Saturday, September 7, 2013

Miaka 55 ya uigizaji, aeleza alivyopata jina la Majuto


Katika magazeti ya Mwananchi Wikiendi, tutakuletea mfululizo wa makala kuhusu mchekeshaji na mwigizaji nguli nchini Amri Athumani maarufu King Majuto, ambapo kwa kuanzia anaeleza alivyoanza kazi hiyo hata kuitwa Majuto. Endelea...
Umaarufu wa mtu hauji bila kuwepo sababu, kisa au chanzo hata kumfanya mhusika kutambulika na kujulika katika eneo fulani, jamii hata taifa.
Hili huwatokea watu katika fani au tasnia mbalimbali mfano siasa, uanaharakati, mchezo wa soka, filamu na maigizo.
Ndivyo ilivyo kwa Amri Athumani maarufu King Majuto, ambaye ni mwingizazi na mchekeshaji maarufu nchini anayetambulika na kutajwa kirahisi hata na watoto katika Tanzania hata nje ya mipaka yake.
Kwa maelezo yake, King Majuto amekuwa mwigizaji wa vichekesho kwa miaka 55 sasa, akijivunia mafanikio makubwa na kutambuliwa hata kimataifa.
Umaarufu wake ndiyo uliomsukuma mwandishi wa makala haya kufunga safari hadi eneo la Donge mkoani Tanga yalipo maskani ya Majuto ambaye hata ukimwona tu unaweza kucheka kutokana na vituko vyake vingi vyenye kuvutia na kufurahisha.
Alivyoanza kuigiza
Majuto anaeleza alivyoanza kuigiza akisema: “Nilianza kuigiza mwaka 1958 nikiwa na umri wa miaka 10. Nilikuwa darasa la pili, Shule ya Msingi ya Msembweni mkoani Tanga, kuna siku tukiwa darasani mlevi mmoja alikuwa akipita karibu na shule yetu, huku akipiga ngoma kwa nguvu.”
Anaongeza:”Mwanafunzi mmoja akajiunga kucheza huku mlevi yule akizidi kusogea na kuongeza mdundo, mwalimu aliyekuwa akifundisha alikasirika na kumtuma mwanafunzi mwingine kumfukuza yule mlevi, lakini badala ya kumfukuza mlevi na kumwita mwanafunzi anayecheza naye akajiunga kucheza.”
Anasema kuwa mwalimu alivyoona hivyo, alitoka nje ya darasa kwa kishindo na kwenda kumfukuza yule mlevi, lakini cha kushangaza wakati mwalimu alipomkaribia yule mlevi alianza kutingisha mabega yake kufuatisha mdundo ya ngoma, badala ya kumfukuza mlevi naye alijiunga na kuanza kucheza.
“Baada ya dakika tano kama shule nzima ilikuwa ikicheza ngoma, na baada ya hapo niliazimia kuwa msanii kwa kuwa sanaa ilimlainish hata mwalimu wetu aliyekuwa mkali kupita kiasi,” anasimulia Majuto.
Anaongeza kuwa mwaka 1966 alimaliza darasa la nane na mwaka uliofuatia alijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), ambapo walikuwa wakilipwa Sh20 na kufanya kazi hadi mwaka 1970, alipolazimika kuacha kwa sababu alikosa nafasi ya kufanya sanaa kama ndoto zake zilivyokuwa zikimtuma tangu 

No comments:

Post a Comment