Tuesday, August 27, 2013

yaliyo jiri jana:::::ACTRESS AUNT EZEKIEL ACHANWA VIBAYA NA CHUPA AKIWA CLUB.

Actress maarufu Swahiliwood Aunt Ezekiel amechimbwa na kitu chenye ncha kali kinachodaiwa kuwa chupa katika mkono wake wa kushoto. Tukio hilo lilitokea juzi katika ukumbi wa Club Billicanas wakati Wema Sepetu akitambulisha wasanii wapya wa Bongofleva. Habari ambazo bado sio rasmi ni kuwa huenda muigizaji huyo alikumbwa na tukio hilo hatari kutokana na issue za kimapenzi yaani kugombea mwanaume siku za nyuma au sasa. Tutakujuza zaidi kinachoendelea. Ugua pole Aunt. Angalia picha chini jinsi actress huyo alivyojeruhiwa.......


http://swahiliworldplanet.blogspot.com/2013/08/actress-aunt-ezekiel-ajerehiwa-vibaya.html (source)
Mkono uliojeruhiwa kabla ya kufungwa
                                                 Baada ya kufungwa







Mama ajifungua watoto wawili walioungana Dar, mmoja hana kichwa

Share  Print

Mkazi wa Zanzibar, Pili Hija akiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam jana na watoto wake walioungana.  Picha na Juliana Malondo
Mtoto huyo ambaye hana kichwa anapumua pia akiguswa anapata hisia na kutingisha mguu mmoja.
Dar es Salaam. Mkazi wa Jang’ombe Visiwani Zanzibar, Pili Hija (24), amejifungua watoto walioungana huku mmoja akiwa hana kichwa.
Watoto hao ambao wapo Wodi namba 36 katika Jengo la Wazazi la Hospitali ya Taifa Muhimbili mbali na kuzaliwa mmoja akiwa hana kichwa, wameungana sehemu ya uti wa mgongo, mkono mmoja na wanatumia njia moja ya haja kubwa.
Akizungumza na mwandishi wetu jana, mama wa watoto hao, alisema: “Nilijifungulia nyumbani, nilisikia uchungu mara moja na hapo hapo nikajifungua kwa njia ya kawaida na jirani yangu ndiye aliyenisaidia,”alisema na kuongeza:
“Nilijifungua saa moja  asubuhi, nilijua nitazaa pacha kwa kuwa nilishafanya kipimo katika Hospitali ya Makunduchi, wakaniambia nitajifungua pacha lakini mmoja si binadamu ni kiwiliwili.
“Nimeolewa, mume wangu ni mwanajeshi, nina watoto wengine wawili mmoja wa kike na mwingine wa kiume, mume wangu hajui tukio hili kwani yupo kambini Zanzibar na hatuna mawasiliano yoyote kwa sasa,” alisema.
Daktari wa Upasuaji wa Watoto Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dk Zaituni Bokhary alisema; “Hii ni mara ya kwanza kwa jambo hili kutokea katika miaka ya hivi karibuni. Mara ya mwisho lilitokea mwaka 1984.
“Tulikuwa tufanye upasuaji leo lakini tumeahirisha na utafanyika Alhamisi (kesho) asubuhi katika Kitengo cha Mifupa cha Muhimbili (Moi).”
Msimamizi wa Wodi ya Watoto walikolazwa, Dk Edna Majaliwa  alisema: “Hakuna sababu maalumu kitaalamu  inayosababisha watoto kuungana, mara nyingi zinapokutana mbegu za X na Y na kutengeneza mimba kunakuwa na hatua za ukuaji wiki nne, wiki nane, wiki 12, 16 na kuendelea.

KAGAME HATAKANYAGA TENA ARDHI YA TANZANIA.....WABUNGE WA RWANDA WASUSA JIJINI ARUSHA

RAIS Paul Kagame wa Rwanda, sasa hayupo tayari kukanyaga ardhi ya Tanzania kutokana na kile kinachoonekana kuwa ni mgogoro wa kidiplomasia unaoendelea kati yake na Rais Jakaya Kikwete.

Wakati hayo yakifikia hapo, kikao cha Bunge la Afrika Mashariki (EALA), linakoketi mjini Arusha kilivunjika baada ya Spika wa bunge hilo, Magreth Zziwa, kugongana kauli na Mbunge mmoja wa Rwanda jambo lililosababisha wabunge wote wa Rwanda kususia kikao na kutoka nje ya ukumbi wa Bunge.

Mwenendo wa hayo yaliyojitokeza jana katika Bunge la Afrika Mashariki hadi kikao kuvunjika, msingi wake ni mgogoro unaowagusa wakuu hao wawili wa dola.

Habari zilizolifikia gazeti hili toka katika vyanzo vyake mbalimbali vilivyo ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, lakini pia katika vikao vya Bunge hilo la Afrika Mashariki vinavyoendelea jijini Arusha zinaeleza kuwa, Rais Kagame hata kama ataalikwa kuja nchini leo, hatakuja.

MTANZANIA Jumatano limedokezwa kuwa jambo hilo tayari limethibitishwa na Wabunge wa Rwanda wanaohudhuria vikao vya (EALA).

Taarifa toka ndani ya Bunge hilo zilizolifikia MTANZANIA Jumatano zinaeleza kuwa, tayari mzimu wa msigano huo uliojitokeza baina ya wakuu hao wawili wa dola, umeanza kuwavuruga wabunge hao baada ya jana kikao cha Bunge hilo kuvunjika, kutokana na kuibuliwa kwa hoja ya kutaka vikao vya Bunge hilo kufanyika kwa utaratibu wa kuzunguka kila nchi.

Zinaeleza zaidi kuwa; Ni katika hoja hiyo wabunge wa Kenya na Rwanda walionekana kuungana na kuwa kitu kimoja na hivyo kususia kikao hicho cha jana, jambo ambalo lilimlazimisha Spika wa Bunge hilo, Magreth Zziwa kuvunja kikao.

HALI ILIVYOKUWA

MTANZANIA Jumatano limedokezwa kuwa, wabunge hao walianza kutoka ndani ya kikao kilichokuwa kikiendelea jana, baada ya mmoja wa wabunge hao kutoka Rwanda, James Ndahiro kuomba mwongozo kwa Spika.

Habari zinaeleza kuwa chanzo cha mbunge huyo wa Rwanda kuomba mwongozo, kilitokana na Mbunge kutoka Kenya, Peter Mathuki kutoa hoja ya kutaka suala la vikao hivyo kufanyika kila nchi wanachama, lijadiliwe.

“Sasa baada ya mbunge huyo wa Kenya kutaka suala la vikao vya Bunge kufanyika kila nchi wanachama yaani ‘rotation’ lijadiliwe pale kikaoni, Spika akamwambia hilo ni jambo la haraka sana na ikizingatiwa imebaki wiki moja vikao viishe na kwamba kama anataka lizungumziwe, alilete kama ‘motion’.

“Baada ya Spika kujibu hivyo, ndipo mbunge wa Rwanda akaomba mwongozo kwa Spika…Spika akamjibu kwamba anataka mwongozo gani tena wakati ameshamjibu yule wa Kenya, ndipo wabunge wa Rwanda wakatoka ndani ya kikao wakisema hawataki kuburuzwa huku wakifuatiwa na wa Kenya.”

Taarifa zaidi zilieleza kuwa kitendo hicho ambacho kilisababisha kikao kuvunjika, kilikwamisha kuapishwa kwa Waziri mpya wa EALA kutoka Rwanda.

Ilielezwa kuwa baada ya wabunge hao kutoka, Spika aliahirisha kikao kwa kutumia kanuni kwamba, baada ya dakika 15 warudi.

“Baada ya dakika 15 tuliporudi, wabunge wakawa wachache huku wale wa Rwanda na Kenya hawakurudi tena na waliorudi walikuwa jumla 13 pamoja na Spika kati ya wabunge 45. Ndipo Spika akasema hatuwezi kuendelea na kikao kutokana na uchache wa wabunge, hivyo kikaahirishwa hadi kesho (leo),” kilisema chanzo chetu hicho.

Hata hivyo wakati hayo yanajitokeza, utaratibu wa vikao vya Bunge la Afrika Mashariki  unaelekeza kuwa vitafanyikia Arusha ambako ni makao makuu.

Habari zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa, Kamati ya kuratibu Mambo ya Bunge iliyokutana Entebe Uganda, ilipanga kuwa kwa mwaka vikao vya Bunge vitakuwa sita huku vitatu vikifanyika Arusha ambako ni makao makuu, kimoja Nairobi na vingine viwili bado haijajulikana.

Pamoja na Kamati kufikia uamuzi huo, bado inaelezwa kuwa baadhi ya wabunge wanapinga vikao hivyo kuendelea kufanyika na hasa wa Rwanda ambao inadaiwa kuwa wamepewa maagizo fulani kutoka kwenye Serikali yao

Mbali na hilo la vikao, nyufa nyingine zinazoelezwa kuhatarisha msingi wa Bunge hilo, ni kile kinachodaiwa kuwapo kwa utendaji wa upendeleo wa Spika, Margaret Zziwa.

Kwamba Spika Zziwa amekuwa akishutumiwa kupanga safari za nje kwa upendeleo na kwamba hazieleweki zinapangwaje.

KAGAME KUTOKANYAGA TANZANIA

Wakati hayo yakijiri, imeelezwa kuwa hata Rais Kagame, akialikwa kuhutubia vikao vya Bunge hilo, hataweza kuja nchini kutokana na mgogoro uliopo.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili toka ndani ya bunge la EALA, zinaeleza kuwa wabunge kutoka Rwanda wananung’unika vikao kufanyika Arusha na wameeleza bayana kwamba itakuwa vigumu kwa rais wao kuja hapa nchini endapo ataalikwa na Spika wa Bunge hilo kuja kuhutubia katika vikao hivyo.

“Kwa kawaida vikao vya bunge vinapofanyika, mara nyingi anayehutubia vikao ni Mwenyekiti wa EAC, ambaye kwa sasa ni Yoweri Museveni na rais wa nchi ambako vikao vinafanyika, lakini wakati mwingine spika anaweza akaamua na kumteua rais kutoka nchi yoyote.

“Sasa Spika akimteua Kagame ni dhahiri itakuwa ngumu kuja Tanzania kutokana na mgogoro unaoendelea baina yake na Rais Kikwete,” kilisema chanzo chetu hicho cha habari.

Msigano wa kauli baina ya viongozi hao wakuu wa dola, ulijitokeza baada ya Rais Kikwete kutoa ushauri kwa Rais Kagame wa kukaa meza moja na waasi wa FDLR.

Hata hivyo baada ya siku chache, Kagame alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Rwanda akimkejeli Kikwete hadi kufikia kutoa kauli zenye vitisho dhidi yake.

Tangu Rais Kikwete alipotoa ushauri huo, Kagame amekuwa akiendelea kutoa lugha zisizo na staha kwa Tanzania.

Baadhi ya vyombo vya habari nchini Rwanda, navyo vimekuwa na mwelekeo huo huo, ambapo hivi karibuni vilianza kuhusisha ushauri huo wa Rais Kikwete kuwa msingi wake unatokana na undugu uliopo kati ya mke wake, Mama Salma Kikwete na wabaya wa Kagame.

Kwamba mke wa Rais Kikwete ni binamu wa kiongozi wa zamani wa Rwanda, Juvenal Habyarimana, habari ambazo zimekanushwa vikali na Serikali.

Ni katika mwenendo huo huo, wiki iliyopita ilibainika kuwa Rwanda na Uganda zinakusudia kutangaza kujitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam kuanzia mwezi ujao.

Katika hilo, leo Marais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Yoweri Museveni wa Uganda pamoja na Paul Kagame wa Rwanda, wanatarajiwa kuzindua Gati ya bandari ya Mombasa yenye thamani ya dola za Marekani milioni 66.7 ambayo ni zaidi ya Sh bilioni 100 za Kitanzania.

Bandari hiyo ambayo itaongeza uwezo kwa asilimia 33, Rais Museveni ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya Afrika Mashariki (EAC), ataongoza zoezi hilo la uzinduzi.

Baadhi ya wachambuzi wa sayansi ya kiuchumi, wanasema kuwa endapo Rwanda na Uganda zitajitoa kutumia bandari ya Dar es Salaam, hizo zitakuwa ni habari mbaya kwa nchi.


 -Mtanzania

Lukuvi: Wabunge wengi wamo orodha ya dawa za kulevya


 Print 

Dodoma. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi amesema baadhi ya majina ya wabunge yametajwa miongoni mwa watu wanaoshukiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya lakini Serikali haiwezi kuwataja hadharani kwa haraka.
Majibu hayo ya Waziri Lukuvi yamekuja baada ya wabunge kumbana na wengine wakizomea baada ya kueleza ugumu wa kutaja majina ya washukiwa pasi na ushahidi wa kutosha.
“Serikali haiwezi kutaja majina haraka kiasi hicho kwani inaogopa kukurupuka na kushindwa mahakamani, hivyo lazima tuwe makini sana na jambo hilo. Hatuwezi kukurupuka tu eti ni fulani wakati hatuna vithibitisho.
“Kumbukeni wengine mpo humu ndani ya Bunge na tukianza wengi mtakwisha maana katika orodha hiyo kubwa na ninyi mmo na orodha ni kubwa kweli ambayo wakati mwingine inatakiwa umakini wa hali ya juu,” alisema Lukuvi alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Karatu (Chadema), Mchungaji Israel Natse.
Katika swali lake ambalo lilisababisha kelele za kuzomea, Natse alitaka majina hayo yatajwe hadharani. Hata hivyo, hali ilitulia baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuingilia kati na kusema: “Hii tabia ya zomeazomea siitaki humu ndani, acheni tabia hiyo lazima mumsikilize mtu kwa kile anachokisema kwanza lakini mtindo huu si mzuri...”
Patashika hiyo ilitokana na swali la Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Catherine Magige aliyetaka kujua iwapo Serikali inaweza kuwaambia Watanzania ukubwa wa biashara hiyo nchini na kama haioni kama kuna tatizo katika ukaguzi wa abiria na mizigo katika viwanja vya ndege na juhudi za Serikali kumaliza tatizo hilo.
Akijibu swali hilo, Lukuvi alisema ukubwa wa biashara hiyo hapa nchini unadhihirishwa na idadi ya Watanzania 274 waliokamatwa kati ya mwaka 2008 hadi Julai mwaka huu kwa kosa la kujihusisha na dawa za kulevya katika nchi mbalimbali za nje.
Alisema Serikali inafahamu ukubwa wa tatizo la matumizi ya biashara hiyo haramu ya dawa za kulevya nchini na alitaja takwimu za ukamataji wa dawa hizo katika kipindi cha kuanzia mwaka 2000 hadi Machi, 2012.
Alisema pamoja na kukamatwa kwa Watanzania hao nje ya nchi, wageni 31 wanashikiliwa mahabusu katika Magereza ya Keko na Ukonga, Dar es Salaam ambao ni raia wa Iran, Pakistan, Senegal na Afrika Kusini.
Hata hivyo, katika swali lake la nyongeza, Magige alisema uteketezaji wa dawa zinazotajwa kukamatwa umekuwa wa siri kiasi cha kutiliwa shaka kuwa huenda zinachukuliwa na maofisa waliozikamata ndiyo maana hakuna uwazi.
Kuhusu hilo, Waziri Lukuvi alisema suala la uteketezaji wa dawa hizo hauko wazi kutokana na sheria zilizopo kutotoa nafasi ya kuteketezwa mapema kwa kuwa zinatumika kwa ajili ya ushahidi akisema wakati mwingine hukaa zaidi ya miaka 10.

FOOLISH AGE" YA LULU YAENDELEA KUWA GUMZO NCHINI




Msaani mwenye kipaji cha Hali ya juu nchini na Mwenye umri mdogo Elizabeth Michael "LULU"anatarajia kuzindua filamu yake ya Kwanza tokea alipotoka Gerezani, Filamu hii iitwayo FOOLISH AGE ikiwa imetengezwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited itazinduliwa Mnamo tarehe 30 August 2013 Katika Ukumbi wa Mlimani city jijini Dar Es Salaam. 

 

Filamu hiyo inayoelezea Maisha ya kila binadamu katika kila hatua anayopitia katika ukuaji wake.Ni moja ya filamu nzuri na yenye ubora wa hali ya juu kutokana na Sauti,Picha hadi maeneo yaliyotumiwa kucheza filamu.Pamoja na kuwepo lulu humo pia utamuona Msanii Mkongwe Jengua.Filamu hiyo imetengenezwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited na Itakuwa ikisambazwa Na Proin Promotions Limited.Katika Uzinduzi huo wa Filamu hiyo ya Lulu Wasanii mbalimbali akiwemo mwanamuziki Lady Jaydee na Machozi Band anatarajiwa kushusha bonge moja la burudani ya kufa mtu.

Monday, August 26, 2013

BALE KUVUNJA REKODI YA CHRISTIAN RONALDO


Real Madrid and Tottenham have agreed a world record €100 million deal for Gareth Bale to join Real Madrid.

Spurs chairman Daniel Levy finally accepted the Spanish giants’ offer on Sunday and official confirmation of the transfer is expected to be made imminently.
ALL SET FOR MADRID
Alberto Pinero | Goal Spain
Bale isn't officially a Real Madrid player yet - but you wouldn't have thought that by the way he is being paraded in Madrid. He is all over the sports newspapers, radio stations and TV sports news channels. And let's not forget he's been the talk of the Real Madrid, and even Barcelona, press conferences.

It has been this way for several weeks now. Even at the Santiago Bernabeu as early as last Thursday there were people wearing the Madrid shirt with 'Bale 11' emblazoned on the back.

The clubs have come to an agreement on a straight cash deal to be paid in three installments, as Bale becomes the most expensive player in history, eclipsing the €93m Madrid paid Manchester United for Cristiano Ronaldo in 2009.

Tottenham have spoken to Madrid at length about including players in the deal, but left-back Fabio Coentrao is not part of the agreement while Real refused to include young striker Alvaro Morata in the transfer.

Bale is expected to sign a six-year contract at the Santiago Bernabeu reported to be worth €10m a year after tax, where pictures emerged on Friday of the club setting up a stage inside the stadium for his presentation to the supporters.

Tottenham’s decision to accept Real’s offer brings to an end a protracted summer of speculation and negotiations over the Welshman’s future.

Bale shocked Spurs when he told the club he wanted to leave during their pre-season tour of Hong Kong in July while Real Madrid were very public in their courtship of last season’s PFA Player of the Year.

Perez was desperate to make Bale his latest galactico signing after missing out to Barcelona in the race for Brazilian star Neymar at the start of the summer.

Bale has spent the weekend in Marbella in Spain having been given two days off by Villas-Boas, and he is expected to return to England briefly on Monday before flying out to Madrid.

Tottenham are hoping to conclude a €35m move for Roma winger Erik Lamela in the next 48 hours, with the Argentine considered a direct replacement for Bale, who was pencilled in to play on the right of a front three this season.

Spurs have agreed the basics of the deal but remain cautious following Willian’s decision to join Chelsea from Anzhi Makhachkala despite completing a medical and agreeing terms with the north Londoners.

Romanian centre-back Vlad Chiriches is also expected to join from Steaua Bucharest this week in a €9.3m deal, while manager Andre Villas-Boas still wants a left-back and a creative player before the transfer window closes on September 2.

Sunday, August 25, 2013

NICK MBISHI ATANGAZA RASIMI KUWA YEYE NI MUATHIRIKA WA UKIMWI


Tumekuwa  tukishuhudiwa  vituko  mbalimbali  vya  wasanii wetu  ambao  wamekuwa  wakihangaika  usiku  na  mchana  kuusaka  umaarufu....

Wapo  ambao  wamekuwa  wakivua  nguo  zao  jukwaani, wapo  ambao  wamekuwa  wakipiga  picha  za  uchi  na  kuzitupia  mitandaoni.Yote  hiyo  ni  kutafuta  Jina  au  umaarufu ambao  mimi  binafsi  nauita  ni  umaarufu  wa  kishamba.....

Leo  Nick  Mbishi  ametoa  kituko  ambacho  kimenifanya  niamini  kuwa  wasanii  wetu  wana njia  mpya  kwa  sasa  za  kutaka kujulikana ( kuwa  maarufu).

Katika  account  yake  ya  Twitter, Nick  Mbishi  alitoa  post  moja  ikielezea  kuwa  yeye  ni  muathirika  wa  ukimwi.

Post  hiyo  ilikuwa  na  taswira  mbili  za mafumbo . Fumbo  la  kwanza  linamaanisha  kuwa  Yeye  NI  mwathirika  wa  UKIMWI  huku  fumbo  la  pili  likimaanisha  kinyume  chacke.

Baada  ya  post  hiyo, mijadala  kadhaa  ya  watu iliibuka  kwenye  mitanado  ya  jamii.Wapo waliompa  pole  na  wapo  waliompongeza  kwa  ujasiri  wake...

Cha  kushangaza  ni  kwamba, baada  ya  Nick  kuona kuwa issue  imekuwa  serious  kuhusu  madai  ya  yeye  kuwa  na  UKIMWI, alirudi  tena  Twitter  na  kuanza  kuilaumu  mitandao  ya  kijamii....

Kinachonishangaza  ni  kwamba, Nick  anakaumu  nini  wakati  alitamka  mwenyewe??.Hizo  ni  sifa  za  kishamba  za  kutaka  jamii  ikuongelee  na  kukujadili...

Kama  umeamua  kujitangaza, basi  kuwa  serious  ili  watu  wajue  moja.

Hii   ndo  post  yake.

http://freebongo.blogspot.com/2013/08/nick-mbishi-atangaza-rasimi-kuwa-yeye.html

Friday, August 23, 2013

KILA MTU ATAKUA NA MAONI YAKE KWA HII PICHA ::::::::pic of the day::::::::::::

CREDIT: mwananchi.

TUNDAMAN AFANIKIWA KUWATOROKA POLISI AKIWA NUSU UCHI....KISA NI DENI LA LAKI NANE


Msanii Tundaman amejikuta akiambulia aibu ya mwaka baada ya kujitosa nusu uchi mtaani akiwakwepa askari polisi ambao walivamia kwake leo asubuhi kwa lengo la kumkamata....

Chanzo cha Tunda man kusakwa na polisi ni deni la sh. laki nane ambazo alikopa mwanzoni mwa mwaka huu kwa mwanadada mmoja ( jina kapuni).... 

Taarifa zinadai kwamba, baada ya kupewa hela hiyo, Tunda man aligeuka kisima cha matusi ya nguoni kwa mrembo huyo. Kila akipigiwa simu alikuwa hapokei, na akipokea ni matusi ya nguoni..... 

Baada ya hali hiyo, mwana dada huyo aliamua kulifikisha swala lake polisi ambapo Tundaman alikamatwa. Akiwa mikononi mwa polisi, msanii huyo aliomba apewe nafasi ya kulilipa deni lake kwa awamu tatu kuanzia tarehe 12/8/2013 

Baada tarehe hiyo, Tundaman hakuweza kulipa kiasi chochote na wala hakutoa ushirikiano wowote, hali iliyomfanya mwanadada huyo arudi kuripoti polisi.... 

Polisi walianza jitihada za kumsaka ambapo leo majira ya saa nne asubuhi walivamia kwake ( Tabata Savana ) kwa lengo la kumkamata..... 

Bahati nzuri au mbaya, Tundaman alifanikiwa kuwatoroka polisi akiwa na bukta tu ( kwa mujibu wa mashuhuda) na kutokomea kusikojulikana...

Ifuatayo  ni  HATI  YA  MAKUBALIANO  yao  ambayo  mpekuzi  wetu  amefanikiwa  kuipata....

Kama kuna jambo ambalo linaichafua Tanzania katika jukwaa la kimataifa kwa siku hizi, basi ni tatizo la usafirishaji wa dawa za kulevya.
Zamani tatizo hili halikuwa kubwa sana, ni mtanzania mmoja mmoja sana alikuwa akikamatwa nje kwa kusafirisha dawa za kulevya. Kwa hiyo jina la nchi yetu lilikuwa linasikika mara moja moja sana au kwa bahati mbaya kuhusiana na tatizo la dawa za kulevya. Lakini katika siku za hivi karibuni tumesikia kuwa kuna watanzania wanakamatwa Ulaya, Amerika Kaskazini, Amerika Kusini, Asia na hata katika nchi za Afrika, kama ilivyotokea majuzi huko Afrika Kusini. Kwa sasa ukisikia jina la Tanzania linatajwa kuhusiana na tatizo la dawa za kulevya, si bahati mbaya tena na si mara moja moja kama zamani.
Serikali yetu imekuwa ikijitahidi sana kujenga jina zuri la Tanzania na kuitanganza Tanzania kuwa ni kisiwa cha amani, nchi yenye vivutio vingi vya utalii na yenye ukarimu kwa wageni. Na kweli kama ukitembelea nchi yoyote yenye watu wanaoifahamu Tanzania, si vigumu kusikia Tanzania ikisifiwa, lakini kama ukiona mtu amekaa kimya, basi ujue kuna uwezekano kuwa hataki kutaja suala la dawa za kulevya.
Mwanzoni nilikuwa naamini kuwa watanzania ni watu wenye maadili ambao wanapokwenda nje ya nchi wanakumbuka kuwa “mabalozi wazuri” wa nchi. Lakini baada ya kutembelea sehemu mbalimbali duniani, hasa nchi za Asia na Asia Kusini Mashariki, na kukutana na wenyeji na kuwauliuza mtazamo wao kuhusu Tanzania na watanzania, nikagundua kuwa sifa zote nzuri za Tanzania zinafunikwa na sifa mbaya moja au mbili. Kubwa ni tatizo la dawa za kulevya, na nyingine ni ukahaba (Hong Kong).
Pamoja na kuwa ni watanzania wachache sana wanaosafirisha dawa za kulevya, ni hao wachache ndio wanaofanya jina la watanzania wengine walio wengi lichafuke, na kuwafanya watanzania wanaokwenda nje ya Tanzania kwa malengo halali, kama vile biashara, michezo na hata utalii, wakumbwe na matatizo wasiyostahili.
Zamani nilikuwa ninakasirika sana ninapotolewa kwenye mstari wa uwanja wa ndege na kuanza kupekuliwa na kuulizwa maswali ‘ya kipuuzi’, kana kwamba mimi ni mhalifu au mtuhumiwa wa uhalifu. Nilikuwa najihisi kuwa mimi ni mhanga wa ubaguzi wa rangi, kitu ambacho sikutegemea kutoka kwa nchi marafiki zetu. Kuna wakati hata nilifikia hatua ya kukwaruzana na maofisa wa uwanja wa ndege, kwa kuona wananitendea isivyostahili. Lakini baadaye baada ya kuangalia hali halisi na kuona matendo yanayofanywa na baadhi ya watanzania wanaokuwa nje ya Tanzania, nikagundua kuwa wasiwasi walionao maofisa wa viwanja vya ndege vya nchi za Asia kuhusu watu wenye pasi za kusafiria za Tanzania, ni wa haki na unaeleweka, si ubaguzi wa rangi na si ubaguzi dhidi ya watanzania. Kama ni ubaguzi wa rangi, basi matendo ya baadhi yetu ndio yanawapa kisingizio cha kufanya hivyo.
Kinachonifanya nisione kuwa ni ubaguzi wa rangi ni kuwa, nchini China kwa mfano kuna adhabu kali sana kwa watu wanaokamatwa kwa makosa ya dawa za kulevya, wachina wengi wamehukumiwa adhabu ya kifo. Lakini cha ajabu ni kuwa watanzania wanaokamatwa kwa makosa sawasawa na wanayofanya wachina, wanapewa vifungo virefu na adhabu ya kifo, lakini hadi sasa hakuna mtanzania aliyenyongwa ikilinganishwa na wachina na wafungwa wa mataifa mengine.
Kumekuwa na habari za kupotosha kwenye baadhi ya vyombo vya habari vya Tanzania kuhusu jambo hili, lakini ukweli ni kuwa Mpaka sasa hakuna mtanzania aliyehukumiwa adhabu ya kifo kwa makosa ya dawa za kulevya na adhabu yake kutekelezwa. Ni vigumu kujua ni kwanini China haijawanyonga watanzania, lakini ukiangalia sababu ya wachina kutowachukulia hatua kali watanzania, utaona kuwa wanathamini sana urafiki uliojengwa na viongozi wetu, hasa mwalimu Nyerere na mzee Salim Ahmed Salim. Kwa hiyo ukiona jinsi wenyeji wanavyochukuliwa hatua kali, na sisi watanzania “kudekezwa”, hata ukikutana na vitendo vinavyokukosesha raha unapopita uwanja wa ndege, basi inabidi uwe mpole mara moja.
Pamoja na kuwa kila suala la dawa za kulevya linapotajwa, utakachoona kwenye vyombo vya habari ni kuwa kuna mtandao mkubwa wa siri, lakini ni kama tunapuuza madhara yanayoletwa na jambo hili kwa uhusiano kati ya nchi yetu na nchi nyingine, na usumbufu linaoleta kwa watanzania wengine wasio wasafirishaji wa dawa za kulevya.
Inasikitisha kuona kuwa kati ya watu kutoka nchi za Afrika Mashariki, ni watanzania ndio wanaokamatwa zaidi na dawa za kulevya kuliko wale wakenya na waganda. Na hata watanzania wanaokamatwa, wengi wanatoka katika Mikoa miwili ya pwani, ambako baadhi ya vijana wanaona ni “ujiko” kusafirisha dawa za kulevya. Ukiongea na vijana hao, unaweza kuona kuwa hawana elimu hata kidogo, kwani hata uwezo wao wa kuandika kwa Kiswahili na uwezo wa kuongea Kiswahili na kujenga hoja ni mdogo sana, ndio maana inaonekana ni rahisi kwao kurubuniwa kuliko vijana wa Kenya, Uganda na wa nchi nyingine za Afrika Mashariki. Wengi wao wanasema wanaahidiwa kati ya dola elfu mbili na elfu nne wakifikisha “mzigo” salama. Kwa kweli hizo si pesa nyingi ikilinganishwa na hatari ya kazi yenyewe, na hasa ukizingatia kuwa kwa mtanzania anayejituma kufanya kazi nyumbani, anaweza kupata pesa hizo.
Kwa hapa China, mpaka sasa naweza kusema kwa sasa tatizo limefikia kiwango cha kutia hofu, na hasa kwa Hong Kong na Makau ambako kuna wafungwa zaidi ya 100 wa kitanzania. Tofauti na siku za nyuma, idadi ya wafungwa wa kike inazidi kuongezeka siku hadi siku ambapo kwa sasa kuna wafungwa wa kike zaidi ya 20 katika magereza ya China bara na Hong Kong. Kutokana na hali hiyo nina wasiwasi kuwa huenda ile hadhi ya watanzania kuingia katika miji hiyo bila Visa huenda iko mashakani. Lakini vigumu kwangu kama mwandishi wa habari kujua undani wa tatizo hili. Ninachojua ni kuwa kuna watanzania wengi wako gerezani, kutokana na kukamatwa kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya.
Niliwahi kumuuliza aliyekuwa balozi wa Tanzania hapa China na balozi wa sasa kuhusu athari ya tatizo hili kwenye uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania, wote walioonesha kukasirishwa na kusikitishwa na jambo hilo, na kusema linatia aibu. Lakini mabalozi hao hawajui ni nani anayewatuma watanzania wanaokamatwa na dawa za kulevya. Waliokamatwa nao hata siku moja hawataji ni nani aliyewatuma, wao ni kama watu waliokula yamini ya kutosema lolote, hata kama wanapewa adhabu ya kifo. Hata hivyo, wafungwa wanaeleza tu kwamba “Kuna mtandao mkubwa ambao unahitaji ushirikiano mkubwa kupambana nao, zinakopelekwa na zinakotoka dawa hizo”.
Hivi karibuni tumesikia alichokifanya Dk Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, yeye anaona kuwa uwanja unaobeba jina la Mwalimu Nyerere haupaswi kuhusishwa na dawa za kulevya. Alichofanya Dk Mwakyembe pale uwanja wa ndege kwa kweli ni jambo zuri, na kama asingefanya hivyo huenda watanzania tungeendelea kuwa kizani kuhusiana na mambo yanayoweza kuwa yanaendelea katika forodha zetu. Lakini tukiangalia kwa undani tunaweza kuona kuwa, kama uhalifu huo unatokea kwenye uwanja wa ndege unaotakiwa kuwa na usalama mkali, hali ikoje kwenye forodha nyingine mbali na ile ya uwanja wa ndege wa mwalimu Nyerere ambako hakuna kamera za video, ambako Dk Mwakyembe hawezi kwenda kwa ghafla? Kuna Namanga, Holili, Horohoro, Silari, Tunduma nk, hali ya huko ikoje? Dk Mwakyembe anatakiwa kuhakikisha kuwa kilichofanyika katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere kifanyike katika forodha zote. Dk Mwakyembe analia na jina la Mwalimu Nyerere, lakini ni vizuri watanzania wote tukikumbuka kuwa tunatakiwa kulia na jina la nchi yetu, Tanzania.
Kama hali hii ikiendelea inaweza kufika hatua kuwa wanafunzi, wafanyabiashara, wanamichezo, wagonjwa na hata watalii kutoka Tanzania wanaokwenda nje ya nchi, wote watawekwa kwenye kundi la washukiwa wa biashara ya dawa za kulevya.
- See more at: http://www.fikrapevu.com/watanzania-zaidi-ya-100-wako-gerezani-nchini-china-kuhusiana-na-dawa-za-kulevya-20-ni-wanawake/#sthash.WFUZxGSe.dpuf

Thursday, August 22, 2013

MAAJABU YA DUNIA::::::::::::ANGALIA REKODI ZA DUNIA KWA NJIA YA PICHA











Star wa "Prison Break" Wentworth Miller a.k.a Michael Scofield amejiweka wazi kuwa yeye ni Shoga


Star wa "Prison Break",  Wentworth Miller  a.k.a Michael Scofield, amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga), katika barua ya wazi aliyoiandika kwenda kwa Directoe wa St. Petersburg International Film Festival (tamasha la filamu la kimataifa la St. Petersburg).


Muigizaji huyo (41) ameandika barua hiyo kukataa mualiko uliokuwa ukimtaka kuhudhuria tamasha hilo linalofanyika nchini kwao Russia na kwa mara ya kwanza kupitia barua hiyo amejitangaza kuwa yeye ni "Gay" (shoga).
"Asante kwa ukarimu wa mualiko wako, nikiwa kama mtu ambaye amefurahia kutembelea Russia kwa miaka ya nyuma na naweza pia kudai shahada ya asili ya kirusi, ningefurahi kusema ndio, hata hivyo nikiwa kama shoga (gay) lazima nikatae". amesema Miller

Miller akaendelea kusema ... nasumbuliwa sana na tabia ya sasa dhidi ya na jinsi wanavyochukuliwa mashoga na wanawake  na serikali ya Urusi.

"hali hii haikubaliki kabisa kwa namna yoyote ile , na mimi siwezi kwa dhamira nzuri kushiriki katika tukio la kusherehekea linaloandaliwa (wenyeji) na nchi ambayo watu kama mimi kwa mfumo uliopo wananyimwa haki zao za msingi za kuishi na kupenda kwa uwazi"

akamalizia kwa kusema.. kama hali hii itarekebishwa, nitakuwa huru kufanya uchaguzi tofauti.


Miller ameandika barua hiyo baada ya raisi wa Russia, Vladimir Putin kusaini sheria dhidi ya ushoga ambayo mwezi uliopita ilipitishwa sheria hiyo inayozuia mijadala aya wazi dhidi ya mahusiano ya jinsia moja popote ambapo watoto wanaweza kusikia.

Wentworth alipata umaarufu sana pale alipoigiza katika tamthilia ya "Prison Break"  2005-2009, licha ya tetesi za yeye kuwa shoga lakini alikuwa hajawahi kuthibitisha mpaka leo hii.

Wednesday, August 21, 2013

DIAMOND PLATNUMS NDANI SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA.

KWA mara ya kwanza tangu lilipoibuka sakata la watu maarufu kujihusisha ama na utumiaji au usafirishaji wa dawa za kulevya, jina la mwanamuziki anayeaminika kuwa na ukwasi mkubwa kwa sasa hapa nchini, Nasseeb Abdulmaliki, maarufu zaidi kwa jina la Diamond, limeanza kutajwa kuwa ni miongoni mwa vigogo wa ‘unga.’

Tayari mjadala mkubwa wa chini chini umeibuka kwa watu mbalimbali wakiwemo mashabiki wake, na taarifa ambazo zimelifikia MTANZANIA Jumatano kutoka vyanzo mbalimbali zimedai kuwa, mwenendo wa maisha ya Diamond sasa unachunguzwa na baadhi ya maofisa wa vyombo vya dola vya ulinzi na usalama.

Kutajwa kwa jina la Diamond katika sakata hili, kunatiwa nguvu zaidi na mwenendo binafsi wa maisha wa msanii huyo maarufu wa muziki wa kizazi kipya, unaokwenda sambamba na ukwasi mkubwa alioupata katika kipindi kifupi.

Kama hiyo haitoshi, safari za nje ya nchi za mwanamuziki huyo unaohusisha ziara zake nchini Afrika Kusini na Uingereza, pia ni mambo ambayo yamechochea wingu la mashaka lililofikia hatua ya jina lake kuingizwa katika mtandao huo ambao katika siku za karibuni, umewagusa pia baadhi ya watu wenye majina makubwa katika jamii.

Kuhusu ziara hizo, kilicholeta mshtuko na dukuduku dhidi yake ni kuwapo kwa taarifa kwamba, katika moja ya ziara hizo za nje ya nchi, Diamond alifikia hatua ya kusafiri akitumia chumba kinachotumiwa na wageni mashuhuri (VIP), badala ya njia ya wasafiri wa kawaida.

Mbali na hilo, taarifa nyingine zinaeleza kwamba, mizigo ya msanii huyo ambaye mara kadhaa amekuwa akisafiri na kundi la wacheza shoo wake, imekuwa ikipita pasipo kupitishwa katika hatua za ukaguzi kwa namna ile ile ilivyokuwa kwa mabinti wawili wa Kitanzania walionaswa nchini Afrika Kusini baada ya kuruka mfumo wa ukaguzi wa JNIA.

Aidha, ukaribu wa kimahusiano kati ya Diamond na baadhi ya Watanzania wanaoishi nchini Afrika Kusini na ambao majina yao pia yameanza kuhusishwa na biashara hiyo ya mihadarati, ni jambo jingine ambalo limechochea harakati za kufuatiliwa kwa karibu kwa nyendo za Diamond.

Taarifa zaidi kutoka JNIA zinaeleza kwamba, miongoni mwa watu wanaoweza wakawa wamemponza Diamond ni wale ambao walionekana kuwa karibu na Agness Gerald ‘Masogange’ (25) na Melisa Edward (24), siku walipokuwa wakisafiri kwenda Afrika Kusini kabla hawajanaswa katika uwanja wa Ndege wa Oliver Thambo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, wakiwa na shehena ya dawa za kulevya.

Mwenendo wa watu hao unatiliwa shaka kuwa huenda ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya wenye maskani yao nchini Afrika Kusini, kwa sababu mbali na ukaribu na wasichana hao, pia walihusika kwa karibu kuusafirisha mwili wa mwanamuziki Albert Mangwair, aliyefia huko huko Afrika Kusini ambaye taarifa za kufa kwake ziligumbikwa na matumizi ya dawa za kulevya.

Alipoulizwa jana na MTANZANIA Jumatano kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu taarifa hizo na iwapo amekwishahojiwa na vyombo vya dola baada ya jina lake kuanza kutajwa kuwa miongoni mwa orodha ya wasanii wa muziki wanaosafirisha dawa za kulevya, Diamond alikiri kuwa na pesa za kutosha kuishi maisha anayoyataka, lakini akakana kujihusisha na biashara hiyo.

Akifafanua tuhuma moja baada ya nyingine kwa mpangilio aliokuwa akiulizwa na gazeti hili, Diamond alisema katika maisha yake, hajawahi kujihusisha na utumiaji au usafirishaji dawa za kulevya, lakini madai hayo yamekuwa yakitolewa dhidi yake na watu ambao hawajui siri ya mafanikio yake.

“Kazi ngumu siku zote inalipa, sasa napata matunda ambayo yanatokana na kile nilichokifanya, iweje watu wanitilie mashaka, Watanzania ni mashahidi wangu wananiona navyochumia juani, nitaendelea kulia kivulini tu kwani nakula kwa jasho langu.

“Siyo kweli kwamba mizigo yangu haikukaguliwa na kama haikukaguliwa na ingekuwa na kasoro, basi Uingereza wangenitia hatiani, nilipita na nilikaguliwa.” Alisema Diamond.

Alipoulizwa kuhusu taarifa za kuwa mwanamtandao wa kundi la Masogange, pia alikanusha kwa kueleza kuwa hata siku aliyosafiri kwenda Afrika Kusini alikwenda peke yake uwanja wa ndege na kuongeza kuwa alikwenda huko kwa shughuli za kimuziki, ambapo safari nzima iligharimu zaidi ya Dola 30,000 za Kimarekani.

“Afrika Kusini nimekwenda kufanya kazi zangu na safari hiyo imenigharimu zaidi ya Dola 30,000, nilikwenda kurekodi nyimbo yangu mpya inayoitwa namba moja ambayo itaanza kusikika hivi karibuni.

“Unajua Watanzania sasa hivi wanajua mtu hawezi kufanikiwa au kupata maendeleo bila kuuza ‘unga’, hili si sawa juhudi za mtu ndizo zinamfikisha alipo, na mimi juhudi zangu ndio zinanifikisha hapa, watu waache kunijadili vibaya.” Alisema Diamond.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja ikiwa ni takribani miezi miwili sasa tangu Watanzania wawili, Agness Gerald ‘Masogange’ (25) na Melisa Edward (24), waliokuwa na uhusiano wa karibu na baadhi ya wanamuziki maarufu hapa nchini, kukamatwa nchini Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya Sh bilioni 6.8.

Mbali na kuwa na uhusiano wa karibu na wanamuziki, Edward anadaiwa kuwa alikuwa mfanyakazi katika mgahawa mmoja maarufu jijini Dar es Salaam, unaomilikiwa na mmoja wa vijana matajiri hapa nchini ambaye hata hivyo gazeti hili halijafanikiwa kumpata ili kufanya naye mahojiano.

Wakati huo huo, tayari hatua za kinidhamu zimekwishaanza kuchukuliwa dhidi ya wafanyakazi wa JNIA waliohusika kupitisha kilo 150 za dawa za kulevya, ambao Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ametaja majina yao hivi karibuni na kuonyesha kwa waandishi wa habari ushahidi wa kuhusika kwao.


-Mtanzania

Tuesday, August 20, 2013

picha DIAMOND ni utata mtupu alimlenga nani soma maoni ya wadau.....

Mashabiki wa Diamond Platnumz hawajaipenda picha yake inayomuonesha akionesha kidole cha kati aka ‘the middle finger’.

“Is this the right finger that you are talkin about @roma2030 …?” ameandika kwenye picha ya Instagram aliyopiga na rapper Roma Mkatoliki


Hata hivyo picha hiyo imevuta hisia za mashabiki wenye hasira waliomwangushia mvua ya madongo kwenye Instagram ambapo ana followers zaidi ya 36,100 hadi sasa. 

Hizi ni baadhi ya comments:
 
Mafuruzenkonoki: Umekua sasa hivi kijana, hizo ishara haziendani na ulivyo! Change! 
 
Lugnno: Umeimba wimbo ma mc mara matus mara bang umekuwa mc naona inshara ya tus kwenye kdole cmon usizd sana hta km upo mbal utakosea km wkt ule ulvua surual takecare man sijaipenda 
 
luvcartel: Astaghafurullah… juzi ulikua muislam leo ushakua kafir? Subhannallah
 
ladisdallaz: The middle finger? To u nt to us 
 
mmolezson: Diamond n Roma nyie wote wajinga tu, mtu yeyote mwenye akili timamu and rational awez point finger lik dat then anapoist kwenye social networks ili jamaa waone.

Alice_aswile: Aah hapana diamond,hivyo vitu hapa cio mahali pake loh,hivyo mfanyie demu wako gheto. 
 
Makitoti: Ain’t ryt diamond ….just ain’t ryt, we love ur music Ila that pic!!!!naaaah,haifai
Mmolezson:
Kwa hyo hcho kidole mnatuoneshea sis ee, hv unawakumbka wasanii hpa Tz ambao walikuwa maaruf kulko nyie? Je saiz wko wp ee na wala hawakuwa na tabia za limbuken kma ww free lancer. I hate u mother***

 
Trofmo: Very disappointin… Ww km Kioo cha jamii unataka tuelewe vip hii picha?! Plz dis z Tz not states! Our culture is decency & dignity!!! Behave..
 
Chocolatedesweetness: This is too much……..!!! Umeanza kulewa mafanikio eeenhe, ngozi nyeusi taaabu sana, U better apologise and delete this photo before its too late!U shauri tu

FAIDA ZA KUFANYA MAPENZI


 1. Mwili kukingwa na kupata mafua ya marakwa mara kwasababu ya kinga mwili inayopambana na maambukizi itwayo imunoglobini A

2. Wanawakehupata mzunguko wa hedhi usiyobadilika badilika kwasababu ya kupata homoni maalumu za mwanaume zittwazo filemoni.

3. Mwili kuwa imara kupambana na msongo wa mawazo.

4. Kushusha mapigo ya moyo yaliyo juu, hii hukufanya ujiepushe na kupata magonjwa ya moyo.

 5. Kuondoa mafuta yenye madhara mwilini na kutengeneza mafuta yenye manufaa mwilini.

 6. Kuteneneza muonekano mzuri wa misuli ya mapajani namwili kwa ujumla.

7. Kuongeza homoni ya kike itwayo istrojeni, hii humfanya mwanamke kuwa mrembo.

 8. Huongeza uwezo wa kutunza kumbukumbu kwenye ubongo, kwasababu ya mzungumko mzuri wa damu wakati wa kufanya mapenzi

9. Huongeza morali ya kazi na kufanya kujisikia vizuri kimawazo.

 http://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/507422-faida-za-kugegedana-hizi-hapa.html

Dalili za mwanaume anayekupenda kwa Dhati


ANAVYOKUTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana kuliko wasiopendana, ambao kiwango chao ni asilimia 30-50.

Hii ina maana kwamba mwanaume anapotumia muda wake mwingi kumtazama msichana na kugeuka taratibu kuangalia vitu vingine kama mtu asiyependa kuacha kumwangalia, ujue anampenda.

MIPANGO
Mwanaume anayekupenda atakushirikisha kwenye mipango yake hasa ya muda mrefu. Mfano akitaka kununua kiwanja, kujenga nyumba atakuambia na pengine kutaka mchango wako wa hali na mali katika kulifanikisha hilo. Ukiona mwanaume anakuficha mambo yake, tambua kuwa huyo ana walakini kwenye penzi la dhati na la muda mrefu.

ATAONESHA HUZUNI
Katika maisha ya mapenzi kuna wakati wa kuhuzunika. Mwanaume mwenye upendo wa dhati atashirikiana nawe wakati wa huzuni na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa unapata furaha.

ATAKUAMINI
Dalili nyingine ya kupendwa na mwanaume ni kuaminiwa kwenye maisha kwa ujumla. Yaani mwanaume anayekupenda hatakuficha kitu, mfano pesa zake, atakupa uhuru kwenye simu yake na kukuamini katika usimamizi wa miradi yake.

ATAKUPA NAFASI
Ninapozungumzia nafasi nina maana atakukaribisha kwake bila hofu na kukupa nafasi ya kuingia na kutoka bila mipaka, atakupa nafasi ya kuweka vitu vyako kwenye kabati na kuruhusu nguo, picha na vitu vyako kuonekana wakati wote chumbani kwake.

UTAKUWA MWANAFAMILIA
Mwanaume aliyefikia chaguo la mwisho kwa mwanamke humshirikisha mpenzi wake kwenye masuala yake ya kifamilia, mfano atamwalika kwenye vikao vya harusi, kipaimara, atatoa nafasi ya kuambatana naye kuona wagonjwa, kusalimia ndugu na atakuwa huru kukutambulisha kwao.

ATAZUNGUMZA NAWE KUHUSU WATOTO
Kwa kuwa wanaume wengi hufikiria kuwa na familia, mwanaume anayekupenda atazungumza nawe mipango ya kupata watoto kwa kuwa atakuwa amekuchagua wewe kuwa mama wa wanaye na atapenda mazungumzo hayo.

ATAKUSAIDIA
Kwa kuwa kukwama ni sehemu ya maisha yetu, mwanaume anayekupenda atakuwa tayari kukusaidia unapokwama. Kila mara atahakikisha kuwa unakuwa na mafanikio na yeye atakuwa tayari kukupunguzia usumbufu wa maisha, kwa kukufuata kazini, kukusaidia baadhi ya mambo na hata ya nyumbani.

ATAJITOLEA
Ninaposema kujitolea ninamaanisha atakuwa tayari kufanya mambo yako na kuyaweka yake nyuma. Kwa mfano akiwa anapenda mpira na siku hiyo kuna mechi, lakini muda huo ukamwambia akufuate kwa mjomba wako atakuwa tayari kuacha furaha yake na kukujali wewe. Huyu ni mwanaume anayekupenda kwa dhati.

ATAAMBATANA NAWE
Wapenzi wengi wasiokuwa na mapenzi ya dhati huona aibu kuambatana na wapenzi wao kwenye mikusanyiko ya watu, lakini mwanaume anayekupenda atafurahia kutoka moyoni kuongozana nawe kwenye halaiki ya watu na kufurahia uwepo wako bila kuona aibu.

Monday, August 19, 2013

MZIGO MPYA "HTC" HUU HAPA

HTC has just launched an Android 4.2.2 Jelly Bean update with its Sense 5 user interface for the HTC One X. For now, only the unlocked European version of the smartphone can benefit from the update, but the rest of the One X owners should get it in the coming weeks.

With Android 4.2.2 and Sense 5 UI, the HTC One X gets features like Blinkfeed, Lockscreen widgets, as well as the Quick settings panel. The latter brings access to 12 different settings with a single swipe. Another user interface enhancement, albeit minor, is the battery level percent indicator next to the battery icon in the status bar.
The gallery app has been also overhauled with video highlights, which come with 12 different themes. There's also auto exposure and autofocus lock available in the camera app. Lastly, the music app enjoys the got visualization with live lyrics.
The Android 4.2.2 update for the HTC One X weighs at 380 megabytes and brings the software version of the device to 4.18.401.2.
HTC has been launching quite a lot of updates for its Android smartphones this summer. Just the week before, the company issued the very same update for the HTC One X+. In July, the company started seeding Android 4.2.2 for its flagship HTC One, and just a day after that the Butterfly got the Android 4.2.2 treatment.

Mtawa wa kanisa katoliki avamiwa na kujeruhiwa huko zanzibar


MTAWA wa Kanisa Katoliki la Bububu visiwani Zanzibar, Sister Irene Ludovik Mwenda (34), amevamiwa na watu wasiojulikana na kushambuliwa na marungu, hali iliyomsababishia maumivu makali mwilini. Sakata la mtawa huyo lilitokea jana, baada ya kuvamiwa na vijana wapatao kumi, baada ya mtawa huyo kuwa anafuga mbwa ambaye inaelezwa kuwa alikula kuku wa mmoja wa vijana hao.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 11 jioni, jirani na maeneo ya Kanisa la Kigango cha Mtakatifu Thesia Beit –el-rus, katika nyumba wanazoishi watawa wa kanisa hilo.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini na Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtu huyo aliyepigwa ni mwanamke ambaye ni mtumishi wa Kanisa Katoliki la Bububu, Zanzibar.

Kamanda Mkadam, alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliosababishwa na tuhuma za mbwa wa mtawa huyo kuwa amekula kuku wa kijana huyo, ambapo baada ya majibizano kijana huyo alipata jazba, hali iliyosababisha kumpiga ngumi mtawa huyo.

Kamanda huyo alisema kuwa baada ya kutokea tukio hilo, mtawa huyo alikwenda kufungua jalada la malalamiko katika Kituo kidogo cha Polisi cha Beit-el-rus, kuhusu kupigwa kwake na kijana huyo.

“Tupo tunaendelea na uchunguzi juu ya tukio hili, kwani ni ugomvi wa mitaani unaweza kuleta athari kubwa zaidi, lazima tufanye kazi hii kwa umakini zaidi,” alisema Kamanda Mkadam.

Hata hivyo alisema kuwa Jeshi la Polisi linamshikilia kijana huyo kwa ajili ya mahojiano zaidi, ili kujua sababu za kushambuliwa kwa mtawa huyo ambapo mpaka sasa yupo mikononi mwa polisi.

Alisema baada ya kesi hiyo kufikishwa polisi, wazazi wa kijana huyo walifanya juhudi za kuzungumza na mtawa Irene ili kuweza kufikia maridhiano na kijana huyo na pindi wakishindwa kuelewana, shauri lao litafikishwa mahakamani.

Hata hivyo kutokana na makubaliano hayo, mtawa huyo alikubali kumsamehe kijana huyo, huku polisi ikisema kutokana na sababu za kisheria na usalama, kijana huyo hataachiwa na jalada la kesi limepelekwa katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, ili atoe ushauri kuhusu sakata hilo.

KAMA ULIPANDA MBEGU SHAMBA LA "DECI" UTARUDISHIWA.......




MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imewahukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya sh milioni 21 vigogo wanne wa iliyokuwa Kampuni ya Development Entrepreneurship for  Community Initiative (DECI ).
  Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Alocye Katemana, pamoja na adhabu hiyo pia ameiagiza serikali ifanye mchanganuo wa mali za DECI ambazo inazishikilia, kwa kuwa zipo mali zilishikiliwa zisizo za kampuni hiyo bali za watu wengine.

Alisema kuwa fedha za wateja wa DECI walizopanda zirejeshwe kwa wateja wenyewe ambao wataonesha uthibitisho wa kweli kuwa walipanda fedha zao huko.
 
Katika hukumu hiyo iliyotolewa na Hakimu Mkazi, Stewart Sanga na kusomwa na Hakimu Katemana, washitakiwa walikuwa watano, ambao ni Jackson Mtares, Dominick Kigendi, Timotheo ole Loitginye, Samwel Mtares na Arbogast Kipilimba.
 
Washitakiwa hao walikuwa wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Hudson Ndusyepo na Onesmo Kyauke.
 
Hakimu Katemana alisema washtakiwa hao ambao ni wachungaji wa makanisa ya Pentekoste wametiwa hatiani kuanzia wa kwanza hadi wa nne, isipokuwa mshtakiwa wa tano ndiye ameachiliwa huru baada ya mahakama kumuona hana hatia katika makosa hayo mawili.
 
“Mahakama imeridhika kuwa upande wa Jamhuri uliokuwa unawakilishwa na Wakili wa Serikali, Prosper Mwangamila na Justus Mulokozi, umeweza kuthibitisha kesi yao na kwa maana hiyo mahakama inawatia hatiani washitakiwa hao wannne na kumwachilia huru mshitakiwa mmoja, kwa sababu mashitaka dhidi yake Jamhuri imeshindwa kuyathibitisha,” alisema.
 
Alisema katika kosa la kwanza kila mshitakiwa atapaswa alipe faini ya sh milioni tatu au kwenda jela miaka mitatu, na katika kosa la pili kila mshitakiwa atatakiwa alipe faini ya sh milioni 18 au kwenda jela miaka mitatu na kwamba mshitakiwa atakayeweza kulipa faini ataachiliwa huru.
 
Kabla ya hukumu, Hakimu Katemana, aliwapatia nafasi mawakili wa pande zote mbili kuzungumza chochote, ambapo Wakili wa Serikali, Mwangamila, alieleza kuwa washitakiwa ni wakosaji wa mara ya kwanza na kwamba makosa waliyoyatenda yana madhara katika uchumi wa nchi, hivyo akaomba wapewe adhabu kali.
 
Wakili wa washitakiwa, Ndusyepo, alidai kuwa wateja wake ni mara yao ya kwanza kutenda makosa hayo ambayo waliyatenda wakati wakiwa katika harakati za kuwakwamua waumini wao katika lindi la umaskini.
 
Aliomba mahakama isiwapatie adhabu kali kwani wateja wake hawana uwezo wa kulipa fidia, ikizingatiwa kuwa wengine ni wastaafu na hawana huwezo wa kifedha.
 
Jana saa 7:00 mchana, Wakili Ndusyepo aliliambia gazeti hili kuwa tayari ndugu wa Domick na Mtares walikuwa wakielekea benki na ofisa wa mahakama kwenda kulipa faini ili waweze kukwepa adhabu ya kwenda jela.

Juni 12 mwaka 2009, washitakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza, baada ya vuta nikuvute kati ya viongozi na wanachama wa DECI .

Wakili Mwangamila alidai washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka mawili ambayo ni kuendesha na kusimamia mradi wa upatu kinyume cha kifungu 111A (1,3) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16.
 
Alidai kuwa, kati ya mwaka 2007 na Machi 2009, katika makao makuu ya DECI , yaliyopo Mabibo Mwisho, jijini Dar es Salaam, washitakiwa waliendesha na kusimamia mradi wa upatu katika sehemu tofauti nchini, kwa ahadi ya kuwapa wanachama wao fedha zaidi ambazo katika mazingira ya kibiashara ni kubwa kuliko mradi waliokuwa wakiufanya.
 
Mwangamila alidai kuwa, shitaka la pili ni kupokea amana za umma bila kuwa na leseni, kinyume cha kifungu cha 6 (1,2) cha Sheria ya mabenki na Taasisi za Fedha Na. 5 ya mwaka 2006 na kwamba, washitakiwa wote katika kipindi hicho wakiwa kwenye ofisi zao za DECI , walipokea amana kutoka kwa umma bila leseni.

-Tanzania daima

SIRI ZA TRAFIKI FEKI ZAFICHUKA,YADAIWA ALIANZA KAZI MKOANI SINGIDA,AKAJIPA UHAMISHO WA KIKAZI HADI DAR...!!

SIKU chache baada ya kukamatwa kwa askari 'feki' wa Usalama Barabarani mwenye cheo cha Sajini, akifanya kazi ya kuongoza magari eneo ya Tabata Kinyerezi, Dar es Salaam, mambo mapya yamezidi kubainika juu ya sababu za mtu huyo kujiingiza katika kazi hiyo bila kutambuliwa na Jeshi la Polisi.


Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vya kuaminika, zinasema trafiki huyo 'feki', ambaye inadaiwa jina lake halisi ni James Juma Hussein (45), mkazi wa Kimara Matangini, alianzia kazi hiyo mkoani Singida kabla ya kujipa uhamisho wa kikazi kwenda Dar es Salaam.

Chanzo chetu kilieleza kuwa, trafiki huyo alikuwa na shemeji yake aliyeitwa Shaban ambaye aliajiriwa na Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani aliyekuwa akifanyia kazi mkoani Tabora.Vyanzo vyetu viliongeza kuwa, baada ya shemeji yake kufariki mkoani Tabora, trafiki huyo alipata mwanya wa kuchukua nguo za kazini alizokuwa akizitumia shemeji yake.



Inadaiwa trafiki huyo 'feki', aliwahi kupata mafunzo ya upolisi katika Chuo cha Polisi Moshi (CCP), mkoani Kilimanjaro lakini alifukuzwa.Chanzo hicho kiliongeza kuwa, baada ya ndugu wa trafiki huyo kufariki dunia, trafiki 'feki', alikuwa akifanya kazi hiyo bila ndugu zake kujua akianzia mkoani Singida bila kushtukiwa.

"Jamaa aliamua kujirithisha kazi ya shemeji yake, alikwenda Singida na kufanya kazi hiyo kwa muda usiojulikana," kilisema chanzo chetu.Chanzo hicho kiliongeza kuwa, kutokana na uchache wa matrafiki mkoani Singida, aliingiwa hofu ya kuweza kujulikana; hivyo aliamua kujipa uhamisho wa kwenda jijini Dar es Salaam.

"Akiwa Dar es Salaam, alifanya kazi hii kwa muda mrefu bila kujulikana hadi alipokamatwa wiki iliyopita akiwa eneo lake la kazi akiongoza magari," kilisema chanzo hicho.Mtoa habari huyo alisema polisi walianza kumtilia shaka trafiki huyo kutokana na adhabu zake alizokuwa akizitoa kwa madereva.

"Tulianza kuwa na hofu naye kwa sababu yeye adhabu zake kwa kila dereva aliyekuwa akimkamata alimtoza sh. 20,000 hadi 25,000," kilieleza chanzo hicho.Sababu nyingine iliyowafanya polisi wamtilie shaka ni utamaduni wake wa kuondoka mapema kwenye kituo cha kazi ambavyo alikuwa akijipangia mwenyewe.

"Trafiki akiwa kazini, inabidi awe kituoni kwake kuanzia asubuhi hadi jioni muda wa kazi unapomalizika, tulishangaa kuona mwenzetu anaingia kazini asubuhi na kuondoka kabla ya muda wa kazi," kiliongeza chanzo hicho.Inadaiwa trafiki huyo alikuwa akifanya hivyo baada ya kukamilisha mahesabu yake aliyokuwa amejiwekea ambapo hali hiyo iliwafanya polisi waanze kujiuliza maswali na ndipo walipoanza kumfuatilia.

Baada ya kufuatiliwa bila yeye kujua, walibaini hata upigaji wake wa saluti ni utata mtupu ambapo kutokana na hali hiyo, waliweka mtego na kufanikiwa kumkamata.
Hadi sasa anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi ambalo limeahidi kutoa taarifa kamili baada ya uchunguzi wao kukamilika

JAMAA ALIYE WATOROKA KINA MASOGANGE SOUTH AFRICA SOON BAADA YA KUKAMATWA.......

Waziri wa uchukuzi Prof. Harrison Mwakyembe alimtaja mshukiwa mmoja wa dawa za kulevya aitaye Nassoro Mangunga  na  kuwataka  polisi  wamtie  nguvuni  popote  atakapoonekana....

Hata  hivyo, mshukiwa huyu pamoja na picha zake alishaandikwa na gazeti la SANI katika toleo lake la Agosti 7-9, 2013 (toleo la 1042) pamoja na namna alivyosafirisha mzigo pamoja na akina Masogange.

Hii  ni  taarifa  ya  gazeti  hilo:


Unaweza kukimbia lakini huwezi kujificha. Msemo huu unaonekana kutimia kwa kijana anayedaiwa kuambatana na watuhumiwa wa dawa za kulevya waliokamatwa Julai 5 mwaka huu nchini Afrika Kusini, Agness Gerald 'Masogange' (25) na Melisa Edward (24), kunaswa na gazeti hili.

 
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, wasichana hao, Masogange na Melisa walisafiri ndege moja na kijana anayejulikana kwa jina la Nassoro Mangunga wakitoka Dar es Salaam kwenda Afrika Kusini, wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), yenye namba SA 189.


Wakiwa katika ndege hiyo Mangunga, Agness na Melisa walikaa kwenye viti vilivyo jirani kabisa huku Mangunga akiwa katikati yao, kwani Agness alikaa kiti namba 23B, Mangunga alikaa kiti namba 23D na Melisa alikaa kiti namba 23A.


Mangunga ambaye ni rafiki mkubwa wa wanamuziki wa Bongo Flava, Rashidi Abdallah Makwiro 'Chid Benz', Mgaza Pembe 'M2theP' na Albert Keneth Mangweha 'Mangwair', wakati akisafiri na mabinti hao walikuwa na jumla ya mabegi tisa kama kumbukumbu za nyaraka za shirika hilo la ndege zinavyoainisha.


Licha ya nyaraka za kusafirishia mabegi hayo kuonesha jina la Agness Gerald ambaye ni mpenzi wa Mangunga tangu mwanzoni mwa mwaka jana, kuwa ndiye aliyelipia mabegi hayo, ila kwenye sehemu ya anuani ya waraka pepe, imeandikwa  Mangunga.


Aidha, mabegi hayo, yalikuwa na kilo 150 za dawa za kulevya lakini kila mmoja alitakiwa kusafiri na kifurushi cha kilo ishirini kama mzigo wa mkononi ambao husafiri bila malipo, hivyo watatu hao kwa pamoja walikuwa na kilo sitini wote kwa pamoja, hivyi kubaki kilo 90 ambazo walizozilipia Dola za Marekani 94 badala ya Dola 450.


Mangunga ambaye licha ya kuishi zaidi nchini Afrika Kusini, lakini pia ni mkazi wa maeneo ya Ilala jijini Dar es Salaam.


Agness na Melisa, walikamatwa Julai 5, 2013 katika Uwanja wa Ndege wa Oliver Thambo, Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya zenye uzito wa kilo 150 aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya Sh bilioni 6.8 za Kitanzania, na walipotiwa mbaroni, walikuwa na mabegi sita tu kati ya tisa waliyokuwa nayo wakati wanapanda ndege jijini Dar es Salaam.


Inasemekana mabegi hayo matatu yaliondoka na Mangunga na kutokomea kusikojulikana....


Mpekuzi blog