nikagundua kuwa sifa zote nzuri za Tanzania zinafunikwa na sifa mbaya moja au mbili. Kubwa ni tatizo la dawa za kulevya, na nyingine ni ukahaba (Hong Kong).
Pamoja na kuwa ni watanzania wachache sana wanaosafirisha dawa za kulevya, ni hao wachache ndio wanaofanya jina la watanzania wengine walio wengi lichafuke, na kuwafanya watanzania wanaokwenda nje ya Tanzania kwa malengo halali, kama vile biashara, michezo na hata utalii, wakumbwe na matatizo wasiyostahili.
Zamani nilikuwa ninakasirika sana ninapotolewa kwenye mstari wa uwanja wa ndege na kuanza kupekuliwa na kuulizwa maswali ‘ya kipuuzi’, kana kwamba mimi ni mhalifu au mtuhumiwa wa uhalifu. Nilikuwa najihisi kuwa mimi ni mhanga wa ubaguzi wa rangi, kitu ambacho sikutegemea kutoka kwa nchi marafiki zetu. Kuna wakati hata nilifikia hatua ya kukwaruzana na maofisa wa uwanja wa ndege, kwa kuona wananitendea isivyostahili. Lakini baadaye baada ya kuangalia hali halisi na kuona matendo yanayofanywa na baadhi ya watanzania wanaokuwa nje ya Tanzania, nikagundua kuwa wasiwasi walionao maofisa wa viwanja vya ndege vya nchi za Asia kuhusu watu wenye pasi za kusafiria za Tanzania, ni wa haki na unaeleweka, si ubaguzi wa rangi na si ubaguzi dhidi ya watanzania. Kama ni ubaguzi wa rangi, basi matendo ya baadhi yetu ndio yanawapa kisingizio cha kufanya hivyo.
Kinachonifanya nisione kuwa ni ubaguzi wa rangi ni kuwa, nchini China kwa mfano kuna adhabu kali sana kwa watu wanaokamatwa kwa makosa ya dawa za kulevya, wachina wengi wamehukumiwa adhabu ya kifo. Lakini cha ajabu ni kuwa watanzania wanaokamatwa kwa makosa sawasawa na wanayofanya wachina, wanapewa vifungo virefu na adhabu ya kifo, lakini hadi sasa hakuna mtanzania aliyenyongwa ikilinganishwa na wachina na wafungwa wa mataifa mengine.
Kumekuwa na habari za kupotosha kwenye baadhi ya vyombo vya habari vya Tanzania kuhusu jambo hili, lakini ukweli ni kuwa Mpaka sasa hakuna mtanzania aliyehukumiwa adhabu ya kifo kwa makosa ya dawa za kulevya na adhabu yake kutekelezwa. Ni vigumu kujua ni kwanini China haijawanyonga watanzania, lakini ukiangalia sababu ya wachina kutowachukulia hatua kali watanzania, utaona kuwa wanathamini sana urafiki uliojengwa na viongozi wetu, hasa mwalimu Nyerere na mzee Salim Ahmed Salim. Kwa hiyo ukiona jinsi wenyeji wanavyochukuliwa hatua kali, na sisi watanzania “kudekezwa”, hata ukikutana na vitendo vinavyokukosesha raha unapopita uwanja wa ndege, basi inabidi uwe mpole mara moja.
Pamoja na kuwa kila suala la dawa za kulevya linapotajwa, utakachoona kwenye vyombo vya habari ni kuwa kuna mtandao mkubwa wa siri, lakini ni kama tunapuuza madhara yanayoletwa na jambo hili kwa uhusiano kati ya nchi yetu na nchi nyingine, na usumbufu linaoleta kwa watanzania wengine wasio wasafirishaji wa dawa za kulevya.
Inasikitisha kuona kuwa kati ya watu kutoka nchi za Afrika Mashariki, ni watanzania ndio wanaokamatwa zaidi na dawa za kulevya kuliko wale wakenya na waganda. Na hata watanzania wanaokamatwa, wengi wanatoka katika Mikoa miwili ya pwani, ambako baadhi ya vijana wanaona ni “ujiko” kusafirisha dawa za kulevya. Ukiongea na vijana hao, unaweza kuona kuwa hawana elimu hata kidogo, kwani hata uwezo wao wa kuandika kwa Kiswahili na uwezo wa kuongea Kiswahili na kujenga hoja ni mdogo sana, ndio maana inaonekana ni rahisi kwao kurubuniwa kuliko vijana wa Kenya, Uganda na wa nchi nyingine za Afrika Mashariki. Wengi wao wanasema wanaahidiwa kati ya dola elfu mbili na elfu nne wakifikisha “mzigo” salama. Kwa kweli hizo si pesa nyingi ikilinganishwa na hatari ya kazi yenyewe, na hasa ukizingatia kuwa kwa mtanzania anayejituma kufanya kazi nyumbani, anaweza kupata pesa hizo.
Kwa hapa China, mpaka sasa naweza kusema kwa sasa tatizo limefikia kiwango cha kutia hofu, na hasa kwa Hong Kong na Makau ambako kuna wafungwa zaidi ya 100 wa kitanzania. Tofauti na siku za nyuma, idadi ya wafungwa wa kike inazidi kuongezeka siku hadi siku ambapo kwa sasa kuna wafungwa wa kike zaidi ya 20 katika magereza ya China bara na Hong Kong. Kutokana na hali hiyo nina wasiwasi kuwa huenda ile hadhi ya watanzania kuingia katika miji hiyo bila Visa huenda iko mashakani. Lakini vigumu kwangu kama mwandishi wa habari kujua undani wa tatizo hili. Ninachojua ni kuwa kuna watanzania wengi wako gerezani, kutokana na kukamatwa kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya.
Niliwahi kumuuliza aliyekuwa balozi wa Tanzania hapa China na balozi wa sasa kuhusu athari ya tatizo hili kwenye uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania, wote walioonesha kukasirishwa na kusikitishwa na jambo hilo, na kusema linatia aibu. Lakini mabalozi hao hawajui ni nani anayewatuma watanzania wanaokamatwa na dawa za kulevya. Waliokamatwa nao hata siku moja hawataji ni nani aliyewatuma, wao ni kama watu waliokula yamini ya kutosema lolote, hata kama wanapewa adhabu ya kifo. Hata hivyo, wafungwa wanaeleza tu kwamba “Kuna mtandao mkubwa ambao unahitaji ushirikiano mkubwa kupambana nao, zinakopelekwa na zinakotoka dawa hizo”.
Hivi karibuni tumesikia alichokifanya Dk Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, yeye anaona kuwa uwanja unaobeba jina la Mwalimu Nyerere haupaswi kuhusishwa na dawa za kulevya. Alichofanya Dk Mwakyembe pale uwanja wa ndege kwa kweli ni jambo zuri, na kama asingefanya hivyo huenda watanzania tungeendelea kuwa kizani kuhusiana na mambo yanayoweza kuwa yanaendelea katika forodha zetu. Lakini tukiangalia kwa undani tunaweza kuona kuwa, kama uhalifu huo unatokea kwenye uwanja wa ndege unaotakiwa kuwa na usalama mkali, hali ikoje kwenye forodha nyingine mbali na ile ya uwanja wa ndege wa mwalimu Nyerere ambako hakuna kamera za video, ambako Dk Mwakyembe hawezi kwenda kwa ghafla? Kuna Namanga, Holili, Horohoro, Silari, Tunduma nk, hali ya huko ikoje? Dk Mwakyembe anatakiwa kuhakikisha kuwa kilichofanyika katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere kifanyike katika forodha zote. Dk Mwakyembe analia na jina la Mwalimu Nyerere, lakini ni vizuri watanzania wote tukikumbuka kuwa tunatakiwa kulia na jina la nchi yetu, Tanzania.
Kama hali hii ikiendelea inaweza kufika hatua kuwa wanafunzi, wafanyabiashara, wanamichezo, wagonjwa na hata watalii kutoka Tanzania wanaokwenda nje ya nchi, wote watawekwa kwenye kundi la washukiwa wa biashara ya dawa za kulevya.
- See more at: http://www.fikrapevu.com/watanzania-zaidi-ya-100-wako-gerezani-nchini-china-kuhusiana-na-dawa-za-kulevya-20-ni-wanawake/#sthash.WFUZxGSe.dpuf

Thursday, August 22, 2013

MAAJABU YA DUNIA::::::::::::ANGALIA REKODI ZA DUNIA KWA NJIA YA PICHA











Star wa "Prison Break" Wentworth Miller a.k.a Michael Scofield amejiweka wazi kuwa yeye ni Shoga


Star wa "Prison Break",  Wentworth Miller  a.k.a Michael Scofield, amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga), katika barua ya wazi aliyoiandika kwenda kwa Directoe wa St. Petersburg International Film Festival (tamasha la filamu la kimataifa la St. Petersburg).


Muigizaji huyo (41) ameandika barua hiyo kukataa mualiko uliokuwa ukimtaka kuhudhuria tamasha hilo linalofanyika nchini kwao Russia na kwa mara ya kwanza kupitia barua hiyo amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga).
"Asante kwa ukarimu wa mualiko wako, nikiwa kama mtu ambaye amefurahia kutembelea Russia kwa miaka ya nyuma na naweza pia kudai shahada ya asili ya kirusi, ningefurahi kusema ndio, hata hivyo nikiwa kama shoga (gay) lazima nikatae". amesema Miller

Miller akaendelea kusema ... nasumbuliwa sana na tabia ya sasa dhidi ya na jinsi wanavyochukuliwa mashoga na wanawake  na serikali ya Urusi.

"hali hii haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile , na mimi siwezi kwa dhamira nzuri kushiriki katika tukio la kusherehekea linaloandaliwa (wenyeji) na nchi ambayo watu kama mimi kwa mfumo uliopo wananyimwa haki zao za msingi za kuishi na kupenda kwa uwazi"

akamalizia kwa kusema.. kama hali hii itarekebishwa, nitakuwa huru kufanya uchaguzi tofauti.


Miller ameandika barua hiyo baada ya raisi wa Russia, Vladimir Putin kusaini sheria dhidi ya ushoga ambayo mwezi uliopita ilipitishwa sheria hiyo inayozuia mijadala aya wazi dhidi ya mahusiano ya jinsia moja popote ambapo watoto wanaweza kusikia.

Wentworth alipata umaarufu sana pale alipoigiza katika tamthilia ya "Prison Break"  2005-2009, licha ya tetesi za yeye kuwa shoga lakini alikuwa hajawahi kuthibitisha mpaka leo hii.

Wednesday, August 21, 2013

DIAMOND PLATNUMS NDANI SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA.

KWA mara ya kwanza tangu lilipoibuka sakata la watu maarufu kujihusisha ama na utumiaji au usafirishaji wa dawa za kulevya, jina la mwanamuziki anayeaminika kuwa na ukwasi mkubwa kwa sasa hapa nchini, Nasseeb Abdulmaliki, maarufu zaidi kwa jina la Diamond, limeanza kutajwa kuwa ni miongoni mwa vigogo wa ‘unga.’

Tayari mjadala mkubwa wa chini chini umeibuka kwa watu mbalimbali wakiwemo mashabiki wake, na taarifa ambazo zimelifikia MTANZANIA Jumatano kutoka vyanzo mbalimbali zimedai kuwa, mwenendo wa maisha ya Diamond sasa unachunguzwa na baadhi ya maofisa wa vyombo vya dola vya ulinzi na usalama.

Kutajwa kwa jina la Diamond katika sakata hili, kunatiwa nguvu zaidi na mwenendo binafsi wa maisha wa msanii huyo maarufu wa muziki wa kizazi kipya, unaokwenda sambamba na ukwasi mkubwa alioupata katika kipindi kifupi.

Kama hiyo haitoshi, safari za nje ya nchi za mwanamuziki huyo unaohusisha ziara zake nchini Afrika Kusini na Uingereza, pia ni mambo ambayo yamechochea wingu la mashaka lililofikia hatua ya jina lake kuingizwa katika mtandao huo ambao katika siku za karibuni, umewagusa pia baadhi ya watu wenye majina makubwa katika jamii.

Kuhusu ziara hizo, kilicholeta mshtuko na dukuduku dhidi yake ni kuwapo kwa taarifa kwamba, katika moja ya ziara hizo za nje ya nchi, Diamond alifikia hatua ya kusafiri akitumia chumba kinachotumiwa na wageni mashuhuri (VIP), badala ya njia ya wasafiri wa kawaida.

Mbali na hilo, taarifa nyingine zinaeleza kwamba, mizigo ya msanii huyo ambaye mara kadhaa amekuwa akisafiri na kundi la wacheza shoo wake, imekuwa ikipita pasipo kupitishwa katika hatua za ukaguzi kwa namna ile ile ilivyokuwa kwa mabinti wawili wa Kitanzania walionaswa nchini Afrika Kusini baada ya kuruka mfumo wa ukaguzi wa JNIA.

Aidha, ukaribu wa kimahusiano kati ya Diamond na baadhi ya Watanzania wanaoishi nchini Afrika Kusini na ambao majina yao pia yameanza kuhusishwa na biashara hiyo ya mihadarati, ni jambo jingine ambalo limechochea harakati za kufuatiliwa kwa karibu kwa nyendo za Diamond.

Taarifa zaidi kutoka JNIA zinaeleza kwamba, miongoni mwa watu wanaoweza wakawa wamemponza Diamond ni wale ambao walionekana kuwa karibu na Agness Gerald ‘Masogange’ (25) na Melisa Edward (24), siku walipokuwa wakisafiri kwenda Afrika Kusini kabla hawajanaswa katika uwanja wa Ndege wa Oliver Thambo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, wakiwa na shehena ya dawa za kulevya.

Mwenendo wa watu hao unatiliwa shaka kuwa huenda ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya wenye maskani yao nchini Afrika Kusini, kwa sababu mbali na ukaribu na wasichana hao, pia walihusika kwa karibu kuusafirisha mwili wa mwanamuziki Albert Mangwair, aliyefia huko huko Afrika Kusini ambaye taarifa za kufa kwake ziligumbikwa na matumizi ya dawa za kulevya.

Alipoulizwa jana na MTANZANIA Jumatano kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu taarifa hizo na iwapo amekwishahojiwa na vyombo vya dola baada ya jina lake kuanza kutajwa kuwa miongoni mwa orodha ya wasanii wa muziki wanaosafirisha dawa za kulevya, Diamond alikiri kuwa na pesa za kutosha kuishi maisha anayoyataka, lakini akakana kujihusisha na biashara hiyo.

Akifafanua tuhuma moja baada ya nyingine kwa mpangilio aliokuwa akiulizwa na gazeti hili, Diamond alisema katika maisha yake, hajawahi kujihusisha na utumiaji au usafirishaji dawa za kulevya, lakini madai hayo yamekuwa yakitolewa dhidi yake na watu ambao hawajui siri ya mafanikio yake.

“Kazi ngumu siku zote inalipa, sasa napata matunda ambayo yanatokana na kile nilichokifanya, iweje watu wanitilie mashaka, Watanzania ni mashahidi wangu wananiona navyochumia juani, nitaendelea kulia kivulini tu kwani nakula kwa jasho langu.

“Siyo kweli kwamba mizigo yangu haikukaguliwa na kama haikukaguliwa na ingekuwa na kasoro, basi Uingereza wangenitia hatiani, nilipita na nilikaguliwa.” Alisema Diamond.

Alipoulizwa kuhusu taarifa za kuwa mwanamtandao wa kundi la Masogange, pia alikanusha kwa kueleza kuwa hata siku aliyosafiri kwenda Afrika Kusini alikwenda peke yake uwanja wa ndege na kuongeza kuwa alikwenda huko kwa shughuli za kimuziki, ambapo safari nzima iligharimu zaidi ya Dola 30,000 za Kimarekani.

“Afrika Kusini nimekwenda kufanya kazi zangu na safari hiyo imenigharimu zaidi ya Dola 30,000, nilikwenda kurekodi nyimbo yangu mpya inayoitwa namba moja ambayo itaanza kusikika hivi karibuni.

“Unajua Watanzania sasa hivi wanajua mtu hawezi kufanikiwa au kupata maendeleo bila kuuza ‘unga’, hili si sawa juhudi za mtu ndizo zinamfikisha alipo, na mimi juhudi zangu ndio zinanifikisha hapa, watu waache kunijadili vibaya.” Alisema Diamond.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja ikiwa ni takribani miezi miwili sasa tangu Watanzania wawili, Agness Gerald ‘Masogange’ (25) na Melisa Edward (24), waliokuwa na uhusiano wa karibu na baadhi ya wanamuziki maarufu hapa nchini, kukamatwa nchini Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya Sh bilioni 6.8.

Mbali na kuwa na uhusiano wa karibu na wanamuziki, Edward anadaiwa kuwa alikuwa mfanyakazi katika mgahawa mmoja maarufu jijini Dar es Salaam, unaomilikiwa na mmoja wa vijana matajiri hapa nchini ambaye hata hivyo gazeti hili halijafanikiwa kumpata ili kufanya naye mahojiano.

Wakati huo huo, tayari hatua za kinidhamu zimekwishaanza kuchukuliwa dhidi ya wafanyakazi wa JNIA waliohusika kupitisha kilo 150 za dawa za kulevya, ambao Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ametaja majina yao hivi karibuni na kuonyesha kwa waandishi wa habari ushahidi wa kuhusika kwao.


-Mtanzania

Tuesday, August 20, 2013

picha DIAMOND ni utata mtupu alimlenga nani soma maoni ya wadau.....

Mashabiki wa Diamond Platnumz hawajaipenda picha yake inayomuonesha akionesha kidole cha kati aka ‘the middle finger’.

“Is this the right finger that you are talkin about @roma2030 …?” ameandika kwenye picha ya Instagram aliyopiga na rapper Roma Mkatoliki


Hata hivyo picha hiyo imevuta hisia za mashabiki wenye hasira waliomwangushia mvua ya madongo kwenye Instagram ambapo ana followers zaidi ya 36,100 hadi sasa. 

Hizi ni baadhi ya comments:
 
Mafuruzenkonoki: Umekua sasa hivi kijana, hizo ishara haziendani na ulivyo! Change! 
 
Lugnno: Umeimba wimbo ma mc mara matus mara bang umekuwa mc naona inshara ya tus kwenye kdole cmon usizd sana hta km upo mbal utakosea km wkt ule ulvua surual takecare man sijaipenda 
 
luvcartel: Astaghafurullah… juzi ulikua muislam leo ushakua kafir? Subhannallah
 
ladisdallaz: The middle finger? To u nt to us 
 
mmolezson: Diamond n Roma nyie wote wajinga tu, mtu yeyote mwenye akili timamu and rational awez point finger lik dat then anapoist kwenye social networks ili jamaa waone.

Alice_aswile: Aah hapana diamond,hivyo vitu hapa cio mahali pake loh,hivyo mfanyie demu wako gheto. 
 
Makitoti: Ain’t ryt diamond ….just ain’t ryt, we love ur music Ila that pic!!!!naaaah,haifai
Mmolezson:
Kwa hyo hcho kidole mnatuoneshea sis ee, hv unawakumbka wasanii hpa Tz ambao walikuwa maaruf kulko nyie? Je saiz wko wp ee na wala hawakuwa na tabia za limbuken kma ww free lancer. I hate u mother***

 
Trofmo: Very disappointin… Ww km Kioo cha jamii unataka tuelewe vip hii picha?! Plz dis z Tz not states! Our culture is decency & dignity!!! Behave..
 
Chocolatedesweetness: This is too much……..!!! Umeanza kulewa mafanikio eeenhe, ngozi nyeusi taaabu sana, U better apologise and delete this photo before its too late!U shauri tu

FAIDA ZA KUFANYA MAPENZI


 1. Mwili kukingwa na kupata mafua ya marakwa mara kwasababu ya kinga mwili inayopambana na maambukizi itwayo imunoglobini A

2. Wanawakehupata mzunguko wa hedhi usiyobadilika badilika kwasababu ya kupata homoni maalumu za mwanaume zittwazo filemoni.

3. Mwili kuwa imara kupambana na msongo wa mawazo.

4. Kushusha mapigo ya moyo yaliyo juu, hii hukufanya ujiepushe na kupata magonjwa ya moyo.

 5. Kuondoa mafuta yenye madhara mwilini na kutengeneza mafuta yenye manufaa mwilini.

 6. Kuteneneza muonekano mzuri wa misuli ya mapajani namwili kwa ujumla.

7. Kuongeza homoni ya kike itwayo istrojeni, hii humfanya mwanamke kuwa mrembo.

 8. Huongeza uwezo wa kutunza kumbukumbu kwenye ubongo, kwasababu ya mzungumko mzuri wa damu wakati wa kufanya mapenzi

9. Huongeza morali ya kazi na kufanya kujisikia vizuri kimawazo.

 http://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/507422-faida-za-kugegedana-hizi-hapa.html

Dalili za mwanaume anayekupenda kwa Dhati


ANAVYOKUTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana kuliko wasiopendana, ambao kiwango chao ni asilimia 30-50.

Hii ina maana kwamba mwanaume anapotumia muda wake mwingi kumtazama msichana na kugeuka taratibu kuangalia vitu vingine kama mtu asiyependa kuacha kumwangalia, ujue anampenda.

MIPANGO
Mwanaume anayekupenda atakushirikisha kwenye mipango yake hasa ya muda mrefu. Mfano akitaka kununua kiwanja, kujenga nyumba atakuambia na pengine kutaka mchango wako wa hali na mali katika kulifanikisha hilo. Ukiona mwanaume anakuficha mambo yake, tambua kuwa huyo ana walakini kwenye penzi la dhati na la muda mrefu.

ATAONESHA HUZUNI
Katika maisha ya mapenzi kuna wakati wa kuhuzunika. Mwanaume mwenye upendo wa dhati atashirikiana nawe wakati wa huzuni na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa unapata furaha.

ATAKUAMINI
Dalili nyingine ya kupendwa na mwanaume ni kuaminiwa kwenye maisha kwa ujumla. Yaani mwanaume anayekupenda hatakuficha kitu, mfano pesa zake, atakupa uhuru kwenye simu yake na kukuamini katika usimamizi wa miradi yake.

ATAKUPA NAFASI
Ninapozungumzia nafasi nina maana atakukaribisha kwake bila hofu na kukupa nafasi ya kuingia na kutoka bila mipaka, atakupa nafasi ya kuweka vitu vyako kwenye kabati na kuruhusu nguo, picha na vitu vyako kuonekana wakati wote chumbani kwake.

UTAKUWA MWANAFAMILIA
Mwanaume aliyefikia chaguo la mwisho kwa mwanamke humshirikisha mpenzi wake kwenye masuala yake ya kifamilia, mfano atamwalika kwenye vikao vya harusi, kipaimara, atatoa nafasi ya kuambatana naye kuona wagonjwa, kusalimia ndugu na atakuwa huru kukutambulisha kwao.

ATAZUNGUMZA NAWE KUHUSU WATOTO
Kwa kuwa wanaume wengi hufikiria kuwa na familia, mwanaume anayekupenda atazungumza nawe mipango ya kupata watoto kwa kuwa atakuwa amekuchagua wewe kuwa mama wa wanaye na atapenda mazungumzo hayo.

ATAKUSAIDIA
Kwa kuwa kukwama ni sehemu ya maisha yetu, mwanaume anayekupenda atakuwa tayari kukusaidia unapokwama. Kila mara atahakikisha kuwa unakuwa na mafanikio na yeye atakuwa tayari kukupunguzia usumbufu wa maisha, kwa kukufuata kazini, kukusaidia baadhi ya mambo na hata ya nyumbani.

ATAJITOLEA
Ninaposema kujitolea ninamaanisha atakuwa tayari kufanya mambo yako na kuyaweka yake nyuma. Kwa mfano akiwa anapenda mpira na siku hiyo kuna mechi, lakini muda huo ukamwambia akufuate kwa mjomba wako atakuwa tayari kuacha furaha yake na kukujali wewe. Huyu ni mwanaume anayekupenda kwa dhati.

ATAAMBATANA NAWE
Wapenzi wengi wasiokuwa na mapenzi ya dhati huona aibu kuambatana na wapenzi wao kwenye mikusanyiko ya watu, lakini mwanaume anayekupenda atafurahia kutoka moyoni kuongozana nawe kwenye halaiki ya watu na kufurahia uwepo wako bila kuona aibu.

Monday, August 19, 2013

MZIGO MPYA "HTC" HUU HAPA

HTC has just launched an Android 4.2.2 Jelly Bean update with its Sense 5 user interface for the HTC One X. For now, only the unlocked European version of the smartphone can benefit from the update, but the rest of the One X owners should get it in the coming weeks.

With Android 4.2.2 and Sense 5 UI, the HTC One X gets features like Blinkfeed, Lockscreen widgets, as well as the Quick settings panel. The latter brings access to 12 different settings with a single swipe. Another user interface enhancement, albeit minor, is the battery level percent indicator next to the battery icon in the status bar.
The gallery app has been also overhauled with video highlights, which come with 12 different themes. There's also auto exposure and autofocus lock available in the camera app. Lastly, the music app enjoys the got visualization with live lyrics.
The Android 4.2.2 update for the HTC One X weighs at 380 megabytes and brings the software version of the device to 4.18.401.2.
HTC has been launching quite a lot of updates for its Android smartphones this summer. Just the week before, the company issued the very same update for the HTC One X+. In July, the company started seeding Android 4.2.2 for its flagship HTC One, and just a day after that the Butterfly got the Android 4.2.2 treatment.

Mtawa wa kanisa katoliki avamiwa na kujeruhiwa huko zanzibar


MTAWA wa Kanisa Katoliki la Bububu visiwani Zanzibar, Sister Irene Ludovik Mwenda (34), amevamiwa na watu wasiojulikana na kushambuliwa na marungu, hali iliyomsababishia maumivu makali mwilini. Sakata la mtawa huyo lilitokea jana, baada ya kuvamiwa na vijana wapatao kumi, baada ya mtawa huyo kuwa anafuga mbwa ambaye inaelezwa kuwa alikula kuku wa mmoja wa vijana hao.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 11 jioni, jirani na maeneo ya Kanisa la Kigango cha Mtakatifu Thesia Beit –el-rus, katika nyumba wanazoishi watawa wa kanisa hilo.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini na Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtu huyo aliyepigwa ni mwanamke ambaye ni mtumishi wa Kanisa Katoliki la Bububu, Zanzibar.

Kamanda Mkadam, alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliosababishwa na tuhuma za mbwa wa mtawa huyo kuwa amekula kuku wa kijana huyo, ambapo baada ya majibizano kijana huyo alipata jazba, hali iliyosababisha kumpiga ngumi mtawa huyo.

Kamanda huyo alisema kuwa baada ya kutokea tukio hilo, mtawa huyo alikwenda kufungua jalada la malalamiko katika Kituo kidogo cha Polisi cha Beit-el-rus, kuhusu kupigwa kwake na kijana huyo.

“Tupo tunaendelea na uchunguzi juu ya tukio hili, kwani ni ugomvi wa mitaani unaweza kuleta athari kubwa zaidi, lazima tufanye kazi hii kwa umakini zaidi,” alisema Kamanda Mkadam.

Hata hivyo alisema kuwa Jeshi la Polisi linamshikilia kijana huyo kwa ajili ya mahojiano zaidi, ili kujua sababu za kushambuliwa kwa mtawa huyo ambapo mpaka sasa yupo mikononi mwa polisi.

Alisema baada ya kesi hiyo kufikishwa polisi, wazazi wa kijana huyo walifanya juhudi za kuzungumza na mtawa Irene ili kuweza kufikia maridhiano na kijana huyo na pindi wakishindwa kuelewana, shauri lao litafikishwa mahakamani.

Hata hivyo kutokana na makubaliano hayo, mtawa huyo alikubali kumsamehe kijana huyo, huku polisi ikisema kutokana na sababu za kisheria na usalama, kijana huyo hataachiwa na jalada la kesi limepelekwa katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, ili atoe ushauri kuhusu sakata hilo.

KAMA ULIPANDA MBEGU SHAMBA LA "DECI" UTARUDISHIWA.......




MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imewahukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya sh milioni 21 vigogo wanne wa iliyokuwa Kampuni ya Development Entrepreneurship for  Community Initiative (DECI ).
  Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Alocye Katemana, pamoja na adhabu hiyo pia ameiagiza serikali ifanye mchanganuo wa mali za DECI ambazo inazishikilia, kwa kuwa zipo mali zilishikiliwa zisizo za kampuni hiyo bali za watu wengine.

Alisema kuwa fedha za wateja wa DECI walizopanda zirejeshwe kwa wateja wenyewe ambao wataonesha uthibitisho wa kweli kuwa walipanda fedha zao huko.
 
Katika hukumu hiyo iliyotolewa na Hakimu Mkazi, Stewart Sanga na kusomwa na Hakimu Katemana, washitakiwa walikuwa watano, ambao ni Jackson Mtares, Dominick Kigendi, Timotheo ole Loitginye, Samwel Mtares na Arbogast Kipilimba.
 
Washitakiwa hao walikuwa wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke.
 
Hakimu Katemana alisema washtakiwa hao ambao ni wachungaji wa makanisa ya Pentekoste wametiwa hatiani kuanzia wa kwanza hadi wa nne, isipokuwa mshtakiwa wa tano ndiye ameachiliwa huru baada ya mahakama kumuona hana hatia katika makosa hayo mawili.
 
“Mahakama imeridhika kuwa upande wa Jamhuri uliokuwa unawakilishwa na Wakili wa Serikali, Prosper Mwangamila na Justus Mulokozi, umeweza kuthibitisha kesi yao na kwa maana hiyo mahakama inawatia hatiani washitakiwa hao wannne na kumwachilia huru mshitakiwa mmoja, kwa sababu mashitaka dhidi yake Jamhuri imeshindwa kuyathibitisha,” alisema.
 
Alisema katika kosa la kwanza kila mshitakiwa atapaswa alipe faini ya sh milioni tatu au kwenda jela miaka mitatu, na katika kosa la pili kila mshitakiwa atatakiwa alipe faini ya sh milioni 18 au kwenda jela miaka mitatu na kwamba mshitakiwa atakayeweza kulipa faini ataachiliwa huru.
 
Kabla ya hukumu, Hakimu Katemana, aliwapatia nafasi mawakili wa pande zote mbili kuzungumza chochote, ambapo Wakili wa Serikali, Mwangamila, alieleza kuwa washitakiwa ni wakosaji wa mara ya kwanza na kwamba makosa waliyoyatenda yana madhara katika uchumi wa nchi, hivyo akaomba wapewe adhabu kali.
 
Wakili wa washitakiwa, Ndusyepo, alidai kuwa wateja wake ni mara yao ya kwanza kutenda makosa hayo ambayo waliyatenda wakati wakiwa katika harakati za kuwakwamua waumini wao katika lindi la umaskini.
 
Aliomba mahakama isiwapatie adhabu kali kwani wateja wake hawana uwezo wa kulipa fidia, ikizingatiwa kuwa wengine ni wastaafu na hawana huwezo wa kifedha.
 
Jana saa 7:00 mchana, Wakili Ndusyepo aliliambia gazeti hili kuwa tayari ndugu wa Domick na Mtares walikuwa wakielekea benki na ofisa wa mahakama kwenda kulipa faini ili waweze kukwepa adhabu ya kwenda jela.

Juni 12 mwaka 2009, washitakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza, baada ya vuta nikuvute kati ya viongozi na wanachama wa DECI .

Wakili Mwangamila alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka mawili ambayo ni kuendesha na kusimamia mradi wa upatu kinyume cha kifungu 111A (1,3) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16.
 
Alidai kuwa, kati ya mwaka 2007 na Machi 2009, katika makao makuu ya DECI , yaliyopo Mabibo Mwisho, jijini Dar es Salaam, washitakiwa waliendesha na kusimamia mradi wa upatu katika sehemu tofauti nchini, kwa ahadi ya kuwapa wanachama wao fedha zaidi ambazo katika mazingira ya kibiashara ni kubwa kuliko mradi waliokuwa wakiufanya.
 
Mwangamila alidai kuwa, shitaka la pili ni kupokea amana za umma bila kuwa na leseni, kinyume cha kifungu cha 6 (1,2) cha Sheria ya mabenki na Taasisi za Fedha Na. 5 ya mwaka 2006 na kwamba, washitakiwa wote katika kipindi hicho wakiwa kwenye ofisi zao za DECI , walipokea amana kutoka kwa umma bila leseni.

-Tanzania daima

SIRI ZA TRAFIKI FEKI ZAFICHUKA,YADAIWA ALIANZA KAZI MKOANI SINGIDA,AKAJIPA UHAMISHO WA KIKAZI HADI DAR...!!

SIKU chache baada ya kukamatwa kwa askari 'feki' wa Usalama Barabarani mwenye cheo cha Sajini, akifanya kazi ya kuongoza magari eneo ya Tabata Kinyerezi, Dar es Salaam, mambo mapya yamezidi kubainika juu ya sababu za mtu huyo kujiingiza katika kazi hiyo bila kutambuliwa na Jeshi la Polisi.


Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vya kuaminika, zinasema trafiki huyo 'feki', ambaye inadaiwa jina lake halisi ni James Juma Hussein (45), mkazi wa Kimara Matangini, alianzia kazi hiyo mkoani Singida kabla ya kujipa uhamisho wa kikazi kwenda Dar es Salaam.

Chanzo chetu kilieleza kuwa, trafiki huyo alikuwa na shemeji yake aliyeitwa Shaban ambaye aliajiriwa na Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani aliyekuwa akifanyia kazi mkoani Tabora.Vyanzo vyetu viliongeza kuwa, baada ya shemeji yake kufariki mkoani Tabora, trafiki huyo alipata mwanya wa kuchukua nguo za kazini alizokuwa akizitumia shemeji yake.



Inadaiwa trafiki huyo 'feki', aliwahi kupata mafunzo ya upolisi katika Chuo cha Polisi Moshi (CCP), mkoani Kilimanjaro lakini alifukuzwa.Chanzo hicho kiliongeza kuwa, baada ya ndugu wa trafiki huyo kufariki dunia, trafiki 'feki', alikuwa akifanya kazi hiyo bila ndugu zake kujua akianzia mkoani Singida bila kushtukiwa.

"Jamaa aliamua kujirithisha kazi ya shemeji yake, alikwenda Singida na kufanya kazi hiyo kwa muda usiojulikana," kilisema chanzo chetu.Chanzo hicho kiliongeza kuwa, kutokana na uchache wa matrafiki mkoani Singida, aliingiwa hofu ya kuweza kujulikana; hivyo aliamua kujipa uhamisho wa kwenda jijini Dar es Salaam.

"Akiwa Dar es Salaam, alifanya kazi hii kwa muda mrefu bila kujulikana hadi alipokamatwa wiki iliyopita akiwa eneo lake la kazi akiongoza magari," kilisema chanzo hicho.Mtoa habari huyo alisema polisi walianza kumtilia shaka trafiki huyo kutokana na adhabu zake alizokuwa akizitoa kwa madereva.

"Tulianza kuwa na hofu naye kwa sababu yeye adhabu zake kwa kila dereva aliyekuwa akimkamata alimtoza sh. 20,000 hadi 25,000," kilieleza chanzo hicho.Sababu nyingine iliyowafanya polisi wamtilie shaka ni utamaduni wake wa kuondoka mapema kwenye kituo cha kazi ambavyo alikuwa akijipangia mwenyewe.

"Trafiki akiwa kazini, inabidi awe kituoni kwake kuanzia asubuhi hadi jioni muda wa kazi unapomalizika, tulishangaa kuona mwenzetu anaingia kazini asubuhi na kuondoka kabla ya muda wa kazi," kiliongeza chanzo hicho.Inadaiwa trafiki huyo alikuwa akifanya hivyo baada ya kukamilisha mahesabu yake aliyokuwa amejiwekea ambapo hali hiyo iliwafanya polisi waanze kujiuliza maswali na ndipo walipoanza kumfuatilia.

Baada ya kufuatiliwa bila yeye kujua, walibaini hata upigaji wake wa saluti ni utata mtupu ambapo kutokana na hali hiyo, waliweka mtego na kufanikiwa kumkamata.
Hadi sasa anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi ambalo limeahidi kutoa taarifa kamili baada ya uchunguzi wao kukamilika

JAMAA ALIYE WATOROKA KINA MASOGANGE SOUTH AFRICA SOON BAADA YA KUKAMATWA.......

Waziri wa uchukuzi Prof. Harrison Mwakyembe alimtaja mshukiwa mmoja wa dawa za kulevya aitaye Nassoro Mangunga  na  kuwataka  polisi  wamtie  nguvuni  popote  atakapoonekana....

Hata  hivyo, mshukiwa huyu pamoja na picha zake alishaandikwa na gazeti la SANI katika toleo lake la Agosti 7-9, 2013 (toleo la 1042) pamoja na namna alivyosafirisha mzigo pamoja na akina Masogange.

Hii  ni  taarifa  ya  gazeti  hilo:


Unaweza kukimbia lakini huwezi kujificha. Msemo huu unaonekana kutimia kwa kijana anayedaiwa kuambatana na watuhumiwa wa dawa za kulevya waliokamatwa Julai 5 mwaka huu nchini Afrika Kusini, Agness Gerald 'Masogange' (25) na Melisa Edward (24), kunaswa na gazeti hili.

 
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, wasichana hao, Masogange na Melisa walisafiri ndege moja na kijana anayejulikana kwa jina la Nassoro Mangunga wakitoka Dar es Salaam kwenda Afrika Kusini, wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), yenye namba SA 189.


Wakiwa katika ndege hiyo Mangunga, Agness na Melisa walikaa kwenye viti vilivyo jirani kabisa huku Mangunga akiwa katikati yao, kwani Agness alikaa kiti namba 23B, Mangunga alikaa kiti namba 23D na Melisa alikaa kiti namba 23A.


Mangunga ambaye ni rafiki mkubwa wa wanamuziki wa Bongo Flava, Rashidi Abdallah Makwiro 'Chid Benz', Mgaza Pembe 'M2theP' na Albert Keneth Mangweha 'Mangwair', wakati akisafiri na mabinti hao walikuwa na jumla ya mabegi tisa kama kumbukumbu za nyaraka za shirika hilo la ndege zinavyoainisha.


Licha ya nyaraka za kusafirishia mabegi hayo kuonesha jina la Agness Gerald ambaye ni mpenzi wa Mangunga tangu mwanzoni mwa mwaka jana, kuwa ndiye aliyelipia mabegi hayo, ila kwenye sehemu ya anuani ya waraka pepe, imeandikwa  Mangunga.


Aidha, mabegi hayo, yalikuwa na kilo 150 za dawa za kulevya lakini kila mmoja alitakiwa kusafiri na kifurushi cha kilo ishirini kama mzigo wa mkononi ambao husafiri bila malipo, hivyo watatu hao kwa pamoja walikuwa na kilo sitini wote kwa pamoja, hivyi kubaki kilo 90 ambazo walizozilipia Dola za Marekani 94 badala ya Dola 450.


Mangunga ambaye licha ya kuishi zaidi nchini Afrika Kusini, lakini pia ni mkazi wa maeneo ya Ilala jijini Dar es Salaam.


Agness na Melisa, walikamatwa Julai 5, 2013 katika Uwanja wa Ndege wa Oliver Thambo, Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya zenye uzito wa kilo 150 aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya Sh bilioni 6.8 za Kitanzania, na walipotiwa mbaroni, walikuwa na mabegi sita tu kati ya tisa waliyokuwa nayo wakati wanapanda ndege jijini Dar es Salaam.


Inasemekana mabegi hayo matatu yaliondoka na Mangunga na kutokomea kusikojulikana....


Mpekuzi blog

Saturday, August 17, 2013

UNYAMA ULIO KITHIRI:::::::: MWANAMKE ABAKWA NA KUCHOMEKWA KISU SEHEMU ZA SIRI HUKO SHINYANGA

mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 30 amekutwa amekufa katika makaburi ya Majengo soko la mjini Kahama mkoani Shinyanga huku mwili wake ukiwa ametobolewa macho na kuonesha kupigwa na kitu kizito usoni.
Mwanamke huyo ambaye hajatambulika jina lake na anakotoka alikuwa amevaa Blauzi nyeusi yenye madoa meupe, viatu vyenye urembo wa silva, mnene kiasi, mweusi na mwenye nywele ndefu.

Mwili wa Mwanamke huyo amegunguliwa leo majira ya saa sita Mchana baada ya watu waliokuwa wanachimba kaburi kuuona mwili huo pembeni ya eneo hilo na kutoa taarifa Polisi.
Kwa mujibu wa majirani wanaoishi eneo la makaburi hayo, tukio hilo linakisiwa kutokea usiku wa kuamkia jana huku baadhi ya kina mama wakisema kuwa walisikia sauti ya mwanamke akipiga mayowe katika eneo la mnadani.
 
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha Majengo  Kaskazini Noel Mseven amesema amepata taarifa kutoka kwa wananchi na baada ya kufika katika eneo hilo walibaini kuwa sehemu za siri za mwanamke huyo ziliingiziwa kitu chenye ncha kali.
 
Jeshi la Polisi wilayani Kahama limethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku Mrakibu msaidizi wa Polisi Aziz Mayunga akitoa wito kwa wananchi kufika katika chumba cha kuhifadhia maiti ili kuutambua mwili huo.

Thursday, August 15, 2013

TINDIKALI YAUZWA KWEUPE.....!!!!


LICHA ya serikali kutangaza kudhibiti upatikanaji holela wa tindikali, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa kimiminika hicho bado kinapatikana kirahisi mitaani..........................BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI»
Mwishoni mwa wiki iliyopita, IGP Said Mwema, Mkurugenzi wa Mashitaka Tanzania, Dk. Eliezer Feleshi na Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samweli Manyele walitoa tamko la kudhibiti upatikanaji holela wa tindikali ambao umesababisha kujeruhiwa kwa watu wengi nchini.

Jumatatu iliyopita, mapaparazi wetu walizama mitaani na kuanza kuisaka bidhaa hiyo ili kuona kama upatikanaji wake una ugumu wowote.
 

Katika maabara moja iliyopo Kinondoni, Dar mapaparazi waliambiwa tindikali inapatikana, nusu lita shilingi 45,000. Maabara moja iliyopo Ilala, bidhaa hiyo inapatikana kwa nusu lita shilingi 30,000, lakini bei inaweza kupungua hadi shilingi 25,000.
 

Mapaparazi hawakuishia hapo, walifika hadi Kipawa jijini Dar ambapo walikutana na mwalimu mmoja wa shule ya sekondari ambaye alisema anaiuza bidhaa hiyo kwa shilingi 16,000 tu na hashushi zaidi ya hapo. Tindikali hiyo ni mali ya shule. Zoezi la kuiandaa likaanza ambapo mwalimu huyo alikuwa akichanganyachanganya malighafi na kupata tindikali kamili.

Ili kuithibitisha kuwa ni tindikali kweli, aliwapa mapaparazi makaratasi maalum (litmus paper) ambayo hutumiwa kufanyia ‘test’ kitaalam. Makaratasi hayo hubadilika rangi toka bluu kuwa mekundu kila yanapokutana na tindikali na kuashiria kuwa ni yenyewe. Wakati akiendelea kuchanganya, mara kadhaa wanafunzi waliingia lakini aliwatoa nduki.

Huku akirekodiwa video kwa siri (ipo Global), mwalimu huyo alisema amekuwa akiwauzia watu mbalimbali bidhaa hiyo na alikiri kwamba huwa hawaulizi wanakwenda kufanyia nini kama ambavyo hakuwauliza mapaparazi wetu.
 

Hadi mapaparazi wetu wanaondoka shuleni hapo, mwalimu huyo hakujua kama wanunuzi waliokwenda kununua tindikali hiyo ni ‘wapelelezi’ mahiri kutoka Global Publishers.  Mitaani watu wanasema tindikali ni silaha mpya ya maangamizi kwa kizazi cha sasa ambapo kila kukicha hofu ya watu kujeruhiwa na kimiminika hicho inazidi kupanda.
 

Mpaka sasa, Watanzania wengi wameshamwagiwa tindikali na watu wanaosadikiwa ni wabaya wao. Miongoni mwa watu waliokumbwa na balaa hilo ni mmiliki wa Home Shopping Center, Said Mohamed Saad, Shehe wa Bakwata wilayani Arumeru, Issa Makamba na mtu  aliyedaiwa ni mpiga debe wa CCM, Igunga  Mussa  Tesha.
 

Wengine ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo, Katibu wa Mufti Zanzibar, Shehe Fadhili Soraga na wasichana wawili raia wa Uingereza, Kirstie Trup na Katie Gee.Chanzo;GLOBAL PUBLISHERS BLOG

SOMA NI MUHIMU::::::: Mapenzi kwa njia ya MDOMO Ni chanzo cha SARATANI YA KOO....


Saratani imeendelea kuwa tishio hapa nchini huku hofu ikiendelea kuikumba jamii kutokana na wataalamu wa afya kushindwa kufahamu tiba halisi ya maradhi hayo hatari. Takwimu kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road zinaonyesha ongezeko la saratani ya mdomo na koo kwa kiasi kikubwa kutoka kesi 167 mwaka 2006 hadi 277 mwaka 2012.

Mkurugenzi wa Idara ya Kinga Ocean road, Julius Mwaiselage anaeleza kuwa watanzania wasipende kuiga mambo ambayo si sahihi bila kujua madhara yake kama kufanya mapenzi kwa njia ya mdomo. “Saratani ya mdomo ipo, na nyingine zinasababishwa na zinaa “ anasema Dk Mwaiselage.

Tafiti za saratani

Tafiti mbalimbali zimewahi kufanyika nchini na kubaini kuwepo kwa ongezeko la saratani ya mdomo.Utafiti uliofanywa na Dk Innocent Mosha wa Kitengo cha Patholojia cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), umebaini aina za saratani 1,594, kati ya hizo 509 zikiwa ni za midomo kwa mwaka 2003 pekee.

Matokeo hayo yanaonyesha kuwa kati ya saratani 509 za mdomo, saratani 242 zilisababishwa na Virusi vya Human Papiloma ambavyo hutokana na zinaa. “Ninachojua mimi ni kuwa Virusi vya HPV husababishwa na magonjwa ya zinaa, hivyo mtu anayeugua saratani ya aina hiyo, imetokana na zinaa,” anasema Dk Mosha.

Wanaume waathirika zaidi wa Saratani

Takwimu hizo ni zile zilizopatikana kwa watu waliokwenda kufanyiwa uchunguzi katika Mkoa wa Dar es Salaam pekee. Dk Mosha anasema kuwa wanaume ndiyo huathiriwa zaidi na saratani ya mdomo ambapo kwa hapa nchini, asilimia 53 ya wanaume waliofika MNH kwa ajili ya vipimo, walibainika kuugua saratani hiyo, huku wanawake wakiwa ni asilimia 47. Utafiti kama huo ulifanywa pia na Dk Amos Mwakigonja, mkuu wa Idara ya Patholojia katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Muhimbili (MUHAS).

Dk Mwakigonja alifanya utafiti wa saratani ya mdomo aina ya Kaposi’s Sarcoma ambapo wagonjwa 78 walibainika na saratani hiyo kuanzia mwaka 1990 hadi 2003. “Saratani za mdomo zipo za aina nyingi na zimetofautiana kulingana na visababishi vyake,” anasema Dk Mwakigonja. Katika utafiti wake Dk Mwakigonja alibaini kuwa wanawake wengi walikuwa na saratani ya mdomo aina ya Kaposi’s Sarcoma kuliko wanaume.

Hata hivyo, utafiti huo ulionyesha kuwa asilimia 50 ya wanaume walikuwa na saratani ya mdomo hatari zaidi (systemic) kuliko wanawake ambao ni asilimia 37.

Mapenzi kwa mdomo husababisha maradhi

Dk Mwakigonja anasema kuwa mapenzi yoyote kwa njia ya mdomo lazima yasababishe maradhi ya zinaa iwapo mmoja ameambukizwa. Pia anasema kwamba sampuli nyingi za wanaume wanaojihusisha na mapenzi na wanaume wenzao (mashoga) zilibainika na saratani ya mdomo. Utafiti huo ni sehemu ya utafiti wa Shahada ya Uzamivu ambao ulionyesha kuwa wagonjwa wengi wa saratani ya mdomo walikuwa ni wanaume wenye umri wa miaka kati ya 38 na kuendelea na wanawake ni 31.

Ufatiti wa WHO Tanzania

Shirika la Afya Duniani (WHO) pia lilifanya utafiti mwaka 2010 nchini kwa kushirikiana na Kituo cha Taarifa za HPV, ambapo ilibainika kuwa asilimia 20 ya saratani za koo na mdomo nchini zinasababishwa na ufanyaji wa mapenzi kwa njia ya mdomo.

Taarifa hizo za WHO zinaeleza kuwa wanaume 747 hugundulika na saratani ya mdomo kila mwaka wakati wanawake 472 hubainika na saratani hiyo pia. Wakati huohuo, wanaume wanaopoteza maisha kutokana na saratani hiyo ni 444, kwa mwaka na wanawake ni 270, kwa mwaka. Utafiti wa WHO umebaini kuwa saratani ya mdomo inashika nafasi ya sita katika aina 24 za saratani 24 zinazoisumbua zaidi Tanzania.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa wanaume wanaoathirika zaidi ni wenye umri wa kati ya miaka 15 na 55, ambao tayari wameshaanza kujihusisha na ngono. Kama maradhi mengine ya kuambukiza, Virusi vya HPV huambukizwa kwa urahisi zaidi kutoka kwa wanawake kwenda kwa wanaume kuliko kutoka kwa wanaume kwenda kwa wanawake. Utafiti huo uliodhaminiwa na mfuko wa Bill na Melinda Gates na Kituo cha Saratani na Mpango wa Utafiti wa Taasisi ya ICO unaeleza kuwa mitandao ya kijamii na picha za ngono ndiyo chanzo cha watu wengi kuiga ufanyaji wa mapenzi ya aina hiyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, tafiti zimefanyika na kubaini kuwa asilimia 70 ya wagonjwa wanaobainika na saratani ya koo na mdomo duniani, husababishwa na Virusi vya Human Pappiloma vinavyotokana na magonjwa ya zinaa.Tafiti hizo zinaonyesha kuwa wagonjwa wengi wanaogundulika na saratani hiyo ni wanaume wenye umri wa kati, wenye uwezo wa kifedha, wasiovuta sigara wala siyo walevi waliokubuhu.

Utafiti huo ulibaini kuwa wanaume wapo hatarini zaidi kupata saratani ya koo inayosababishwa na Virusi vya HPV. Miaka ya 80, idadi ndogo ya watu waliougua saratani ya koo walihusishwa na maambukizi ya Virusi vya HPV. Kihistoria, watu waliobainika na ugonjwa huo, ni wenye umri wa miaka 70 kwenda juu ambao walikuwa ni wale walevi waliokubuhu na wavuta sigara.

Ilielezwa kuwa Virusi vya HPV vipo kwa wingi kiasi ambacho watu wazima wanaojihusisha na ngono ya aina yeyote ile, huweza kupata maambukizi ya zinaa hata kama siyo saratani. Hata hivyo ilibainishwa kuwa saratani isababishwayo na virusi vya HPV ni rahisi kuitibu kuliko saratani ya koo isababishwayo na tumbaku au pombe kali.

Virusi vya HPV ni nini?

Kwa jina la jumla, saratani ya koo au mdomo huitwa saratani ya kichwa na shingo. (Neck and Head Cancer) HPV ni miongoni mwa virusi hatari zaidi duniani visababishwavyo na magonjwa ya zinaa na vinaweza kuathiri sehemu mbalimbali za mwili. Zipo aina zaidi ya 120 za HPV, baadhi huweza kuzalisha usugu (warts) ambazo si saratani katika sehemu za siri, mikononi na miguuni. Maambukizi ya HPV hufanyika kwa urahisi, hata kwa kugusana ngozi au majimaji, huku maambukizi mengine yakisababishwa na ngono.

Virusi hatari na vinavyosababisha saratani ni HPV-16, HPV-18, HPV-31 na HPV 45. Aina hii ya Virusi vya HPV husababisha saratani ambapo uvimbe waweza kujitokeza kwa ndani na unaweza usionekane ukilinganisha na vivimbe vingine vya saratani. Wataalamu wanasema HPV-16 na HPV-18 inahusishwa zaidi na saratani ya shingo ya kizazi na endapo mapenzi kwa njia ya mdomo yatafanywa na mtu mwenye uambukizo huu ni rahisi

Muuaji Wa Bilionea Kilimanjaro Anaswa


Polisi wamefanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiashara tajiri wa madini ya Tanzanite huko Mirerani anayetajwa kuwa ndiye aliyepanga na kukodi watu waliomuua bilionea Erasto Msuya. 

Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zimedai kuwa mfanyabiashara huyo alikamatwa mwishoni mwa wiki na jana na juzi alikuwa akihojiwa na makachero.


Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mfanyabiashara huyo ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki mbili zilizotumika katika mpango huo na pia alitoa fedha kwa ajili ya kununua simu mpya na laini mpya.“Tumewakamata watu wametupa mwanga mzuri na huyo mfanyabiashara ndiye aliyetoa fedha za kununulia pikipiki na siku moja kabla ya tukio zilihifadhiwa nyumbani kwake,” alidokeza polisi mmoja.

Habari hizo zimedai kuwa polisi pia imewahoji mawakala wa kampuni za simu ambao walitumiwa kusajili laini mpya za simu zilizotumika kumpigia marehemu na kutumika kupanga mauaji hayo.

Pikipiki hizo mbili, zilinunuliwa siku moja kabla ya tukio kisha zikahifadhiwa nyumbani kwa mfanyabiashara huyo hadi siku iliyofuata ambapo aliwakabidhi wauaji na zote zimekamatwa.

Mahojiano kati ya mfanyabiashara huyo na Polisi yamekuwa yakifanyika kwa siri na katika kituo cha polisi (jina tunalo) na kwamba mambo ni mazuri ingawa jina lake halijatajwa.

credit  http://networkedblogs.com/O73DM

Tuesday, August 13, 2013

YAMEZIDI SASA:::::: BILIONEA MWINGINE AUAWA KWA KUPIGWA RISASI JIJINI DAR

MAUAJI ya wafanyabiashara wakubwa ‘mabilionea’ yameshika kasi nchini ambapo baada ya tajiri mkubwa Arusha, Erasto Msuya kuuawa kwa risasi hivi karibuni, Agosti 3, 2013 bilionea Elia Daniel Endeni (49) naye aliuawa kwa kupigwa risasi nje kwa mwanamke anayedaiwa kuwa ni mke wake mdogo aitwaye Juliana Labson (28).

Tukio hilo lilijiri siku hiyo saa 2 usiku maeneo ya Temeke Mikoroshini jijini Dar es Salaam ambako ni nyumbani kwa Juliana.
 

Elia alikuwa na kampuni iitwayo Elia Herdons Ltd ya kupakua na kupakia mizigo ya makontena bandarini, maduka na majumba ambapo polisi walikuta shilingi 151,000,000 taslimu ofisini kwake akiwa amezihifadhi.

Ilidaiwa kuwa muda huo, Elia alikuwa amefika nyumbani kwa mwanamke huyo lakini kabla hajashuka katika gari lake, Pick-up lenye namba za usajili T 319 AFJ alichomolewa kwenye gari na kupigwa risasi na watu wawili wasiojulikana.


Taarifa zilieleza kwamba waliotekeleza unyama huo walikuwa wakimfuata marehemu huyo kwa nyuma wakiwa kwenye pikipiki.

Baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili walisema marehemu alikuwa na kawaida ya kufika nyumbani kwa Juliana nyakati za usiku na kabla ya kushuka kwenye  gari, alikuwa akimpigia simu mwanamke huyo ili afungue mlango.

“Ilikuwa wakati anapiga simu ndipo alivamiwa na watu hao ambao walivunja kioo cha gari kwa kutumia kitako cha bastola kisha kutoa ‘loki’ ya mlango na kumchomoa.
 


“Walimdhibiti bila kutoa sauti, wakati huo sisi tulikuwa tumekaa nje tukishuhudia lakini tuliamini kwamba huenda walikuwa wamegongana barabarani kwani hata marehemu hakusikika akiomba msaada,” alisema mwanamke mmoja jirani ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.

Mwanamke huyo aliendelea kusema kwamba hakukusikika mlio wa risasi, bali marehemu alianza kulia ghafla akiomba msaada.

Aliongeza kuwa watu walipokaribia eneo la tukio, wauaji hao walipiga risasi mfululizo hewani, kitendo kilichowafanya watawanyike kuokoa maisha yao na majambazi hayo yakatoweka.

Inadaiwa majirani walipofika, walimkuta tajiri huyo akiwa amelala katika dimbwi la damu huku ameishiwa nguvu kiasi kwamba alishindwa kuongea chochote.

Habari zinasema mke huyo mdogo aliyezaa naye watoto wawili, alipotoka ndani alizimia baada ya kuona Elia akiwa katika dimbwi la damu.

Muda mfupi baadaye, polisi walifika eneo la tukio na kumchukua majeruhi kumpeleka Hospitali ya Temeke ambapo alifariki dunia akiwa njiani.

Taarifa zinadai kwamba Julai 28, mwaka huu marehemu Elia alikoswa na risasi akiwa njiani kwenye gari akitokea msibani Same, Kilimanjaro.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, ACP Engelbert Kiondo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba walifika katika eneo hilo wakiwa na wasiwasi kwamba huenda watu hao walimnyang’anya bastola.


“Ilitubidi twende ofisini kwake Kurasini na kupekua, tukaikuta bastola. Hili suala linaonekana ni kisasi kwa sababu wamemuua bila kuchukua kitu chochote, tunaendelea na upelelezi,” alisema Kamanda Kiondo.

Mazishi ya Elia yalifanyika Jumatano iliyopita, Same ambapo Juliana alikuwa miongoni mwa waombolezaji. Mke mkubwa wa marehemu aishiye Kimara King’ong’o jijini Dar ndiye aliyekuwa ameongoza msiba huo.

Monday, August 12, 2013

CHEKA NA MTANDAO;;;; Atumia Biblia Kumtongoza Msichana na Kumpata!


Jamaa: Hello mrembo, samahani, una mpenzi?
Binti: Hapana. Sina mpenzi.
Jamaa: Kitabu cha Mwanzo 2: 18 “Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”
Binti: Lakini mimi sikupendi jamani.
Jamaa: Waraka wa kwanza wa Yohana 4:8 “Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.”
Binti: Mh! Mi ntajuaje kwamba na wewe unamaanisha hayo maneno?
Jamaa: Injili ya Mathayo 12:34b “Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.”
Binti: Jamani leo kazi. Mi ntajuaje kwamba we ni mkweli na mwaminifu?
Jamaa: Injili ya Marko 13:31 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Binti: Wewe! Na kwanini umekuja kwangu? Wasichana mbona wako wengi tu!
Jamaa: Mithali 31:29 “Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote.”
Binti: We una mambo wewe! Sasa mimi kwangu umependa kitu gani?
Jamaa: Wimbo Ulio Bora 4:7 “Mpenzi wangu, u mzuri pia pia, Wala ndani yako hamna ila.”
Binti: Mh! Huo uongo, mbona mimi hata sio mzuri kihivyo. Unaongeza chumvi tu!
Jamaa: Mithali 31:30 “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.”
Binti: Nikisema nimekukubalia itakuaje?
Jamaa: Mwanzo 2:24 ” Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”
Binti: Jamani we mkaka. Inakuaje unajua maandiko kiasi hicho?
Jamaa: Yoshua 1:8 “Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.”
Binti: Wowwww! Naona unampenda sana Mungu.
Jamaa: Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini.”
Binti: Mh! Haya bwana. Basi nipe muda nifikirie ombi lako.
Jamaa: Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.”
Binti: Mh! Jamani wewe, haya, nimekubali. Mpaka hapo nakupenda tayari!!
Jamaa: Ufunuo wa Yohana 22:21b “Amina”

HII KALI::: Bilionea Msuya kuzikwa leo, jeneza lafunguliwa kwa ‘rimoti’


Arusha. Mazishi ya kifahari yanaandaliwa na familia ya marehemu Erasto Msuya, huku ikielezwa kuwa jeneza litakalotumika kubeba mwili wake linafunguka kwa kutumia ‘rimoti’.
Msuya aliyeuawa wiki iliyopita, anazikwa leo huku familia ikitangaza kutokulipiza kisasi kwa waliohusika, badala yake wamemwachia Mungu.
Kinachovutia katika msiba huo ni jeneza lililobeba mwili wa mfanyabiashara huyo lililoagizwa Nairobi, la aina yake huku likifunguliwa kwa kutumia ‘rimoti’.
Jeneza hilo lililoagizwa kutoka Kampuni ya Montezuma & Monalisa Funeral Home, linafunguliwa kwa kubonyeza kifaa maalumu hata mhusika anapokuwa mbali.
Hali hiyo ilionekana kuwaacha na mshangao maelfu ya waombolezaji waliofika kuaga mwili wakati wa ibada iliyofanyika nyumbani kwake, Kwa Iddi, wilayani Arumeru.
Mfanyabiashara huyo aliyeuawa kwa kumiminiwa risasi zaidi ya 20 na watu wasiojulikana, anazikwa leo nyumbani kwao eneo la Kairo Mirerani, Wilaya ya Simanjiro, mkoani Manyara.
Kaka wa marehemu, Israel Msuya, alisema jana kuwa mazishi hayo yatafanyika makaburi ya familia ya mzee Elisaria Msuya ‘Kikaango’, baba wa marehemu Erasto.
Kwa mujibu wa Kamati ya Maandalizi ya mazishi hayo inayoongozwa na kaka mkubwa wa familia ya Msuya, Gady, zaidi ya Sh100 milioni zimepangwa kugharimia shughuli za maombolezo na mazishi.
Jeneza na gari maalumu la kubebea mwili wa marehemu yameagizwa kutoka Kampuni ya Montezuma & Monalisa Funeral Home ya Nairobi, Kenya kwa gharama ya Sh8 milioni.
Chakula, vinywaji, mapambo na magari ya kukodishwa kutoka Arusha kwenda Mirerani na kurudi yanatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh80 milioni.
Katika hatua nyingine, polisi mkoani Arusha imeendelea kuwahoji wafanyabiashara maarufu wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani, wilayani Simanjiro, wakidaiwa kuhusika na kifo hicho.
Habari zilizopatikana jana zinadai mfanyabiashara mmoja kijana ambaye aliibuka ghafla kuwa tajiri mkubwa kutokana na biashara ya madini ya Tanzanite, anashikiliwa Arusha kwa mahojiano.
Jana, kwenye viunga vya Mji wa Mirerani watu walitangaziwa kuwa mfanyabiashara huyo, alikuwa anashikiliwa kwa mahojiano kuhusiana na kifo hicho.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, hakupatikana mara moja kuelezea suala hilo kwani simu yake ilipopigwa ilikuwa haipatikani.
Marehemu ameacha mke na watoto wanne, huku akiacha rasilimali nyingi ikiwamo jumba la kifahari lililopo Sakina kwa Idd, hoteli maarufu za SG Resort na Mezza Luna zilizopo Arusha.